Skip to main content

Posts

Showing posts from August, 2026

TMA YATOA UTABIRI WA HALI YA HEWA, YAWAONYA WANAOTUMIA BAHARI

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa utabiri wa hali ya hewa wa saa 24 kuanzia saa 3:00 usiku wa Agosti 19, 2026, ikieleza kuwa baadhi ya maeneo nchini yanatarajiwa kuwa na mawingu kiasi, mvua na ngurumo, huku maeneo mengine yakitarajiwa kuwa na vipindi vya jua. Kwa mujibu wa TMA, mikoa ya Kagera na Mara inatarajiwa kuwa na hali ya mawingu kiasi, mvua na ngurumo katika maeneo machache pamoja na vipindi vya jua. Mikoa ya Arusha na Kilimanjaro inatarajiwa kuwa na mawingu kiasi, mvua nyepesi katika maeneo machache na vipindi vya jua. Aidha, Visiwa vya Unguja na Pemba, Kigoma, Tabora, Katavi, Manyara, Dodoma, Singida, Mwanza, Geita, Shinyanga, Simiyu, Pwani ikiwemo Mafia, Tanga, Dar es Salaam, Morogoro, Lindi, Mtwara, Ruvuma, Mbeya, Rukwa, Iringa, Njombe na Songwe vinatarajiwa kuwa na hali ya mawingu kiasi pamoja na vipindi vya jua. Mawimbi makubwa baharini TMA imesema upepo wa Pwani unatarajiwa kuvuma kwa kasi ya hadi kilomita 30 kwa saa katika Pwani yote, ukitoka Kusini...

Utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24,zijazo kuanzia leo Agust 18,2026

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa utabiri wa hali ya hewa wa saa 24 kuanzia saa 3:00 usiku wa Agosti 18, 2026, ikieleza kuwa baadhi ya maeneo nchini yanatarajiwa kukumbwa na mawimbi kiasi, mvua na ngurumo pamoja na vipindi vya jua. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, katika mikoa ya Kagera, Mara na Simiyu, kunatarajiwa hali ya mawimbi kiasi, mvua na ngurumo katika maeneo machache pamoja na vipindi vya jua. TMA imesema katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro, hali ya mawimbi kiasi, mvua nyepesi katika maeneo machache pamoja na vipindi vya jua inatarajiwa. Kwa upande wa Zanzibar, ikiwemo Unguja na Pemba, pamoja na mikoa ya Kigoma, Tabora na Katavi, Mwanza, Geita na Shinyanga, Manyara, Dodoma na Singida, mvua pamoja na mawimbi kiasi na vipindi vya jua vinatarajiwa. Hali kama hiyo inatarajiwa pia katika mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Morogoro, Lindi na Mtwara, pamoja na Ruvuma, Mbeya, Rukwa, Iringa, Njombe na Songwe. Katika taarifa hiyo, TMA imeeleza kuwa kwa Pwani, kuanzia Kusi kwe...

TMA YATOA MWELEKEO WA MVUA ZA VULI OKTOBA–DESEMBA 2026, EL NIÑO YATAJWA KUCHANGIA MVUA KUBWA

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema mvua za msimu wa Vuli za Oktoba hadi Desemba 2026 zinatarajiwa kuwa za wastani hadi juu ya wastani katika maeneo mbalimbali nchini, huku uwepo wa hali ya El Niño ukitajwa kuwa miongoni mwa sababu zinazoweza kuchangia vipindi vya mvua kubwa katika baadhi ya maeneo. Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam wakati akitoa mwelekeo wa mvua hizo, Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Ladislaus Chang’a, amesema mvua hizo zinatarajiwa kuanza katika wiki ya kwanza na ya pili ya Oktoba katika baadhi ya maeneo. Amesema katika mikoa ya Arusha na Manyara, mvua zinatarajiwa kuwa za wastani hadi juu ya wastani, huku hali kama hiyo ikitarajiwa pia katika ukanda wa Kaskazini unaojumuisha Tanga, Dar es Salaam, kaskazini mwa Morogoro pamoja na visiwa vya Mafia na Pemba. TMA imesema uwepo wa El Niño unaweza kuchangia kuongezeka kwa vipindi vya mvua kubwa, hali ambayo inaweza kusababisha mafuriko na athari katika miundombinu, kilimo, usafiri na shughuli nying...

Utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24, zijazo

 

Utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24, zijazo kuanzia leo Agust 16,2026

 

JAJI MSHIBE ASISITIZA MAANDALIZI YA KISEKTA KATIKA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NIÑO

Dodoma, 14 Agosti 2026:  Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Mheshimiwa Jaji Mshibe Ali Bakari, amezitaka sekta zote nchini kutumia ipasavyo taarifa za hali ya hewa katika kufanya maandalizi ya kisekta ya kukabiliana na athari zinazoweza kusababishwa na uwepo wa El Niño. Mhe. Jaji Mshibe aliyasema hayo wakati akifungua Mkutano wa 25 wa kujadili Utabiri wa Msimu wa Mvua za Vuli, Oktoba hadi Disemba 2026, uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa PSSSF, Dodoma “Tunapojiandaa kupokea taarifa ya utabiri wa mvua za Vuli, Oktoba hadi Disemba 2026, ni muhimu kila mmoja wetu kuwa na jukumu la kufuatilia kwa karibu na kuelewa taarifa hizo ili kuanza maandalizi ya hatua za kuchukua katika kukabiliana na athari za hali ya hewa zinazotarajiwa kujitokeza katika sekta yake, kwa kutambua kuwa upo uwezekano mkubwa kwa El Niño kuendelea kuimarika kuelekea mwishoni mwa mwaka 2026,” alisisitiza Mhe. Jaji Mshibe. Mhe. Jaji mshibe aliongeza kuwa Tanzania, kama ilivyo kwa nchi n...

JKCI YATAKIWA KUENDELEZA KAMBI ZA MATIBABU YA MOYO NCHINI COMORO

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imetakiwa kuangalia namna ya kupeleka huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo nchini Comoro kutokana na huduma hizo kutopatikana nchini humo. Rai hiyo imetolewa leo na Balozi wa Tanzania nchini Comoro Mhe. Dkt. Salim Hamad alipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt. Peter Kisenge kuona namna ambavyo huduma zinazotolewa na JKCI zinaweza kuwakomboa wananchi wa Comoro. Dkt. Hamad alisema baada ya JKCI kuweka kambi maalumu ya matibabu ya moyo katika kisiwa cha Anjouan kilichopo nchini Comoro uongozi wa kisiwa hicho umeitaka JKCI kuingia mkataba nao wa kuendelea kufanya kambi za matibabu jambo ambalo linaonesha umahiri wa huduma zinazotolewa na wataalamu wa JKCI.“Nilifurahi nilipokutana na uongozi wa kisiwa cha Anjouan na kuniomba niwajulishe kuwa wanataka tuingie nao mkataba wa kufanya kambi za matibabu, hii ni hatua kubwa kwa nchi yetu katika kutoa huduma bingwa za matibabu ...

Utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24, zijazo

  Usikose kufuatilia utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24 zijazo kuanzia leo tarehe 13,2026

KIZIMKAZI 2026: WIZARA YA NISHATI YAENDELEA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

Wataalam wa Wizara ya Nishati wanaendelea kutoa elimu na ufafanuzi kwa wananchi wanaotembelea Banda la Wizara na taasisi zake katika Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi 2026, yanayofanyika Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar. Wananchi wanapata fursa ya kufahamu shughuli, miradi na huduma mbalimbali zinazotekelezwa katika sekta ya nishati, ikiwemo masuala ya umeme, mafuta, gesi asilia na nishati safi ya kupikia. Karibu tukuhudumie.

TFS YAWAPA ELIMU WACHONGAJI VINYAGO MWENGE

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umewapa elimu wafanyabiashara na wachongaji wa vinyago katika eneo la Mwenge jijini Dar es Salaam kuhusu sheria, kanuni na taratibu za uvunaji, usafirishaji na biashara ya mazao ya misitu, ikiwemo namna ya kusafirisha bidhaa hizo nje ya nchi. Akizungumza wakati wa zoezi hilo jana, Agosti 12, 2026, Mhifadhi wa Misitu wa TFS Wilaya za Kinondoni na Ubungo, Dotto Ndumbikwa, alisema hatua hiyo inalenga kuwawezesha wafanyabiashara kuelewa taratibu zinazotakiwa, kufanya biashara zao kwa ufanisi na kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza kutokana na kutofuata sheria. Ndumbikwa alisema TFS imeambatana na wahifadhi kutoka Kanda ya Mashariki, wakiwemo wanaosimamia shughuli za misitu katika eneo la Uwanja wa Ndege, kwa lengo la kusikiliza changamoto za wafanyabiashara na kuzitafutia ufumbuzi. “Tunapokaa kuwasikiliza na kuwapa elimu, inawasaidia wao kuendelea na biashara zao vizuri bila kupata matatizo,” alisema. Aliwataka wafa...

RAIS SAMIA ATAMBUA MCHANGO WA WIZARA YA NISHATI NA TAASISI ZAKE KATIKA KUFANIKISHA MDAHALO WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

KIZIMKAZI, ZANZIBAR Wizara ya Nishati pamoja na taasisi zake imetunukiwa tuzo ya kutambua mchango wake katika kufanikisha Mdahalo wa Nishati Safi ya Kupikia, uliofanyika Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 11 Agosti 2026. Tuzo hiyo imetolewa usiku wa kuamkia tarehe 12 Agosti 2026 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na kupokelewa kwa niaba ya Wizara ya Nishati na taasisi zake na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba. Mdahalo huo, uliokuwa na lengo la kujadili namna ya kuongeza kasi ya upatikanaji na matumizi ya nishati safi ya kupikia iliyo endelevu, salama na nafuu kwa wananchi na taasisi, uliwakutanisha wadau mbalimbali kutoka Serikalini, sekta binafsi, washirika wa maendeleo, taasisi za fedha, wanateknolojia, watafiti na asasi za kiraia. Mdahalo huo uliandaliwa na Taasisi ya Mwanamke Initiatives Foundation (MIF), kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhamasisha na kuchagiza hatua za pamoja kati...

WMA MSHINDI WA PILI NANE NANE KANDA YA ZIWA MASHARIKI

Na WMA - NYAKABINDI, SIMIYU  Wakala wa Vipimo (WMA) umefanikiwa kupata nafasi ya Mshindi wa Pili katika kundi la Taasisi za Umma kwenye Kilele cha Maonesho ya Wakulima, Wafugaji na Wavuvi (Nane Nane) Kanda ya Ziwa Mashariki. Maonesho hayo yaliyohusisha mikoa ya Mara, Simiyu na Shinyanga yalifanyika katika Viwanja vya Nyakabindi, Mkoa wa Simiyu na kumalizika kwa ushindi huo mnono kwa WMA.  Mgeni Rasmi katika Hafla ya kilele cha maonesho hayo alikuwa ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo ambaye ndiye aliwakabidhi WMA cheti na kikombe cha ushindi wa pili sambamba na washindi wengine. Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Meneja wa WMA Mkoa wa Simiyu, Bi. Happy Titi alisema ushindi huo ni matunda ya jitihada za WMA katika kutoa elimu kwa wakulima na wafanyabiashara kuhusu umuhimu wa kutumia vipimo sahihi. “Tunamshukuru Mungu na tunampongeza Afisa Mtendaji Mkuu na wafanyakazi wote. Ushindi huu unatupa nguvu zaidi ya kuendelea kuelimish...

TTCL YAWEKEZA MIUNDOMBINU KUBORESHA HUDUMA KWA WATEJA

  Na Mwandishi Wetu Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kuwekeza katika miundombinu ya mawasiliano pamoja na mifumo ya ndani na nje kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wateja na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma. Akizungumza kuhusu maboresho hayo, Mbanguka amesema uwekezaji huo umeiwezesha TTCL kuendelea kutoa huduma bora za mawasiliano kwa wananchi, huku ikiimarisha mifumo inayowezesha kuwahudumia wateja kwa urahisi na kwa gharama nafuu. “TTCL imekuwa kinara katika utoaji wa huduma bora za mawasiliano. Haya yote yanawezekana kutokana na miundombinu ambayo tumeiboresha zaidi, lakini pia uwekezaji katika mifumo ya ndani na mifumo ya nje ya namna ya kuwahudumia wateja wetu kwa urahisi na unafuu zaidi,” amesema Mbanguka. Amesema shirika hilo litaendelea kuboresha miundombinu yake ili kuhakikisha huduma za mawasiliano zinawafikia wananchi katika maeneo mbalimbali nchini, sambamba na kuimarisha mifumo ya huduma kwa wateja. Mbanguka ameongeza kuw...

WAZIRI NDEJEMBI AANZA ZIARA MAALUM MKOANI SHINYANGA

  Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb.), amewasili mkoani Shinyanga kwa ziara maalum ya kikazi ya kukagua utekelezaji na kuzindua miradi ya maendeleo, pamoja na kuzungumza na wananchi katika wilaya za Mkoa wa Shinyanga. Waziri Ndejembi, ambaye ni Mlezi wa Mkoa wa Shinyanga Kiserikali, mara baada ya kuwasili amefika katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Mboni Mhita, tarehe 09 Agosti 2026. Waziri Ndejembi akiwa mkoani hapo, atakagua mradi wa ujenzi wa barabara ya Kahama – Kakola, mradi wa ujenzi wa jengo la Mama na Mtoto katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama, kukagua ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Shinyanga, pamoja na kuwasha umeme wa REA katika Kitongoji cha Mwanubi, Kolandoto.

Utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24, zijazo

KILA KILO INAYOPOTEA NI SHILINGI INAYOPOTEA - MENEJA FEDHA WA WMA ATOA SOMO NANE NANE

Na WMA - DODOMA. Meneja wa Fedha wa Wakala wa Vipimo  (WMA), Bw. Ibrahim Mbinga, amesema usimamizi mbovu wa vipimo ndiyo adui mkubwa wa mfuko wa mfanyabiashara, mkulima na mnunuzi. Akizungumza na wadau katika banda la WMA kwenye Maonesho ya 33 ya Nane Nane, Dodoma, Agosti 8, 2026 Meneja huyo amefafanua jinsi vipimo visivyo rasmi vinavyosababisha upotevu wa fedha usioonekana. Mbinga ameeleza kuwa majukumu ya WMA yanalenga kuokoa wafanyabiashara, wakulima na walaji. “Watu wengi wanafikiri kupima kwa ndoo au visado ni rahisi. Lakini ukweli ni kwamba unajipiga risasi mguuni. Kila kilo, kila lita iliyopotea ni shilingi iliyotoka mfukoni mwako,” alisema. Akidadavua kuhusu hesabu ya fedha kwenye vipimo, alisema vipimo ni sawa na mfuko wa fedha. “Gunia la mahindi kilo 100 ukiuza kwa ndoo 18 badala ya mizani, unapoteza kilo 10. Kama gunia ni shilingi 100,000, umepoteza shilingi 10,000. Ukiuza magunia 10 kwa wiki, umepoteza shilingi 100,000. Kwa mwezi ni milioni 1.2. Hiyo pesa ingekuwa wapi?...

WMA YAMUAHIDI MKUU WA WILAYA YA IRAMBA KUIMARISHA UTENDAJI KAZI KWENYE VIPIMO

Na WMA - DODOMA. Wakala wa Vipimo (WMA) umemhakikishia Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Mhe. Selemani Mwendwa kuwa utaongeza kasi ya utendaji kazi wa masuala ya vipimo katika wilaya hiyo ili kulinda uchumi wa wakulima na wafugaji. Hakikisho hilo limetolewa jana Agosti 8, 2026 alipotembelea banda la WMA kwenye Maonesho ya 33 ya Wakulima Nane Nane, Viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela, Dodoma, na kupatiwa elimu ya vipimo. Meneja wa WMA Mkoa wa Singida, Bw.  Willie Amosi alisema kuwa "WMA itashirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kuratibu na kutoa elimu ya vipimo katika maeneo mbalimbali ya Iramba kwa  lengo la kufikia wakulima wa mahindi, alizeti na pamba pamoja na wafugaji kwenye minada na masoko. Aidha,  alimjulisha  Mkuu wa Wilaya kuwa WMA  itajipanga ili  kuanzisha Klabu za Vipimo (Vipimo Clubs) katika shule mbalimbali  za msingi na sekondari ikiwa ni mikakati ya kufika Tanzania nzima, hususan Tanzania Bara ambao ndiyo uwanda wa WMA.  Vilevile, Meneja ...

KIONGOZI MSTAAFU WA WMA ASEMA VIPIMO SAHIHI NDIYO MSINGI WA UCHUMI

Na WMA - DODOMA. Kiongozi mstaafu wa Wakala wa Vipimo (WMA), aliyekuwa Mkurugenzi wa Huduma Saidizi Bw. Deogratius Aloyce Maneno amesema uwekezaji wa Serikali katika masuala ya vipimo ndiyo ufunguo wa kujenga uchumi imara na soko la haki. Alisema hayo jana Agosti 8, 2026 alipotembelea banda la WMA kwenye Maonesho ya 33 ya Wakulima (Nane Nane), yaliyofanyika kitaifa katika Viwanja vya Dkt. John Malecela, Dodoma. Baada ya kupokelewa na wataalamu wa WMA na kupewa maelezo ya maboresho mapya ya vifaa na elimu ya vipimo, Mkurugenzi Mstaafu alisema anajivunia kuona kazi aliyoshiriki kuianzisha ikiendelea na kukua. “Nimefurahishwa sana kuona WMA imepiga hatua kubwa. Tulipoanza tulikuwa na changamoto za vifaa na uelewa, lakini leo naona vijana wanasimama wenyewe kutoa elimu. Hii ndiyo tija ya uwekezaji,” alisema. Kutokana na uzoefu wake wa miaka mingi WMA, kiongozi huyo alitoa ushauri katika maeneo kadhaa ili kuboresha zaidi huduma za uhakiki wa vipimo.  Kwanza, alisema kuwa ni jambo jema k...

MTENDAJI MKUU WMA AHAMASISHA WANANCHI KUTUMIA MIZANI ILIYOHAKIKIWA

Na WMA - DODOMA WAKALA wa Vipimo  (WMA) umewataka wafanyabiashara na wananchi kuacha mara moja matumizi ya vipimo visivyo rasmi, ikiwemo ndoo, mafungu, visado na makopo, katika uuzaji wa mazao ya kilimo na mifugo na badala yake kutumia mizani iliyohakikiwa kwa mujibu wa sheria. Wito huo umetolewa na Afisa Mtendaji Mkuu wa WMA, Alban Kihula, leo Agosti 8, 2026 wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya 33 ya Kitaifa ya Siku ya Wakulima Nane Nane, yaliyokuwa yakifanyika katika Viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela, jijini Dodoma. Kihula amesema matumizi ya vipimo visivyo rasmi yanaweza kusababisha kutokuwepo kwa usawa katika biashara na kuwaathiri wananchi kwa kuwafanya wasipate thamani halisi ya bidhaa wanazonunua au kuuza. Amesema WMA imeendelea kutoa elimu kwa wananchi, wakulima, wafugaji na wafanyabiashara kuhusu matakwa ya Sheria ya Vipimo, Sura ya 340, ikiwemo namna ya kutambua vipimo vilivyohakikiwa na uwekaji wa alama sahihi kwenye bidhaa zilizofungashwa. “I...

WANAFUNZI WA MTEMI MAZENGO WATOA ELIMU YA VIPIMO KWA NAIBU WAZIRI LONDO NANE NANE

Na WMA - DODOMA. Wanafunzi wa Klabu ya Vipimo (Vipimo Club)  kutoka Shule ya Msingi Mtemi Mazengo ya jijini Dodoma, wamegeuka walimu kwa siku moja baada ya kumpa elimu ya vipimo Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo, katika banda la Wakala wa Vipimo  (WMA), kwenye Maonesho ya 33 ya Wakulima Nane Nane, Dodoma. Leo Agosti 7, 2026, Naibu Waziri Londo alishangazwa na ufasaha wa wanafunzi hao walipomweleza umuhimu wa vipimo sahihi, kuandika kwa usahihi vifungashio katika bidhaa zilizofungashwa pamoja na madhara ya lumbesa. “Nimefurahishwa sana. Watoto hawa ni mabalozi wazuri wa jamii. Uwekezaji wa WMA katika kizazi kijacho unaleta matokeo,” alisema. Wanafunzi hao walikuwa katika ziara iliyoratibiwa na Wakala wa Vipimo ikiwa ni sehemu ya mpango wa elimu ya vipimo kwa vitendo.  Mkakati wa WMA ni  kuwajengea wanafunzi uelewa wa vipimo kwa nadharia na vitendo ambapo  leo wanafunzi hao wa Klabu ya Vipimo ndiyo walikuwa wakitoa huduma zote bandani ikiwemo ...

TIRDO YALEA UBUNIFU WA VIWANDA, YASUKUMA TEKNOLOJIA ZA KUONGEZA THAMANI YA MAZAO

  Na Ayra News  Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) limesema linaendelea kuwa chachu ya maendeleo ya viwanda kwa kuhamasisha matumizi ya teknolojia za kuongeza thamani ya mazao ya kilimo, hatua inayolenga kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvunwa na kuongeza kipato kwa wakulima na wajasiriamali. Akizungumza katika Maonyesho ya Nanenane 2026,Mtaalam na Mtafiti wa Teknolojia za Nishati, Mhandisi Augustino Masse kutoka TIRDO alisema shirika hilo linaimarisha mnyororo wa thamani wa mazao kupitia utafiti, ubunifu na teknolojia zinazosaidia mazao kudumu kwa muda mrefu bila kupoteza ubora wake. Alisema kuwa, tafiti zinaonesha kuwa zaidi ya asilimia 40 ya mazao yanayoharibika kwa haraka, yakiwemo nyanya, matunda na mboga za majani, hupotea kutokana na ukosefu wa teknolojia sahihi za uhifadhi na usindikaji. Kutokana na hali hiyo, TIRDO imeendelea kuhamasisha matumizi ya makaushio yanayotumia nishati ya jua, teknolojia inayowezesha mazao kukauka kwa viwango vin...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...