Posts

Showing posts from May, 2026

SALOME: NGUZO ZA ZEGE NA CHUMA KUTUMIKA KUKABILI CHANGAMOTO YA KUANGUKA KWA NGUZO ZA UMEME ZA MITI.

Image
  NAIBU Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amesema Serikali kupitia TANESCO inaendelea kubadilisha nguzo chakavu kwa kuweka nguzo imara zaidi, zikiwemo nguzo za zege na chuma, pamoja na kuimarisha misingi ya nguzo katika maeneo yenye udongo laini ili kukabili changamoto ya kuanguka kwa nguzo za umeme. Salome ameeleza hayo leo, Mei 22, 2026, Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mhe. Sara Msafiri Ally, Mbunge wa Mvomero, aliyetaka kujua ni lini Serikali itatatua changamoto ya kuanguka kwa nguzo za umeme katika Tarafa ya Mgeta. Akijibu swali hilo, Salome amesema Serikali inatambua uwepo wa changamoto ya kuanguka kwa nguzo za umeme katika baadhi ya maeneo ya Tarafa ya Mgeta kutokana na sababu mbalimbali, ikiwemo mvua nyingi, uwepo wa udongo usiohimilivu pamoja na uchakavu wa baadhi ya nguzo. Amesema Serikali kupitia TANESCO inaendelea kufanya ukaguzi wa mara kwa mara wa miundombinu ya umeme ili kubaini na kushughulikia changamoto hizo mapema pindi zinapojitokeza. Aidha, Sa...

WAZIRI WA NISHATI NDEJEMBI AKUTANA NA BALOZI WA NORWAY

Image
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Mhe. Tone Tinnes yaliyolenga kuimarisha na kuendeleza ushirikiano kati ya nchi hizo mbili katika sekta ya nishati. Mazungumzo hayo yamefanyika leo Mei 22, 2026 katika Ofisi  Ndogo za Wizara ya Nishati zilizopo jijini Dar es Salaam. Viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ikiwemo mashirikiano ya kimkakati katika uendelezaji wa gesi, umeme, nishati jadidifu pamoja na kubadilishana uzoefu wa kitaalamu  na juhudi za kukuza sekta ya nishati kwa nchi hizo mbili. Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Kamishna wa Mafuta na Gesi kutoka wizara ya nishati, Bw. Goodluck Shirima, Mkurugenzi wa Maendeleo na Uzalishaji kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Bw. Paschal Njiko pamoja na wataalamu wengine.

BANDARI YA MBAMBA BAY KUFUNGUA FURSA MPYA ZA BIASHARA YA MAFUTA UKANDA WA KUSINI

Image
  Na Mwandishi Wetu Ujenzi wa Bandari ya Mbamba Bay unatarajiwa kuchochea kwa kiasi kikubwa biashara ya mafuta katika ukanda wa Kusini na kufungua njia mpya za usafirishaji wa bidhaa hiyo kuelekea nchi jirani kupitia miundombinu ya kisasa inayojengwa eneo hilo. Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa bandari hiyo, Meneja wa Mipango ya Mafuta wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), Gilbert Jungulu, amesema mradi huo una nafasi ya kuifanya Tanzania kuwa kitovu muhimu cha usambazaji wa mafuta kwa nchi za Malawi, Msumbiji na maeneo mengine ya ukanda huo. Amesema PBPA itaendelea kuratibu uagizaji wa mafuta nchini pamoja na kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha miundombinu muhimu ya mafuta, ikiwemo maghala ya kuhifadhia mafuta, inajengwa na kuimarishwa ili kurahisisha biashara ya kikanda. “Endapo maghala ya kuhifadhia mafuta yatakamilika hapa Mbamba Bay, itakuwa rahisi meli kushusha mafuta kwa ajili ya kuhifadhiwa na baadaye kusafirishwa kwenda nchi j...

TANESCO YAENDELEA KUWAELIMISHA WANAOFANYA SHUGHULI ZA KIUCHUMI KWENYE MIUNDOMBINU YA UMEME

Image
  Ni katika muendelezo wa ukaguzi wa miundombinu ya umeme Dar es salaam Yatoa rai kwa wananchi kuondoka kwa ajili ya usalama wa maisha na mali zao Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeendelea kuwasisitiza wananchi wanaofanya shughuli zao za kiuchumi katika miundombinu ya umeme kuondoka katika maeneo hayo kwa hiari, kwa kuwa wanahatarisha usalama wa maisha na mali zao. Akizungumza katika muendelezo wa zoezi la kukagua miundombinu ya umeme Mei 18, katika eneo la Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam, Msimamizi Msaidizi wa Njia Kuu za Kusafirisha Umeme Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Nicholaus Kivelege, amesema TANESCO inafanya jitihada za makusudi kutoa elimu kuhusu athari za kuendelea kufanya shughuli za kiuchumi chini ya njia kubwa za kusafirisha umeme katika maeneo mbalimbali nchini. Amesema licha ya jitihada hizo, bado baadhi ya wananchi wanaendelea kufanya shughuli hizo, hivyo amewaomba viongozi wa serikali za mitaa katika maeneo husika kuongeza nguvu ya kutoa elimu kuhusu madhara y...

TFS YATAKA VIWANGO VYA UBORA VILINDWE KATIKA BIASHARA YA ASALI

Image
  Tabora, Mei 21, 2026 Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umewataka wananchi wanaojihusisha na ufugaji nyuki na uchakataji wa mazao yatokanayo na nyuki kuzingatia viwango vya ubora na usalama wa bidhaa zao, ukionya kuwa uzalishaji usiozingatia sheria unaweza kuhatarisha masoko ya ndani na nje ya nchi. Tahadhari hiyo ilitolewa leo na Meneja wa Rasilimali Nyuki wa TFS, SACC Hussein Msuya, wakati wa majadiliano ya biashara kwa biashara na mdahalo kuhusu maendeleo ya sekta ya ufugaji nyuki nchini, uliofanyika katika Viwanja vya Kumbukumbu ya Vita mkoani Tabora kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Nyuki Duniani. SACC Msuya alisema Tanzania imeendelea kujijengea sifa kimataifa kutokana na ubora wa mazao yake ya nyuki, hususan asali na nta, lakini akasisitiza kuwa ubora huo unaweza kupotea iwapo wafugaji na wachakataji hawatazingatia viwango vilivyowekwa na mamlaka husika. “Utumiaji wa vifungashi bora ni takwa la kisheria na unasimamiwa na sheria ya viwango. Kwa mujibu wa kan...

DIWANI JESCA MAHMOUD MSOLLA AZINDUA KLINIKI YA VYETI VYA KUZALIWA BUYUNI

Image
  Na AyraNewstz DIWANI wa kata ya Buyuni   Wilayani Ilala Mkoa Dar es Salaam, JESCA MAHMOUD MSOLLA, amezindua Kiliniki ya vyeti vya kuzaliwa kata ya Buyuni kwa ajili ya kuwasogezea wananchi huduma za kijamii karibu na makazi yao.  Kampeni hiyo ya kutoa vyeti vya kuzaliwa  ambayo itakuwa wa siku kumi kutoa huduma ofisi za Afisa Mtendaji wa kata ya Buyuni ilianza Mei 13 itaendelea mpaka Mei 24 mwaka huu . Akizungumza kwa niaba ya Diwani wa Buyuni, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Buyuni ,Sylvanus Benard Mwenda ,alisema zoezi hilo limeratibiwa na Diwani Jesca Mohmoud Msola kwa ajili ya kutatua kero za wananchi wake sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya chama cha Mapinduzi  CCM . "Diwani Jesca Mohmoud Msola, ameiona hii changamoto kubwa ya vyeti vya kuzaliwa ndio akabeba jukumu la kuleta RITA waweze kutoa vyeti vyeti vya kuzaliwa vinatolewa hapo hapo kwa gharama za Serikali "amesema Mwenda. Mwenda amesema katika Jamii lazima uwe na vyeti vya kuzaliwa ili uweze kupata...

LONDO - VIPIMO SAHIHI NI MSINGI WA UCHUMI WA VIWANDA NA TEKNOLOJIA

Image
  Na Habar Plus Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo (Mb), amesema Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuimarisha mifumo ya vipimo nchini ili kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania katika soko la kimataifa, kukuza viwanda na kujenga uchumi wa kisasa unaotegemea sayansi na teknolojia. Mhe. Londo ametoa kauli hiyo leo Mei 20,2026 jijini Dodoma wakati akifunga rasmi maadhimisho ya Siku ya Vipimo Duniani ambapo amesisitiza kuwa maendeleo ya viwanda, biashara na huduma bora hayawezi kufikiwa bila uwepo wa vipimo sahihi na vinavyoaminika. Amesema serikali itaendelea kuboresha mazingira ya kisera na kisheria ili kuwezesha biashara, kuvutia uwekezaji na kuongeza ufanisi wa sekta binafsi kwa kuzingatia matumizi ya vipimo vinavyokubalika kitaifa na kimataifa. “Hakuna biashara yenye uaminifu bila vipimo sahihi, hakuna viwanda vinavyoweza kushindana kimataifa bila mifumo sahihi ya vipimo, na hakuna sera bora bila taarifa sahihi zinazotokana na sayansi ya vipimo,” amesema M...