Skip to main content

Posts

TMA YATOA UTABIRI WA HALI YA HEWA, YAWAONYA WANAOTUMIA BAHARI

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa utabiri wa hali ya hewa wa saa 24 kuanzia saa 3:00 usiku wa Agosti 19, 2026, ikieleza kuwa baadhi ya maeneo nchini yanatarajiwa kuwa na mawingu kiasi, mvua na ngurumo, huku maeneo mengine yakitarajiwa kuwa na vipindi vya jua. Kwa mujibu wa TMA, mikoa ya Kagera na Mara inatarajiwa kuwa na hali ya mawingu kiasi, mvua na ngurumo katika maeneo machache pamoja na vipindi vya jua. Mikoa ya Arusha na Kilimanjaro inatarajiwa kuwa na mawingu kiasi, mvua nyepesi katika maeneo machache na vipindi vya jua. Aidha, Visiwa vya Unguja na Pemba, Kigoma, Tabora, Katavi, Manyara, Dodoma, Singida, Mwanza, Geita, Shinyanga, Simiyu, Pwani ikiwemo Mafia, Tanga, Dar es Salaam, Morogoro, Lindi, Mtwara, Ruvuma, Mbeya, Rukwa, Iringa, Njombe na Songwe vinatarajiwa kuwa na hali ya mawingu kiasi pamoja na vipindi vya jua. Mawimbi makubwa baharini TMA imesema upepo wa Pwani unatarajiwa kuvuma kwa kasi ya hadi kilomita 30 kwa saa katika Pwani yote, ukitoka Kusini...
Recent posts

Utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24,zijazo kuanzia leo Agust 18,2026

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa utabiri wa hali ya hewa wa saa 24 kuanzia saa 3:00 usiku wa Agosti 18, 2026, ikieleza kuwa baadhi ya maeneo nchini yanatarajiwa kukumbwa na mawimbi kiasi, mvua na ngurumo pamoja na vipindi vya jua. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, katika mikoa ya Kagera, Mara na Simiyu, kunatarajiwa hali ya mawimbi kiasi, mvua na ngurumo katika maeneo machache pamoja na vipindi vya jua. TMA imesema katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro, hali ya mawimbi kiasi, mvua nyepesi katika maeneo machache pamoja na vipindi vya jua inatarajiwa. Kwa upande wa Zanzibar, ikiwemo Unguja na Pemba, pamoja na mikoa ya Kigoma, Tabora na Katavi, Mwanza, Geita na Shinyanga, Manyara, Dodoma na Singida, mvua pamoja na mawimbi kiasi na vipindi vya jua vinatarajiwa. Hali kama hiyo inatarajiwa pia katika mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Morogoro, Lindi na Mtwara, pamoja na Ruvuma, Mbeya, Rukwa, Iringa, Njombe na Songwe. Katika taarifa hiyo, TMA imeeleza kuwa kwa Pwani, kuanzia Kusi kwe...

TMA YATOA MWELEKEO WA MVUA ZA VULI OKTOBA–DESEMBA 2026, EL NIÑO YATAJWA KUCHANGIA MVUA KUBWA

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema mvua za msimu wa Vuli za Oktoba hadi Desemba 2026 zinatarajiwa kuwa za wastani hadi juu ya wastani katika maeneo mbalimbali nchini, huku uwepo wa hali ya El Niño ukitajwa kuwa miongoni mwa sababu zinazoweza kuchangia vipindi vya mvua kubwa katika baadhi ya maeneo. Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam wakati akitoa mwelekeo wa mvua hizo, Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Ladislaus Chang’a, amesema mvua hizo zinatarajiwa kuanza katika wiki ya kwanza na ya pili ya Oktoba katika baadhi ya maeneo. Amesema katika mikoa ya Arusha na Manyara, mvua zinatarajiwa kuwa za wastani hadi juu ya wastani, huku hali kama hiyo ikitarajiwa pia katika ukanda wa Kaskazini unaojumuisha Tanga, Dar es Salaam, kaskazini mwa Morogoro pamoja na visiwa vya Mafia na Pemba. TMA imesema uwepo wa El Niño unaweza kuchangia kuongezeka kwa vipindi vya mvua kubwa, hali ambayo inaweza kusababisha mafuriko na athari katika miundombinu, kilimo, usafiri na shughuli nying...

Utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24, zijazo

 

Utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24, zijazo kuanzia leo Agust 16,2026

 

JAJI MSHIBE ASISITIZA MAANDALIZI YA KISEKTA KATIKA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NIÑO

Dodoma, 14 Agosti 2026:  Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Mheshimiwa Jaji Mshibe Ali Bakari, amezitaka sekta zote nchini kutumia ipasavyo taarifa za hali ya hewa katika kufanya maandalizi ya kisekta ya kukabiliana na athari zinazoweza kusababishwa na uwepo wa El Niño. Mhe. Jaji Mshibe aliyasema hayo wakati akifungua Mkutano wa 25 wa kujadili Utabiri wa Msimu wa Mvua za Vuli, Oktoba hadi Disemba 2026, uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa PSSSF, Dodoma “Tunapojiandaa kupokea taarifa ya utabiri wa mvua za Vuli, Oktoba hadi Disemba 2026, ni muhimu kila mmoja wetu kuwa na jukumu la kufuatilia kwa karibu na kuelewa taarifa hizo ili kuanza maandalizi ya hatua za kuchukua katika kukabiliana na athari za hali ya hewa zinazotarajiwa kujitokeza katika sekta yake, kwa kutambua kuwa upo uwezekano mkubwa kwa El Niño kuendelea kuimarika kuelekea mwishoni mwa mwaka 2026,” alisisitiza Mhe. Jaji Mshibe. Mhe. Jaji mshibe aliongeza kuwa Tanzania, kama ilivyo kwa nchi n...

JKCI YATAKIWA KUENDELEZA KAMBI ZA MATIBABU YA MOYO NCHINI COMORO

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imetakiwa kuangalia namna ya kupeleka huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo nchini Comoro kutokana na huduma hizo kutopatikana nchini humo. Rai hiyo imetolewa leo na Balozi wa Tanzania nchini Comoro Mhe. Dkt. Salim Hamad alipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt. Peter Kisenge kuona namna ambavyo huduma zinazotolewa na JKCI zinaweza kuwakomboa wananchi wa Comoro. Dkt. Hamad alisema baada ya JKCI kuweka kambi maalumu ya matibabu ya moyo katika kisiwa cha Anjouan kilichopo nchini Comoro uongozi wa kisiwa hicho umeitaka JKCI kuingia mkataba nao wa kuendelea kufanya kambi za matibabu jambo ambalo linaonesha umahiri wa huduma zinazotolewa na wataalamu wa JKCI.“Nilifurahi nilipokutana na uongozi wa kisiwa cha Anjouan na kuniomba niwajulishe kuwa wanataka tuingie nao mkataba wa kufanya kambi za matibabu, hii ni hatua kubwa kwa nchi yetu katika kutoa huduma bingwa za matibabu ...