Skip to main content

MWENYEKITI ILALA ATOA MAAGIZO HAYA KWA VIONGOZI KATA YA LIWITI, SEGEREA NA TABATA

 

Na Mwandishi wetu, HPMedia, Dar es Salaam

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ilala Said Sidde amewataka Madiwani na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa kutoa taarifa za utekelezaji wa Ilani ya chama hicho kwa wenyeviti wa mashina ili waweze kuwaambia wanachama wao kazi zilizofanywa na serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt, Samia Suluhu Hassan.


Rai hiyo ameitoa alipokuwa katika Mkutano na viongozi wa Kata ya Liwiti, Segerea na Tabata ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake pamoja na kamati ya siasa wilaya kujitambulisha na kuwashukuru wanachama kwa kuwachagua kushika nafasi hizo, na kuahidi wapo tayari kutekeleza majukumu yao hususani katika kipindi hiki cha mkakati wa kufanya kazi za chama ndani ya chama na nje ya chama.

Amesema kuwa, mikakati yao kama viongozi wa CCM Ilala ni kuhakikisha kuwa wanashinda uchaguzi wa Serikali za mitaa 2024 kwa mitaa yote 159 na uchaguzi mkuu 2025 kushinda kata zote 36 na majimbo 3 na kura za ndio kwa Rais Dkt. Samia hivyo uongozi wa wilaya wamefanya vikao na wenyeviti wa mitaa, wabunge madiwani na wakuu wa idara pamoja na Mkurugenzi ili kuainisha maeneo yenye kero na changamoto ili zichukuliwe na serikali kuu na kufanyiwa kazi ikifika kipindi cha uchaguzi mambo yaende vizuri


"Msingi mkubwa wa vikao hivyo tulivyofanya ni maandalizi ya kujiandaa na uchaguzi wa serikali za mitaa mwakani na uchaguzi mkuu 2025 pamoja na mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa inayoendelea kwa sasa hivyo nimpongeza Mheshimiwa Rais kwa kuondoa zuio la mikutano kwani tunamengi tumefanya ya kuwaeleza wananchi na kuendana na kauli ya raisi ya kujibu hoja kwa hoja na sio matusi"amesema Mwenyekiti Sidde.

Aidha, amewataka viongozi hao kuwa na mahusiano mazuri kujua changamoto zinazowakabili wananchi na jinsi zitakavyotatulia ili wakiwa kwenye mikutano ya hadhara wawe na lakusema kwa wananchi kuwa wametekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo ikiwemo ujenzi wa shule, hospitali, matunda ya vyoo, vivuko na barabara jambo ambapo watakua wametekeleza kwa vitendo agizo la Mwenyekiti wa Chama na Rais Dkt.Samia la kujibu hoja kwa hoja kwenye mikutano ya hadhara.


"Agenda za vyama vya upinzani kuhusu bidhaa za vyakula kupanda itaisha siku si nyingine kutokana na kutolewa kwa mbolea za ruzuku ambazo zitaongeza uzalishaji na agenda za Elimu na Afya tayari CCM imeshatatua kwa kiasi kikubwa hawatakuwa na lakusema na miundombinu ya Barabara inaendelea kutatuliwa "amesema Mwenyekiti Sidde

Sambamba na hayo amesema Viongozi wa mashina ndio msingi wa chama na ndio wenye wanachama hivyo ni vyema kushirikiana nao na uwepo wa mahusiano mazuri baina yao na serikali utawawezesha kujua mambo ambayo CCM imefanya ikiwemo ujenzi wa shule zahanati vyoo na wajue gharama na faida ya miradi hiyo.

Hata hivyo amewaomba viongozi wa mashina ambao bado hawajaunda kamati yao ya watu 4 kuhakikisha kuwa wanaiunda ili kusaidia ufikishwaji wa taarifa mapema toka ngazi za tawi na kumpunguzia mzigo Mwenyekiti na balozi wa shina kutoa taarifa za mikutano kwa wananchi.

Katika hatua nyingine amewaomba Wenyeviti wa mashina kufanya vikao vya mara kwa mara kwani ndio kwenye mizizi ya chama na sehemu ambapo wananchi wanaweza kupeleka kero na changamoto zao zikapelekwa tawini na kutatuliwa na zinaposhindikana kupelekwa ngazi za juu zaidi.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...