Skip to main content

Posts

Showing posts from June, 2026

UKARABATI WA KITUO CHA KUZALISHA UMEME CHA HALE WAFIKIA ASILIMIA 83 YA UTEKELEZAJI

Waziri Ndejembi amtaka mkandarasi kukamilisha ukarabati kwa wakati bila kuongezewa muda wa mkataba Kukamilika kwake kutaongeza ufanisi wa uzalishaji na kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika Mkoa wa Tanga na maeneo ya jirani Na Mwandishi Wetu, Korogwe – Tanga Serikali imeendelea kusimamia utekelezaji wa miradi ya ukarabati wa miundombinu ya umeme nchini, huku Mradi wa Ukarabati wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale wilayani Korogwe, mkoani Tanga, ukifikia asilimia 83 ya utekelezaji. Akikagua maendeleo ya Mradi huo tarehe 29 Juni, 2026 Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb), amemtaka mkandarasi kuhakikisha anakamilisha kazi ndani ya muda uliopangwa, akisisitiza kuwa Serikali haitakuwa tayari kuongeza muda wa mkataba wa utekelezaji wa mradi huo. Waziri Ndejembi amesema kukamilika kwa ukarabati wa Kituo cha Hale kutaimarisha ufanisi wa uzalishaji wa umeme, kuongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika na kuchochea shughuli za kiuchumi katika Mkoa wa Tanga na maeneo ya jirani. “M...

Utabiri wa hali hewa kwa saa 24 zijazo

 

Utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24 zijazo

 

KATIBU MKUU WA NISHATI ZAMBIA AIPONGEZA TANZANIA KWA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA SEKTA YA UMEME

Aeleza Ushirikiano katika utekelezaji wa Mradi wa TAZA na faida zake Kikanda. Asifu jitihada za kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia. Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati nchini Zambia,  Mhe. Arnold Simwaba, amesema kuwa Tanzania na Zambia zimeendelea kushirikiana katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwemo Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa TAZA (Tanzania–Zambia Power Interconnection Project), wenye lengo la kuunganisha gridi za umeme za nchi hizo mbili kwa manufaa ya pande zote. Mhe. Simwaba ameyasema hayo Juni 25, 2026, mkoani Dodoma, wakati wa kikao cha pamoja kilichowakutanisha wajumbe kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Wizara ya Nishati ya Zambia, Mamlaka ya Umeme Vijijini ya Zambia pamoja na Shirika la Umeme Zambia (ZESCO), kwa lengo la kubadilishana uzoefu na kujadili namna ya kuboresha huduma za umeme. Ameipongeza Tanzania kwa kupiga hatua kubwa katika sekta ya umeme baada ya miradi mingi ya umeme kukamilika nchini. Aidha, amesifu ...

SERIKALI IMEDHAMIRIA KULETA MAPINDUZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA - NAIBU WAZIRI SALOME

Imepunguza kodi kwenye vifaa vya Nishati Safi. Lengo ni kuwafikia wananchi wa aina zote. Imeelezwa kuwa Serikali  ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeweka dhamira  ya dhati  katika kuleta  mapinduzi ya matumizi ya Nishati  Safi ya kupikia yanayoongozwa na mkakati wa taifa wa Nishati Safi ya kupikia  kwa mwaka 2024-2034 unaolenga kuhakikisha asilimia 80 ya watanzania wanatumia Nishati Safi ya kupikia ifikapo 2034. Ameyasema hayo Naibu Waziri wa Nishati  Mhe. Salome Makamba alipokuwa akifunga kongamano la kuhamasisha na kuelimisha juu ya matumizi ya Nishati  safi ya kupikia Juni 25, 2026 lilokuwa likifanyika katika Ukumbi  wa East  Africa Commercial Logistic Center uliopo Jijini  Dar es Salam. Mhe. Salome amesema kuwa ni muda wa kuhakikisha kila mtanzania ananufaika na matumizi ya Nishati Safi  ya Kupikia ili kuweza kulinda afya pamoja na kutunza Mazingira hali itakayosaidia Nchi kuingia kwenye mapinduzi  makubwa ya Matumi...

NAFUU YA MAFUTA KUANZA KUONEKANA JULAI _ NDEJEMBI

Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema Watanzania wataanza kushuhudia kushuka kwa bei za mafuta kuanzia mwezi Julai mwaka huu kufuatia kuanza kushuka kwa bei ya mafuta ghafi katika soko la dunia baada ya kusitishwa kwa mapigano ya Mashariki ya Kati. Akijibu mwongozo wa Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu, Bungeni jijini Dodoma leo, Juni 26, 2026, Waziri Ndejembi amesema Serikali imezielekeza EWURA, TPDC na PBPA kuhakikisha manufaa ya kushuka kwa bei za mafuta katika soko la dunia yanawafikia walaji nchini. Amesema licha ya athari za vita kati ya Iran, Israel na Marekani zilizosababisha usumbufu katika usafirishaji wa mafuta kupitia Mlango wa Hormuz, Tanzania iliendelea kuwa na uhakika wa upatikanaji wa mafuta bila kukumbwa na uhaba. Ndejembi amesema hatua za haraka zilizochukuliwa na Serikali zilihakikisha mafuta yanapatikana katika maeneo yote ya nchi, huku Tanzania ikiendelea kuwa miongoni mwa nch...

SALOME MAKAMBA AFUNGA MAONYESHO YA NISHATI EXPO 2026

Apongeza juhudi za REA kusambaza Nishati Safi ya kupikia vijijini Ayra Newstz, Dar Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba leo tarehe 25 Juni, 2026 amefunga rasmi Maonesho na Kongamano la Nishati Safi Expo 2026  yaliyofanyika katika ukumbi wa EACLC jijini Dar es Salaam Akiwa katika banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ameipongeza REA kwa kuendelea kusambaza na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia hususan katika maeneo ya vijijini na pembezoni mwa miji.  "Naipongeza REA kwa kazi kubwa mnayoifanya katika kuimarisha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia na naendelea kuwahimiza wananchi kuendelea kutumia teknolojia mpya za nishati safi ili kulinda afya, mazingira na kuboresha ustawi wa jamii, " Ameongeza Mhe. Makamba.  Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuwekeza na kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha malengo ya Taifa ya matumizi ya nishati safi ya kupikia yanafikiwa kwa manufaa ya Watanzania wote. Aidha, Mhe. Makamba ameelezwa hatua mbali...

MAMBO ALIA NA SERIKALI, AWAITA VIJANA AGUST 12

  Na Ayra Newstz  Mratibu wa Jukwaa la Vijana Taifa la Chama cha Ukombozi wa Umma(JUVICHA), Masoud Mambo, amesema kuwa Serikali imeshindwa kutengeneza mazingira rafiki kwa vijana na badala yake imekuwa ikiweka vikwazo vikubwa katika ukuaji wa uchumi wa vijana wa Kitanzania kwa kushindwa kuona thamani kubwa ya vijana katika ukuaji wa uchumi.  Amesema hayo, jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Makao Makuu ya CHAUMA, ambapo ameeleza vijana ndio soko kubwa kutokana na uzalishaji mkubwa wanaoufanya, lakini pamoja na umuhimu huo wa vijana katika uzalishaji na ukuaji wa uchumi wa taifa, bado wamekuwa wakikumbana na changamoto lukuki, kama ambavyo vyama vya siasa, taasisi na makundi mbalimbali vimekuwa vikiwasemea. Amesema kumekuwepo na sheria, sera na taratibu kadhaa ambazo kimsingi 7zinamnyima kijana nafasi ya kukua kiuchumi na kupata fursa ya kuingia katika ushindani wa soko la kimataifa. Aidha, amesema kuwa vijana wa Kitanzania wanakumbwa na c...

SERIKALI YAJIPANGA KUKABILIANA NA ATHARI ZA ELNINO _ TMA

  Dodoma  Serikali imesema imejipanga kikamilifu kukabiliana na madhara yanayoweza kusababishwa na hali ya El Niño kufuatia tahadhari iliyotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA). Akizungumza hii leo 24 Juni, 2026 wakati wa ufunguzi wa kikao cha wadau wa usimamizi wa maafa, Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Operesheni na Uratibu kutoka Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Kanali Selestine Masalamado, amesema kuwa tayari Serikali imeandaa Rasimu ya Mpango wa Taifa wa Dharura ili kuimarisha maandalizi na hatua za kukabiliana na hali hiyo. Amesema mpango huo unalenga kuhakikisha kunakuwa na uratibu madhubuti, utekelezaji wa hatua za mapema pamoja na kupunguza athari zinazoweza kujitokeza kwa wananchi, mali zao na miundombinu. “Kikao hiki kinatoa fursa kwa wizara, taasisi, mikoa na wadau wengine kupitia rasimu hii kwa kina na kutoa maoni yatakayosaidia kupatikana kwa mpango shirikishi na unaotekelezeka,” amesema Kanali Mas...

MD TWANGE ATOA RAI KWA MAMENEJA TANESCO KUONGEZA KASI YA KUPAMBANA NA WIZI WA MIUNDOMBINU YA UMEME

Afungua Mkutano Mkuu wa mwaka wa Mameneja na Wakurugenzi wa Kanda, Dodoma Asisitiza umuhimu wa kuongeza ubunifu katika ukusanyaji wa mapato. Awapongeza kwa kazi nzuri na kuendelea kuimarisha mahusiano na wadau Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Bw. Lazaro Twange, ametoa rai kwa mameneja wa TANESCO nchini kusimamia na kupambana kwa nguvu zote na changamoto ya wizi wa miundombinu ya umeme, ambayo imekuwa ikijitokeza katika maeneo mbalimbali ya mikoa wanayoisimamia. Bw. Twange ameyasema hayo Juni 24, 2026, mkoani Dodoma wakati akifungua Mkutano mkuu wa mwaka wa Mameneja na Wakurugenzi wa Kanda, wenye lengo la kujadili masuala mbalimbali yanayohusu Shirika pamoja na Kurugenzi ya Usambazaji. Licha ya kuwapongeza mameneja hao kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kuwahudumia wananchi, amesema kuna haja ya kila mmoja kuona uchungu wa mali za Shirika kwa kuongeza jitihada za kuhakikisha changamoto ya wizi wa miundombinu ya umeme inatokomezwa. “Nawapongeza kwa kazi nzuri m...

Utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24 zijazo

 

NDEJEMBI ATAKA KASI YA UTENDAJI KAZI WA WIZARA YA NISHATI NA TAASISI KUONGEZEKA

Lengo ni kukidhi matarajio ya wananchi katika Sekta ya Nishati  Dodoma Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amewataka watendaji na watumishi wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake  kuongeza kasi ya utekelezaji wa majukumu yao katika mwaka  mpya wa fedha 2026/2027 ili  kuweza kukidhi matarajio makubwa ya wananchi katika sekta ya nishati. Mhe. Ndejembi ameyasema hayo katika kikao kazi kilichojumuisha viongozi wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake kilicholenga kupata matokeo ya tathmini ya utendaji kazi wa Wizara na taasisi hizo. Kikao kazi hicho kilihudhuriwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba na  Makatibu Wakuu, Mhandisi Felchesmi Mramba na Dkt.James Mataragio. Waziri Ndejembi amesema wananchi wanamatarajio mbalimbali ikiwemo kupata  umeme wa uhakika, kuongezeka kwa uzalishaji na matumizi ya gesi asilia na mafuta, uhakika wa upatikanaji wa mafuta nchini pamoja na nishati safi ya kupikia   "Mwaka wa fedha unaokuja twendeni tukachap...

WIZARA YA NISHATI YASISITIZA USHIRIKIANO KUFIKIA ASILIMIA 80 YA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA IFIKAPO 2034

Dar es Salaam.  Wizara ya Nishati imesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo katika kufanikisha lengo la Taifa la kufikia asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034. Wito huo umetolewa na Mjiolojia Mkuu wa Wizara ya Nishati, Bw. Ngereja Mgejwa, kwa niaba ya Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia, wakati akifungua Maonesho na Kongamano la Nishati Safi ya Kupikia 2026 (Clean Cooking Expo 2026), Juni 23, 2026 katika Ukumbi wa EACLC jijini Dar es Salaam. Akizungumza katika kongamano hilo, Bw. Mgejwa amesema nishati safi ya kupikia ni ajenda muhimu ya kitaifa inayohitaji ushirikiano wa wadau wote ili kuleta mabadiliko ya kudumu katika sekta ya nishati. Amesema matumizi ya nishati safi yana mchango mkubwa katika kulinda afya za wananchi, hususan wanawake na watoto, kuhifadhi mazingira, kuinua elimu kwa watoto wa kike na kuongeza tija ya kiuchumi. Ameeleza kuwa kazi iliyopo mbele ni kuhakikisha wananchi wanapata nisha...

Utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24 zijazo

 Usikose kufuatilia utabiri wa hali ya hewa  

SEMU AIPINGA BAJETI KUU YA SERIKALI, ATOA HOJA HIZI..

Ayra Nwestz  Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Dorothy Semu, amesema Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2026/27 imeshindwa kutoa majibu ya msingi kwa changamoto zinazowakabili Watanzania katika sekta muhimu za afya, kilimo na biashara. Akizungumza wakati wa kuwasilisha uchambuzi wa bajeti hiyo, Semu amesema kuwa watanzania walitarajia kuona utekelezaji wa ahadi mbalimbali zilizotolewa na Serikali kuhusu kuboresha huduma za afya, hususan mpango wa afya kwa wote, lakini hali halisi inaonesha kuwa gharama za matibabu zinaendelea kuwa mzigo mkubwa kwa wananchi. Ameeleza kuwa gharama za vipimo na matibabu ya magonjwa sugu zimeendelea kuwa kubwa katika hospitali za umma, huku wananchi wakilazimika kulipia huduma ambazo awali zilitarajiwa kutolewa kwa urahisi zaidi. Kwa mujibu wake, bajeti hiyo haijaeleza namna itakavyopunguza gharama hizo wala kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wananchi wote. Semu alihoji utekelezaji wa mfumo wa bima ya afya kwa wote, akidai kuwa mfumo ul...

AMUUA BABA YAKE, AMFUKIA CHUMBANI

  Ayra Newstz  Siri iliyoficha ukewli juu ya kutoweka kwa Ramadhan Jafari maarufu @Muna, (47), eneo la Mbezi Luguruni, Ubungo, imebainika baada ya Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam kukamilisha uchunguzi wa kina uliodumu kwa takribani wiki moja. Kulingana na taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Kanda Maalum Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro leo Juni 23, 2026, Ramadhan Jafari aliyeripotiwa kupotea tarehe 16 Juni, 2026, amebainika kufariki dunia katika mazingira ya kusikitisha ndani ya makazi yake eneo la Kwembe. SACP Muliro amesema  taarifa ya kupotea kwa mzee huyo ilipokelewa na Kituo cha Polisi Kimara Gogoni na kuwashwa balaza la uchunguzi mara moja, huku wapelelezi kwa kushirikiana na wananchi walifanya ufuatiliaji wa nyumba hadi nyumba, simu hadi simu, hadi ukweli ulipopatikana. Katika uchunguzi wa Jeshi la Polisi walimkamata kijana Juma Ramadhan maarufu @Juli, 21, ambaye ni mtoto wa marehemu, chanzo cha Polisi kinasema baada ya mahojiano ya kina, mtuhumiwa aliel...

ILI KUFIKIA UMEME WA MEGAWATI 8,000 IFIKAPO 2030; NDEJEMBI ATAJA VYANZO

Waziri wa Nishati, Mhe.Deogratius Ndejembi, amesema Serikali imejipanga kuongeza uzalishaji wa umeme kutoka megawati 4,300 za sasa hadi kufikia megawati 8,000 ifikapo mwaka 2030 kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali mikubwa ya uzalishaji wa umeme nchini. Amesema hayo akichangia Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 Bungeni jijini Dodoma Akifafanua kuhusu hilo amesema kuwa, Dira ya Taifa imeweka lengo la kufikia uzalishaji wa megawati 74,000 za umeme ifikapo mwaka 2050, huku maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi yakielekeza Taifa kufikia angalau megawati 8,000 ifikapo mwaka 2030. Mhe.Ndejembi amesema katika bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027, Wizara ya Nishati imeweka mikakati madhubuti ya kuanza utekelezaji wa miradi mikubwa ya uzalishaji wa umeme itakayosaidia kufikia lengo hilo. Miongoni mwa miradi hiyo ni mradi wa kuzalisha umeme kwa kutumia nishati ya jua wa megawati 100 katika eneo la Kis...

MADIWANI WA MPANDA NA NSIMBO WAIPONGEZA SERIKALI KWA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA KITUO CHA KUFUA UMEME CHA JULIUS NYERERE

Na Mwandishi wetu, Rufiji - Pwani Madiwani wa Halmashauri za Wilaya za Mpanda na Nsimbo mkoani Katavi, wakiongozana na baadhi ya wabunge na viongozi wengine, wamepongeza uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali katika Kituo cha Kufua Umeme cha Julius Nyerere (JNHPP) baada ya kujionea kwa karibu uendeshaji wa kituo hicho na mchango wake katika maendeleo ya sekta ya nishati nchini. Viongozi hao walitembelea kituo hicho tarehe 20 Juni 2026 kwa lengo la kujionea uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali, kufahamu namna kituo kinavyoendeshwa pamoja na kupata uelewa wa mchango wake katika kuimarisha upatikanaji wa umeme nchini. Ziara hiyo ilihusisha madiwani 22 pamoja na baadhi ya wabunge na viongozi wengine kutoka Mkoa wa Katavi. Akizungumza baada ya ziara hiyo, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mpanda, Charles Philipo, aliishukuru Serikali kwa juhudi kubwa inazoendelea kufanya katika kuimarisha sekta ya nishati na kuipongeza TANESCO kwa kuwapatia viongozi hao fursa ya kujionea kituo hicho. “Tunais...

WAZIRI NDEJEMBI: WAKANDARASI WA UMEME WASIOFANYA VIZURI WASIPEWE MIRADI MINGINE

Apongeza mchango REA katika kufikisha asilimia 78.1 ya upatikanaji umeme vijijini. Apongeza wakandarasi wazawa waliofanya vizuri katika utekelezaji wa miradi; Ataka wapewe kazi zaidi. Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, ameuelekeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kuhakikisha kuwa wakandarasi ambao hawajafanya vizuri katika utekelezaji wa miradi ya umeme inayosimamiwa na Wakala huo  kutopewa  kazi nyingine, ili kutokwamisha lengo la Serikali la kuwafikishia wananchi huduma ya umeme kwa wakati na kwa ufanisi. Mhe. Ndejembi ametoa maelekezo hayo tarehe 22 Juni, 2026 jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), wakandarasi wa miradi ya umeme pamoja na wadau wa miradi ya nishati vijijini.  Kikao hicho kilienda sambamba na utoaji wa tuzo kwa wakandarasi waliofanya vizuri katika utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini na vitongojini, ikiwemo waliokamilisha kazi mapema kabla ya muda wa mwisho wa mikataba yao. "Umeme sasa si anasa, ni ...

WATAALAM WA REA ZAMBIA KUJIFUNZA MAFANIKIO YA TANZANIA KATIKA USAMBAZAJI UMEME VIJIJINI

Viongozi wa Mamlaka ya Nishati Vijijini (REA) kutoka nchini Zambia wamewasili nchini kwa ajili ya ziara ya kujifunza na kubadilishana ujuzi na Wakala wa Nishati Vijijini (REA). REA Zambia ambao wameongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Zambia anayeshughulikia Umeme, Mhandisi Arnold Simwaba wamewasili leo Juni 21, 2026 katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kupokelewa na Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati Tanzania, Wilson Nyamanga pamoja na Mkurugenzi wa Umeme Vijijini kiutoka REA Tanzania, Mhandisi Jones Olotu, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa REA Tanzania, Renatus Msangira. Uongozi wa REA Zambia utakuwa nchini kwa ziara ya kikazi ya Siku 7 ambapo pamoja na vikao vya kubadilishana ujuzi, wajumbe hao wanatarajiwa kutembelea miradi mbalimbali ya umeme vijijini inayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini.

TMA YAENDELEA KUJENGA UWELEWA KUHUSU MASUALA YA HALI YA HEWA, WIKI YA UTUMISHI

  Ayra Nwestz, Dodoma Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) yaendelea kuwajengea uelewa wananchi juu ya masuala mbalimbali ya hali ya hewa kupitia maonesho ya wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kufanyika katika viwanja vya Chinangali Park, Jijini Dodoma kuanzia Tarehe 16 – 23 Juni 2026. Maadhimisho hayo yalifunguliwa rasmi tarehe 17 Juni 2026 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, na yanatarajiwa kufikia kilele chake tarehe 23 Juni 2026. Katika maonesho hayo, wananchi wameendelea kukaribishwa kutembelea banda la TMA ili kutumia fursa hiyo kujifunza namna ya kuzitafsiri taarifa za hali ya hewa pamoja na matumizi sahihi kwa sekta husika ikiwemo kilimo, usafiri na uvuvi, hatua itakayosaidia kuongezeka kwa ufanisi katika shughuli za kimaendeleo. Kaulimbiu ya maadhimisho hayo ni: “Kuchochea uwajibikaji jumuishi kwa huduma endelevu.”

MSUVA AUNGA MKONO MPANGO WA MAFUNZO WA JAB KUELEKEA AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu Mchezaji wa Kimataifa wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Simon Msuva, amepongeza mpango wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) wa kuandaa mafunzo maalum kwa Waandishi wa Habari kuelekea Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2027), akisema hatua hiyo itasaidia kuimarisha mchango wa sekta ya habari katika kuitangaza Tanzania, kukuza vipaji vya wanamichezo na kuibua fursa mbalimbali za maendeleo zitakazotokana na mashindano hayo. Msuva ametoa pongezi hizo leo, tarehe 19 Juni 2026, alipotembelea Ofisi za Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari zilizopo Posta Mpya, Mtaa wa Jamhuri jijini Dar es Salaam na kufanya mazungumzo na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi hiyo, Wakili Patrick Kipangula. Amesema Waandishi wa Habari wamekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya michezo nchini kwa kutangaza vipaji vya wanamichezo, kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika michezo na kuitangaza Tanzania ndani na nje ya nchi. “Mimi nawaombea waweze kutengeneza elimu ...