Skip to main content

MATHAMANI - SIJAKATAA UTEUZI



Na mwandishi wetu,HPMedia, Kigoma

Aliyekua Makamu wa Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Dinah Elias Mathamani amesema hajakataa uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Mkoani kigoma aliyoteuliwa na Rais wa Jamhuribya muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan uliofanyika January 25, 2023.


Kauli hiyo ameitoa  January  31 mbele ya waandiahibwa habari mara baada ya kula kiapo cha uongozi kwa nafasi ya Mkuu wa Wilaya mbele ya mkuu wa Mkoa wa kigoma Thobias Andengenye katika ukumbi wa Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma.


Amesema kuwa, amesikitishwa na taarifa zilizokua zinasambaa kwenye mitandao ya kijamii ya kuwa amekataa nafasi ya uteuzi aliyopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kudai kuwa hazina ukweli wowote bali amefurahishwa sana na uteuzi huo na kuwa yupo tayari kuitumikia katika kiapo cha maadili ya uongozi.


"Baada ya majina kutangazwa na kuona jina langu ni mmoja wa wateule nilifurahi na nikaanza kufanya mawasiliano na viongozi wa Wilaya yangu na kujiandaa na safari ya kuja kwenye kituo changu cha kazi, niliona ni nafasi ya pekee kwangu na ninamshukuru sana Rais Samia kwa nafasi hii aliyonipa ya kuwatumikia wananchi"amesema DC Dinah.


Ameongeza kuwa, imani aliyopewa na Rais Samia ya kumteua kuwatumia wananchi atahakikisha anaitendea haki kwa kufanya kazi usiku na mchana ili kuleta maendeleo katika Wilaya hiyo na kusimamia ilani ya chama cha Mapinduzi ili itakapofika mwaka 2025 wapate cha kuwaeleza wananchi.


Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amewataka wakuu wa Wilaya zote za Mkoa wa Kigoma kuendelea kusimamia suala la ulinzi na usalama kwenye Wilaya zao kwani wahamiaji haramu wamekuwa wakiingia kupitia njia ambazo siyo za halali hivyo amewataka waweke uthibiti wa njia hizo ambazo si halali kwa wahamiaji kuingia.



"Rais amewaamini akijua uwezo wenu,mtumie vizuri mamlaka mliyonayo huku mkitambua majukumu yenu yanagusa maisha ya wananchi,wahamasisheni wananchi wajiunge na bima ya afya inayokuja bima ya afya kwa wote na bima zingine ili wawe na uhakika wa matibabu pale wanapougua wao na familia zao"amesema Andengenye.


Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...