Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2026

TMA NA EMEDO WAJA NA TUNZO ZA WAANDISHI WA HABARI

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania(TMA) kushirikiana na Shirika la Usimamizi wa Mazingira na Maendeleo (EMEDO) limeungana kuanzisha kutoa tuzo za waandishi wa habari wanaoelimisha jamii kuhusiana na changamoto, matukio ya hali mbaya ya hewa na tahadhari zitokana na usalama kwenye maji. Afisa Uchechemuzi kutoka Shiriki la Usimamizi wa Mazingira na maendeleo(EMEDO) Mary Francis Mahemba amesema, wametambua mchango unaofanywa na vyombo vya habari kuwa ni muhimili muhimu katika kuifikia jamii kutoa taarifa sahihi zitakazoweza kuokoa maisha, kupunguza athari za majanga yanayohusianana hali ya hewa pamoja na kuimarisha uelewa wa jamii kuhusu usalama wa majini. Amefafanua tuzo hizo zinalenga kuhasamasisha utayarishaji wa habari zenye ubora kuhusu matukio ya hali mbaya ya hewa na athari zake kwa jamii, tahadhari za mapema za hali ya hewa, usalama wa vyombo vya usafiri na usafirishaji kwenye maji, uzuiaji wa ajali na vifo vitokanavyo na kuzama maji, pamoja na ustahimilivu wa jamii dhidi ya majanga...

TMA YAITAKA JAMII KUCHUKUA TAHADHARI

Ayra Nwestz Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini (TMA) imeishauri jamii kuchukua hatua stahiki za kiafya ili kujikinga na magonjwa yanayoweza kusababishwa na mabadiliko hali ya hewa ya baridi na vumbi. Ushauri huo umetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Ladislaus Chang'a, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelezea mwelekeo wa hali ya kipupwe katika kipindi cha mwezi Juni hadi Agosti (JJA) mwaka huu. Aidha Dkt. Chang'a pia amewashauri wafugaji kuendelea kuzingatia ratiba za kuogesha mifugo ili kudhibiti visumbufu na magonjwa pamoja na kufuata ushauri wa wataalamu, na maji na malisho yanapaswa kutumika kwa uangalifu ili kupunguza athari zinazotarajiwa. Sambamba amewashauri wakulima kulima kwa kuzingatia ushauri wa maafisa ugani katika maeneo yanayotarajiwa kupata vipindi vya mvua katika kipindi hiki cha msimu wa kipupwe. "Kwa watumiaji wa bahari, taarifa hii itasaidia kupunguza athari za upepo unaotarajiwa. Pia, sekta za ujenzi, madini na uchukuzi zinatarajiwa kunufaika ...

TMA YATOA ELIMU YA HALI YA HEWA KWA WAVUVI KUPITIA MRADI WA ECOFISH

Pemba, 20 Mei 2026 Mradi wa ECOFISH unaotekelezwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Denmark kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Shirika la Denmark la Maendeleo ya Kimataifa (DANIDA), unaendelea kuboresha shughuli za uvuvi kwa jamii ya Pwani na kuimarisha huduma za tahadhari za mapema za hali ya hewa nchini. Katika utekelezaji wa mradi huo, wataalamu kutoka TMA walikutana na wavuvi pamoja na wakulima wa Mwani kwa lengo la kujionea hali halisi ya shughuli zao za kiuchumi na changamoto zitokanazo na mabadiliko ya hali ya hewa  wanazokabiliana nazo, sambamba na kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa katika shughuli za uvuvi na kilimo cha Mwani. Ziara hiyo iliambatana na semina maalum iliyowakutanisha wavuvi na wakulima wa Mwani ikiwa ni sehemu ya juhudi za mradi huo katika kuongeza uelewa wa jamii kuhusu umuhimu wa matumizi ya taarifa za hali ya hewa katika kufanya maamuzi sahihi na salama. Akizungumza katika semina hiyo, Mtaalamu wa H...

NLD YAMPONGEZA MSAJILI, DOYO ATAKA UWAJIBIKAJI WA KISIASA KWA VYAMA VYOTE BILA UBAGUZI

  TANGA -  Chama cha National League for Democracy (NLD) kimesema hatua ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kuvitaka vyama vya CCM na CHADEMA kutoa maelezo kuhusu kauli za baadhi ya viongozi wao ni ishara ya usimamizi wa haki na usawa kwa vyama vyote vya siasa nchini. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Tanga leo, Katibu Mkuu wa NLD, Doyo Hassan Doyo, alisema uamuzi huo unaonyesha kuwa sheria na taratibu za kisiasa zinaweza kutekelezwa kwa usawa bila kuangalia ukubwa au nguvu ya chama husika. Doyo alieleza kuwa hatua ya Msajili kuviandikia barua vyama hivyo viwili imeondoa hisia za upendeleo ambazo zimekuwa zikijitokeza mara kwa mara katika utekelezaji wa sheria zinazohusu vyama vya siasa. Aliongeza kuwa utekelezaji wa sheria kwa usawa unasaidia kuimarisha imani ya wananchi kwa taasisi zinazosimamia mfumo wa kisiasa pamoja na kudumisha misingi ya haki, uwajibikaji na utawala wa sheria. Pamoja na hayo, NLD limewataka viongozi wa kisiasa pamoja na wanachama wa vyama mba...

MD TWANGE AELEZA KUTORIDHISHWA NA KASI YA MKANDARASI WA MRADI WA HALE

Ni ule wa kuboresha kituo cha kufua umeme  Amuagiza kuongeza kasi ya utekelezaji wa Mradi huo Na Mwandishi Wetu, Korogwe, Tanga Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Bw. Lazaro Twange ameeleza kutoridhishwa na kasi ya mkandarasi anayetekeleza mradi wa maboresho ya Kituo cha Kufua Umeme cha Hale kutokana na kuchelewa kukamilika kwa Mradi huo ulioanza kutekelezwa tangu mwaka 2022. Bw. Twange ameyasema hayo leo Aprili 22, 2026 wakati wa ziara yake ya ukaguzi katika mradi wa Hale pamoja na mradi wa usafishaji wa bwawa la Mto Pangani iliyopo katika Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga ambapo amemtaka mkandarasi wa Mradi wa Hale kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi huo ikiwa ni pamoja na kuongeza wafanyakazi pamoja na muda wa kufanya kazi ili ukamilike kwa wakati. “Siridhishwi sana na mwenendo wake. Mkandarasi amewahi kuomba nyongeza ya muda mara mbili na nimepata taarifa kuwa yuko kwenye hatua za kuomba nyongeza nyingine ya tatu. Ndio maana nimekuja kuona kuna nini,” amesema Bw. Twange. Amesema mra...

SALOME: NGUZO ZA ZEGE NA CHUMA KUTUMIKA KUKABILI CHANGAMOTO YA KUANGUKA KWA NGUZO ZA UMEME ZA MITI.

  NAIBU Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amesema Serikali kupitia TANESCO inaendelea kubadilisha nguzo chakavu kwa kuweka nguzo imara zaidi, zikiwemo nguzo za zege na chuma, pamoja na kuimarisha misingi ya nguzo katika maeneo yenye udongo laini ili kukabili changamoto ya kuanguka kwa nguzo za umeme. Salome ameeleza hayo leo, Mei 22, 2026, Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mhe. Sara Msafiri Ally, Mbunge wa Mvomero, aliyetaka kujua ni lini Serikali itatatua changamoto ya kuanguka kwa nguzo za umeme katika Tarafa ya Mgeta. Akijibu swali hilo, Salome amesema Serikali inatambua uwepo wa changamoto ya kuanguka kwa nguzo za umeme katika baadhi ya maeneo ya Tarafa ya Mgeta kutokana na sababu mbalimbali, ikiwemo mvua nyingi, uwepo wa udongo usiohimilivu pamoja na uchakavu wa baadhi ya nguzo. Amesema Serikali kupitia TANESCO inaendelea kufanya ukaguzi wa mara kwa mara wa miundombinu ya umeme ili kubaini na kushughulikia changamoto hizo mapema pindi zinapojitokeza. Aidha, Sa...

WAZIRI WA NISHATI NDEJEMBI AKUTANA NA BALOZI WA NORWAY

Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Mhe. Tone Tinnes yaliyolenga kuimarisha na kuendeleza ushirikiano kati ya nchi hizo mbili katika sekta ya nishati. Mazungumzo hayo yamefanyika leo Mei 22, 2026 katika Ofisi  Ndogo za Wizara ya Nishati zilizopo jijini Dar es Salaam. Viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ikiwemo mashirikiano ya kimkakati katika uendelezaji wa gesi, umeme, nishati jadidifu pamoja na kubadilishana uzoefu wa kitaalamu  na juhudi za kukuza sekta ya nishati kwa nchi hizo mbili. Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Kamishna wa Mafuta na Gesi kutoka wizara ya nishati, Bw. Goodluck Shirima, Mkurugenzi wa Maendeleo na Uzalishaji kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Bw. Paschal Njiko pamoja na wataalamu wengine.

BANDARI YA MBAMBA BAY KUFUNGUA FURSA MPYA ZA BIASHARA YA MAFUTA UKANDA WA KUSINI

  Na Mwandishi Wetu Ujenzi wa Bandari ya Mbamba Bay unatarajiwa kuchochea kwa kiasi kikubwa biashara ya mafuta katika ukanda wa Kusini na kufungua njia mpya za usafirishaji wa bidhaa hiyo kuelekea nchi jirani kupitia miundombinu ya kisasa inayojengwa eneo hilo. Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa bandari hiyo, Meneja wa Mipango ya Mafuta wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), Gilbert Jungulu, amesema mradi huo una nafasi ya kuifanya Tanzania kuwa kitovu muhimu cha usambazaji wa mafuta kwa nchi za Malawi, Msumbiji na maeneo mengine ya ukanda huo. Amesema PBPA itaendelea kuratibu uagizaji wa mafuta nchini pamoja na kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha miundombinu muhimu ya mafuta, ikiwemo maghala ya kuhifadhia mafuta, inajengwa na kuimarishwa ili kurahisisha biashara ya kikanda. “Endapo maghala ya kuhifadhia mafuta yatakamilika hapa Mbamba Bay, itakuwa rahisi meli kushusha mafuta kwa ajili ya kuhifadhiwa na baadaye kusafirishwa kwenda nchi j...

TANESCO YAENDELEA KUWAELIMISHA WANAOFANYA SHUGHULI ZA KIUCHUMI KWENYE MIUNDOMBINU YA UMEME

  Ni katika muendelezo wa ukaguzi wa miundombinu ya umeme Dar es salaam Yatoa rai kwa wananchi kuondoka kwa ajili ya usalama wa maisha na mali zao Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeendelea kuwasisitiza wananchi wanaofanya shughuli zao za kiuchumi katika miundombinu ya umeme kuondoka katika maeneo hayo kwa hiari, kwa kuwa wanahatarisha usalama wa maisha na mali zao. Akizungumza katika muendelezo wa zoezi la kukagua miundombinu ya umeme Mei 18, katika eneo la Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam, Msimamizi Msaidizi wa Njia Kuu za Kusafirisha Umeme Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Nicholaus Kivelege, amesema TANESCO inafanya jitihada za makusudi kutoa elimu kuhusu athari za kuendelea kufanya shughuli za kiuchumi chini ya njia kubwa za kusafirisha umeme katika maeneo mbalimbali nchini. Amesema licha ya jitihada hizo, bado baadhi ya wananchi wanaendelea kufanya shughuli hizo, hivyo amewaomba viongozi wa serikali za mitaa katika maeneo husika kuongeza nguvu ya kutoa elimu kuhusu madhara y...

TFS YATAKA VIWANGO VYA UBORA VILINDWE KATIKA BIASHARA YA ASALI

  Tabora, Mei 21, 2026 Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umewataka wananchi wanaojihusisha na ufugaji nyuki na uchakataji wa mazao yatokanayo na nyuki kuzingatia viwango vya ubora na usalama wa bidhaa zao, ukionya kuwa uzalishaji usiozingatia sheria unaweza kuhatarisha masoko ya ndani na nje ya nchi. Tahadhari hiyo ilitolewa leo na Meneja wa Rasilimali Nyuki wa TFS, SACC Hussein Msuya, wakati wa majadiliano ya biashara kwa biashara na mdahalo kuhusu maendeleo ya sekta ya ufugaji nyuki nchini, uliofanyika katika Viwanja vya Kumbukumbu ya Vita mkoani Tabora kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Nyuki Duniani. SACC Msuya alisema Tanzania imeendelea kujijengea sifa kimataifa kutokana na ubora wa mazao yake ya nyuki, hususan asali na nta, lakini akasisitiza kuwa ubora huo unaweza kupotea iwapo wafugaji na wachakataji hawatazingatia viwango vilivyowekwa na mamlaka husika. “Utumiaji wa vifungashi bora ni takwa la kisheria na unasimamiwa na sheria ya viwango. Kwa mujibu wa kan...

DIWANI JESCA MAHMOUD MSOLLA AZINDUA KLINIKI YA VYETI VYA KUZALIWA BUYUNI

  Na AyraNewstz DIWANI wa kata ya Buyuni   Wilayani Ilala Mkoa Dar es Salaam, JESCA MAHMOUD MSOLLA, amezindua Kiliniki ya vyeti vya kuzaliwa kata ya Buyuni kwa ajili ya kuwasogezea wananchi huduma za kijamii karibu na makazi yao.  Kampeni hiyo ya kutoa vyeti vya kuzaliwa  ambayo itakuwa wa siku kumi kutoa huduma ofisi za Afisa Mtendaji wa kata ya Buyuni ilianza Mei 13 itaendelea mpaka Mei 24 mwaka huu . Akizungumza kwa niaba ya Diwani wa Buyuni, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Buyuni ,Sylvanus Benard Mwenda ,alisema zoezi hilo limeratibiwa na Diwani Jesca Mohmoud Msola kwa ajili ya kutatua kero za wananchi wake sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya chama cha Mapinduzi  CCM . "Diwani Jesca Mohmoud Msola, ameiona hii changamoto kubwa ya vyeti vya kuzaliwa ndio akabeba jukumu la kuleta RITA waweze kutoa vyeti vyeti vya kuzaliwa vinatolewa hapo hapo kwa gharama za Serikali "amesema Mwenda. Mwenda amesema katika Jamii lazima uwe na vyeti vya kuzaliwa ili uweze kupata...

LONDO - VIPIMO SAHIHI NI MSINGI WA UCHUMI WA VIWANDA NA TEKNOLOJIA

  Na Habar Plus Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo (Mb), amesema Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuimarisha mifumo ya vipimo nchini ili kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania katika soko la kimataifa, kukuza viwanda na kujenga uchumi wa kisasa unaotegemea sayansi na teknolojia. Mhe. Londo ametoa kauli hiyo leo Mei 20,2026 jijini Dodoma wakati akifunga rasmi maadhimisho ya Siku ya Vipimo Duniani ambapo amesisitiza kuwa maendeleo ya viwanda, biashara na huduma bora hayawezi kufikiwa bila uwepo wa vipimo sahihi na vinavyoaminika. Amesema serikali itaendelea kuboresha mazingira ya kisera na kisheria ili kuwezesha biashara, kuvutia uwekezaji na kuongeza ufanisi wa sekta binafsi kwa kuzingatia matumizi ya vipimo vinavyokubalika kitaifa na kimataifa. “Hakuna biashara yenye uaminifu bila vipimo sahihi, hakuna viwanda vinavyoweza kushindana kimataifa bila mifumo sahihi ya vipimo, na hakuna sera bora bila taarifa sahihi zinazotokana na sayansi ya vipimo,” amesema M...