Na Mwandishi Wetu Wakati changamoto ya ukosefu wa ajira ikiendelea kuwaathiri vijana wengi nchini, Zain Foundation imeanza kuonekana kuwa chanzo cha matumaini kwa wakazi wa Kata ya Keko, wilayani Temeke, baada ya kuanza kutoa ajira na kuendesha programu za kuwawezesha vijana kujitegemea kiuchumi. Akizungumza kuhusu shughuli za taasisi hiyo, Diwani wa Kata ya Keko na mmiliki wa kampuni ya Zain, Ismaili Said Amanzi, amesema tangu kuzinduliwa kwa Zain Foundation tayari vijana 10 wameajiriwa moja kwa moja, huku wengine wakinufaika kupitia programu mbalimbali za ukuzaji wa vipaji na ujasiriamali. Amesema dhamira ya kuanzisha taasisi hiyo ni kuhakikisha vijana wanapata fursa za kujiajiri na kuendesha maisha yao bila kutegemea wengine. "Lengo letu ni kuwainua vijana wa Keko na kuwafanya wajitegemee kiuchumi. Tunataka watoke kwenye utegemezi na waweze kujenga maisha yao kupitia kazi na vipaji walivyonavyo," amesema. Kwa mujibu wa Amanzi, Zain Foundation ilianza Keko kwa makusudi il...