Skip to main content

BINT CCM YAWASHIKA MKONO KCC, KUELEKEA MIAKA 46 YA CCM

 


Na Mwandishi wetu HPMedia, Dar es Salaam 

Katika kuelekea miaka 46 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mabinti wa Chama cha Mapinduzi ( Binti Ccm) wametembelea kituo cha KCC kilichopo Kigamboni jijini Dar es Salaam cha kulea watoto yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi na kutoa msaada wa vitu mbalimbali vyenye thamani isiyopungua millioni moja 1.

Akizungumza na Mtandao wa Habari Plus Media, Mmoja wa wanzilishi wa Kampeni ya Binti CCM Twilumba Jane amesema msaada huo walioutoa kwa watoto hao ni muendelezo wa kuwafikia watu wenye mahitaji mbalimbali ya kijamii,ambapo wamekua wakifanya hivyo kwa miaka kadhaa tangu kuanzishwa kwa umoja huo. 

Amesema kuwa, miongoni mwa vitu ambavyo wametoa katika kituo hicho ni pamoja na mchele kilo 50, unga kilo 50, mafuta lita 10, sukari kilo 20, maharage kilo 20, counterbook dozen 2, sabuni ya unga kilo 25, sabuni ya mche dozen 1 na nusu, viatu pea zisizopungua 20,nguo pamoja na mabegi ya shule 10.

Aidha, amesema kuwa pamoja na mambo mengine lengo la BintiCCM ni kuhakikisha wanawafikia wahitaji wengi zaidi kwa kuwapatia mahitaji yao muhimu, elimu (capacity building ) n.k.

Ameongeza kuwa, malengo ya kampeni ya Binti CCM ni kujifunza kwa kuhamasishana wenyewe kwa wenyewe kuwa na moyo wa kujitoa kwa ajili ya wahitaji na hata baina yao na kushirikiana katika shughuli zao mbalimbali wanazozifanya za kiuchumi, kijamii, kielimu na hata kisiasa yaani Chama cha Mapinduzi.

"Leo tumefika hapa KCC kigambo na kampeni yetu ya "tuwape tabasamu" kuwafariji watoto hawa, tume furaha pamoja,tumekata keki, tumecheza nao michezo mbalimbali kwa kweli ilikua ni jambo zuri sana kwani hata sisi tumejifunza pia kutoka Kwao"amesema Imelda Antony ambaye ni mratibu wa kampeni ya BintiCcm Mkoa wa Dar es salaam.



Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...