Posts

Showing posts from June, 2026

IZO BATTERY YAZUA GUMZO SOKONI BAADA YA UZINDUZI

Image
  Ayra Nwestz  Ikiwa ni wiki chache tangu kuzinduliwa kwa betri  ya Izo betry kutoka kampuni ya Izo betri imeelezwa kuwa betri za "IZO Battery" zimezua gumzo kubwa sokoni kutokana na muitikio mkubwa wa wateja. Kampuni hiyo imesema wateja wameipokea bidhaa yake kwa mikono miwili kutokana na ubora na uimara wake, jambo lililofikia hatua ya uzalishaji kuzidiwa na mahitaji katika soko. Akizungumza na vyombo vya habari, Mkurugenzi Mkuu Kampuni ya Izo Mahenge amesema ujio wa bidhaa hiyo umeleta mageuzi makubwa katika soko la betrii ambapo ikiwa na sifa kubwa ya kutunza moto kwa muda mrefu. "Sifa kubwa ya betri hii ni kutunza moto kwa muda mkubwa, ambapo sifa hiyo imeifanya betri yetu kuwa rahisi kutumia na kushika soko, haina usumbufu na kupendwa sana na wateja, ndio maana kwa sasa tuna mahitaji makubwa sana sokoni," amesema Izo Ameongeza kuwa, ili kukabiliana na uhitaji kuwa mkubwa katika soko, kampuni hiyo imesema imepanua huduma zake kwa kuwa na mawakala zaidi ya 50 ka...

MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI JENGO LA TANESCO CHAMWINO

Image
Ayra Newstz  Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ndugu. Wazo Mwang’onda ameweka jiwe la msingi katika ujenzi wa jengo la utawala la Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma leo Juni 06, 2026. Ujenzi wa jengo hilo utagharimu kiasi cha Sh Milioni 326 ambapo mpaka sasa tayari kiasi cha Sh Milioni 228 kimeshatumika. Akizungumza mara baada ya kukagua na kuzindua ujenzi wa mradi huo, Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge, Ndugu Mwang'onda ameipongeza Serikali ya awamu ya sita kupitia Wizara ya Nishati kwa namna inavyoendelea kuboresha na kusogeza huduma za umeme kwenye maeneo mbalimbali nchini. Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Chamwino ambaye pia ni Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema ujenzi wa mradi wa jengo hilo ni muendelezo wa utekelezaji wa ahadi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ya umeme. Amesema kukamilika kwa m...

SERIKALI YAJA NA MKAKATI HUU KATIKA KUONGEZA VIRUTUBISHI KWENYE VYAKULA

Image
  Ayra Nwestz  Katika kuhakikisha wananchi wanakuwa salama katika kula vyakula vilivoongezwa virutubishi, Serikali imejipanga kuwafikiwa wakulima wa vijijini ambao  wanatumia mashine za kusagia unga wa mahindi ambazo hazijawekewe madini wala vitamini ili kumlinda mlaji. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam katika mkutano wa 40 wa jukwaa la wadau wa urutubishaji vyakula, Mkurugenzi Msaidizi Huduma za Lishe Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) Luitfrid Nnally amesema Serikali imejipanga kuwafikia watu wa vijijini katika halmashauri mbalimbali kupitia Wizara ya afya na Ofisi ya Waziri Mkuu ambapo wameshaanza kuwapelekea mashine ambazo zinaweza zikaongeza virutubishi kwenye vyakula vyao. Ameongeza pia kwa kutumia utaratibu wa usimamizi wa huduma za lishe kwenye mamlaka za Serikali za mitaa kwenye halmashauri zao mama lishe wananunua virutubishi na kuvisambaza kwa wasindikaji ambao hawafungashi huku tukiendelea kuwasimamia kisheria. "Miaka ya nyuma tulikua tunaag...

MATHIAS CANAL ATWAA TUZO YA USHIRIKI BORA WA KAZI ZA JAMII 2026

Image
  Ayra Newstz  Mwanzilishi na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni za WAZOHURU MEDIA na WAZOHURU APPARTMENTS, Mathias Canal, ametunukiwa Tuzo ya Ushiriki Bora wa Kazi za Jamii 2026, ikiwa ni kutambua mchango wake mkubwa katika kuhamasisha maendeleo ya jamii kupitia shughuli mbalimbali za kijamii na misaada ya kijamii. Tuzo hiyo iliyotolewa usiku wa Juni 5, 2026 jijini Dodoma katika hafla ya utoaji wa tuzo iliyoandaliwa na Central Zone Awards, tukio lililowakutanisha wadau mbalimbali kutoka sekta tofauti waliotoa mchango wa kipekee katika maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla. Waandaaji wa tuzo hizo wamesema Mathias Canal amestahili kutunukiwa tuzo hiyo kutokana na kujitolea kwake, ushiriki wake wa karibu na jamii pamoja na mchango wake endelevu katika kusaidia makundi mbalimbali yenye uhitaji. Tuzo hiyo pia imetambua moyo wake wa huruma, uwajibikaji na dhamira ya kuleta mabadiliko chanya katika maisha ya wananchi. Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Mathias Canal amesema heshim...

LISSA LUXURY HAIR YAZINDULIWA DAR

Image
  Ayra Newstz Chuo cha urembo cha Lissa College leo kimezindua bidhaa yake mpya ya nywele inayojulikana kama (Lissa luxury hair) ambayo itashika soko la urembo kutokana na ubora wa bidhaa hiyo huku bei yake ikiwa rafiki kwa kila mtanzania. Akizungumzia na waandishi wa Habari  Jijini Dar es salaam Mkurugenzi na mmiliki wa chuo hicho, Lissa Leonce amesema kuwa wamekuja na bidhaa hiyo baada ya kufanya utafiti wa kina wa soko la bidhaa za nywele hapa nchini na kuamini kuwa bidhaa yao itashika soko la urembo. "Tumefanya utafiti wa kina wa soko la bidhaa za nywele nchini kwetu na tumegundua kuwa bidhaa yetu itashika soko la urembo kutokana na ubora wake amesema Lissa. Amesema kuwa maono ya chuo hicho ni kwamba, watazidi kubuni bidhaa za nywele ambazo zitaendana na uhalisia wa waafrika na zenye muonekano wa asili ambapo pia zitakuwa na bei ambazo kila mtanzania ataweza kuzimudu. Aidha, chuo hicho pia kimemtambulisha Pinela Justine pamoja na mwanahabari Maimatha Jesse kama mabalozi wa...

WAANDISHI WA HABARI WAPEWA RUNGU, YALIYOTOKEA OCT 29 YAELEZWA

Image
Ayra Nwestz  Waandishibwa habari nchini Tanzania wametakiwa kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu athari za maandamano yasiyo ya amani na vurugu, kwani matukio hayo yanaweza kuathiri maendeleo na rasilimali za taifa. Rai hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam na Mwanafalsafa wa Pan-Afrika kutoka Zimbabwe, Dk. Joshua Maponga, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa makala inayozungumzia matukio yaliyojitokeza kabla na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025. Amesema kuwa, filamu hiyo inabainisha ushahidi unaothibitisha kuwa vurugu ziliratibiwa na kupangwa mapema ambapo wahusika waliongezwa na ushawishi kutoka nje ya nchi jambo ambalo halijawahi kuchapishwa katika vyombo vya habari vya kimataifa.  Ameongeza kuwa,  hali hiyo ni hatari kwa ustawi na usalama wa taifa, hivyo akaishauri Serikali kuchukua hatua za kufanya uhakiki wa mashirika hayo ili kubaini vyanzo vya fedha wanazopata na namna zinavyotumika. Aidha, ameeleza kuwa watu wanaochochea vurugu mara...

NAIBU WAZIRI TAMISEMI APONGEZA MATUMIZI YA MAGARI YA UMEME KATIKA KUHIFADHI MAZINGIRA

Image
Na Mwandishi Wetu, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI anayeshughulikia Afya, Dkt. Jafar Seif, ametembelea banda la Wizara ya Nishati katika maonesho ya wiki ya Mazingira yanayoendelea kwenye Viwanja vya Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma, ambapo amejionea teknolojia mbalimbali za nishati safi zinazolenga kuimarisha maendeleo endelevu na uhifadhi wa mazingira nchini. Akiwa katika maonesho hayo , Dkt. Seif ameweza kutembelea banda  la Wizara ya Nishati ambapo amejionea gari aina ya Nissan Leaf linalotumia umeme na kupata maelezo kuhusu matumizi ya gari hilo  linalotumika kuhamasisha wananchi kuhusu matumizi ya nishati safi na teknolojia rafiki kwa mazingira. Akizungumza katika banda hilo, Dkt. Seif amesema matumizi ya magari ya umeme ni hatua muhimu katika juhudi za Serikali za kuhifadhi mazingira na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.  Ameeleza kuwa teknolojia hiyo inachangia kupunguza uzalishaji wa hewa ya ukaa itokanayo na matumizi ya ...

NAIBU WAZIRI AHIMIZA USHIRIKIANO KUSAMBAZA TAARIFA ZA HALI YA HEWA KWA WANANCHI WA VIJIJINI

Image
Ayra Nwestz  Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Reuben Nhamanilo Kwagilwa, ameitaka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kuendelea kuimarisha ushirikiano na wadau mbalimbali ili kuhakikisha taarifa za hali ya hewa zinawafikia wananchi wote, hususan wanaoishi katika maeneo ya vijijini na maeneo ya mbali yanayokabiliwa na changamoto za upatikanaji wa huduma za mawasiliano. Mhe. Kwagilwa ameyasema hayo alipotembelea banda la TMA wakati wa Ufunguzi wa Maonesho ya Siku ya Mazingira Duniani 2026 yanayofanyika kuanzia tarehe 1 hadi 5 Juni 2026 katika Viwanja vya Jakaya Kikwete Convention Centre (JKCC), jijini Dodoma, chini ya kauli mbiu isemayo "Dira 2050: Tuwajibike Kukijanisha Tanzania" Akizungumza na wataalamu wa TMA, Mhe. Kwagilwa ameipongeza mamlaka hiyo kwa kazi kubwa inayoendelea kufanya katika utoaji wa huduma za hali ya hewa na kusisitiza umuhimu wa kuhakikisha taarifa hizo zinawafikia wananchi wanaozitegemea katika shughuli zao za...

MHA. MRAMBA NA BENKI YA DUNIA WAJADILI UIMARISHAJI WA GRIDI YA TAIFA

Image
Dar es Salaam,  Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Umeme na Nishati Jadidifu, Mha. Felchesmi Mramba,  amekutana na wawakilishi wa Benki ya Dunia (WB) kujadili matokeo ya utafiti uliofanyika chini ya ufadhili wa benki hiyo ukilenga kuimarisha mfumo wa Gridi ya Taifa nchini. Utafiti huo umebainisha maeneo muhimu ya utekelezaji yatakayosaidia kuimarisha Gridi ya Taifa ili kuhakikisha mfumo wa umeme nchini unakidhi mahitaji ya sasa na ya baadaye. Akizungumza katika kikao hicho, Mha. Mramba ameishukuru Benki ya Dunia kwa kuendelea kuunga mkono maendeleo ya sekta ya nishati nchini kupitia ufadhili na usimamizi wa tafiti mbalimbali zenye lengo la kuboresha miundombinu ya umeme na kuongeza ufanisi wa huduma kwa wananchi. Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuweka mkazo katika utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa kwenye ripoti hiyo ili kusaidia mipango ya uwekezaji, kuboresha uendeshaji wa mfumo wa umeme, kuendeleza usasa wa Gridi ya Taifa na kuongeza uimara wa hudum...

GOLDEN VALUE WAPATIWA ELIMU YA NISHATI KATIKA MAONESHO YA WIKI YA MAZINGIRA DUNIANI 2026

Image
Na Mwandishi Wetu, Meneja wa Shule ya Golden Value Bi. Nuru Nyundo, ameongoza wanafunzi wa darasa la nne na la sita kutembelea banda la Wizara ya Nishati pamoja na taasisi zake katika Maonesho ya Wiki ya Mazingira Duniani 2026 yanayoendelea katika katika Viwanja vya Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma Ziara hiyo imelenga kuwapatia wanafunzi elimu kuhusu sekta ya nishati na mchango wake katika uhifadhi wa mazingira.  Wakiwa katika banda hilo, wanafunzi walipata fursa ya kujifunza kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia, nishati jadidifu na teknolojia mbalimbali zinazosaidia kupunguza uharibifu wa mazingira. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Bi. Nyundo amesema  kuwa kuwashirikisha wanafunzi katika maonesho hayo ni njia muhimu ya kuwajengea uelewa wa mapema kuhusu umuhimu wa kutunza mazingira na kutumia nishati kwa njia endelevu ili kulinda afya na mazingira kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo. Kwa upande wake, mwanafunzi Maria Yusuph wa darasa la sita amepong...

WATUMISHI 12 WA HALMASHAURI YA KIGAMBONI NA TAMISEMI WAFIKISHWA MAHAKAMANI

Image
  Ayra Nwestz  Watumishi 12 wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigamboni na Ofisi ya Rais Tamisemi Dodoma wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa tuhuma za wizi na ubadhilifu wa fedha kiasi cha shilingi milioni 169,617,520 maarufu kama (FEDHA ZA BAKAA) Taarifa hiyo imetolewa leo Juni 2,2026 jijini Dar es salaam na Kaimu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Temeke Francis Luena wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelezea mafanikio ya utendaji kazi wa Taasisi hiyo kwa kipindi cha  Mwezi Januari hadi Machi,2026. Luena amesema kuwa uchunguzi ulifanyika kwa mujibu wa sheria na mwezi Septemba 2,2025 washtakiwa hao walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa makosa ya kuendesha genge la uhalifu,uchepuzi, ubadhilifu,utakatishaji fedha na kuisababishia hasara Serikali,makosa ambayo ni kinyume cha sheria ya uhujumu uchumi Na.200,sheria ya kuzuia na Kupambana na rushwa Na.329, na sheria ya utakatishaji fedha Na.423. "Waliofikishwa mahakamani ambao ni watumishi kutoka...

HORMUZ YAPANDISHA TENA, BEI YA MAFUTA, DUNIA SASA NJIA PANDA

Image
Kuvunjika kwa mazungumzo ya Marekani na Iran kwafuta matumaini ya kushuka kwa bei za nishati duniani* DAR ES SALAAM. Dunia inazidi kushuhudia  kipindi kigumu cha sintofahamu ya nishati baada ya bei za mafuta kuanza kupanda kwa mara nyingine kufuatia kusimama kwa mazungumzo kati ya Marekani na Iran yaliyokuwa yameanza kutoa matumaini ya kurejea kwa utulivu katika Mlango wa Hormuz. Siku chache zilizopita, masoko ya mafuta duniani yalikuwa yameanza kuonyesha dalili za kutulia ambapo bei za mafuta zilishuka kwa zaidi ya asilimia 6 hadi 7 baada ya taarifa za uwezekano wa kufikiwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano na kufunguliwa kwa Hormuz, njia muhimu inayobeba karibu asilimia 20 ya mafuta yote yanayouzwa duniani. Reuters, CNN, Al Jazeera na vyombo vingine vya kimataifa viliripoti kuwa wafanyabiashara wa mafuta walikuwa wameanza kuondoa kile kinachoitwa risk premium kutokana na matarajio ya amani kurejea katika Ghuba ya Uajemi. Matumaini hayo sasa yanaonekana kuyeyuka. Wiki hii Iran...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24, ZIJAZO

Image