Skip to main content

DC MPOGOLO AWATAKA WATENDAJI WASIWE KIKWAZO KWA SERIKALI


Na Mwandishi wetu, HPMedia, Dar 

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Edward Mpogolo, amewataka watendaji wa wilaya ya Ilala kuwa karibu na Viongozi wa chama na Serikali huku akiwasisistiza wasiwe sehemu ya vikwazo katika kuleta maendeleo .

Wito huo ameutoa alipokua katika ziara ya kujitambulisha kwa watendaji na viongozi wa chama Tarafa ya Ilala jijini Dar es Salaam ambapo amesema dhumuni la ziara hiyo kujitambulisha ,kujenga Mahusiano pamoja na kutatua kero mbalimbali zilizopo Wilayani humo .

"Naomba Watendaji wa Tarafa ya Ilala mshirikiane na chama na Serikali katika kujenga mahusiano pamoja na wananchi msiwe sehemu ya vikwazo ndani ya Wilaya Ilala  " alisema Mpogolo .

Aidha, amewataka Watendaji kushikamana na Serikali kutumikia wananchi katika utekekezaji wa Ilani katika kuunga mkono Juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kusimamia miradi ya Maendeleo ikiwemo ya sekta ya afya na sekta ya Elimu .

Hata hivyo, amewataka watendaji hao endapo kutatokea mtu amekosea basi wakosoane kwa staha na kwa kupitia vikao vilivyowekwa badala ya kusemana katika vijiwe na mikutano ya Wananchi .



Diwani wa Kata ya Ilala Saady Kimji, alimpongeza Mpogolo kwa mada nzuri Semina elekezi amewapatia Watendaji na Viongozi wa chama Ili kila mtu aweze jua Majukumu yake .


Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi CCM kata ya Ilala Habibu Nasser alimpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kumteua Mkuu wa Wilaya Edward Mpogolo kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala watashirikiana naye katika utekekezaji wa Majukumu yake ya Chama na Serikali .

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...