Makamu wa RAIS wa Seneti ya Jumuiya (SMAUJATA) shujaa wa maendeleo wa ustawi wa Jamii Fredrick Nelson Rwegasira amechukua fomu ya kutia nia ya kugombea Ubunge Jimbo la Kivule. Rwegasira amechukua fomu hiyo leo Julai 1,2025 katika Ofisi za Katibu wa CCM Ilala Chief Sylvester Yaredi. Aidha amesema kwamba amejipima na kujitambua kua anafaa kugombea nafasi hiyo kwa ajili ya kuwaletea maendeleo wananchi wa Kivule.
Katibu wa Shina na mwanachama wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM,( UWT) Kigezi chini Kata ya Buyuni, Happyness Malya amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea Udiwani wa Viti Maalumu Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Amekabidhiwa fomu hiyo leo June 30,2025 na Katibu Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) Wilaya ya Ilala Rosemary Mwakisalu Ofisini kwake Ilala
Na Mwandishi wetu Wananchi wametakiwa kujitokeza kwa wingi kutembelea mabanda ya maonesho ya pili ya huduma za kifedhanq kijamii 'Muharram Expo 2025' yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam Kiongozi Mwandamizi wa Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Mohamed Issa, amesema maonesho hayo ni ishara ya kuingia mwaka mpya wa Kiislamu ambao ni Muharram sawa na mwezi wa kwanza wa kiislamu Hijiria. Amesema kuwa, katika maonesho hayo kutakua na mada mbalimbali ambazo zitatolewa kwa wananchi na wataweza kupata elimu kuhusu uwekezaji ambao hauna riba na watapata elimu namna ya kuweka akiba, kupata mikopo au uwezeshwaji usio na riba. Pia amesema wananchi watapewa elimu kuhusu huduma za Masoko ya mitaji na dhamana na uwekezaji wa pamoja (Collective Investment Schemes) isiyo na riba kama vile mifuko ya Uwekezaji Halal au Halal Fund, hati fungani zisizo na riba inayofahamika kama Sukuk. Aidha, katika Maonyesho h...
Comments
Post a Comment