Skip to main content

SERIKALI KUHAKIKISHA ULINZI NA USALAMA MAHALI PA KAZI

 

Na Magrethy Katengu,HPMedia, Dar 

Serikali  imesema itaendelea kuheshimu mikataba ya Kimataifa kwa kuhakikisha kuwa inaweka ulinzi  na Usalama mahali pa kazi ili kusaidia  Wafanyakazi walioajiriwa au kuniajiri wanafanya kazi zao Kwa amani Ili kusaidia kuchochea Ustawi wa Jamii yenye uchumi Imara .

Akizungumza leo Jijini Dar es salaam Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Vijana Ajira na Watu wenye Ulemavu Patrobas Katambi wakati wa ufunguzi wa Warsha ya kwanza ya siku Moja kuimarisha Uhusiano Bora kati ya Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda biashara ,Taasisi za fedha huduma na ushauri(TUICO) na chama Cha Waajiri ATE ambapo amesema Serikali ina imani sekta zote za kazi kwani zina mchango mkubwa kuongeza Uchumi na Pato la Taifa kuongezeka .

"Warsha hii ya leo itakuwa chachu na kiungo muhimu cha ushirikiano wa Waajiri,Wafanyakazi pamoja na taasisi za kifedha katika kutekeleza Maadhimio ya Shirika la kazi Duniani ILO ili kuboresha mazingira rafiki katika eneo la kazi"amesema Waziri

Hata hivyo Waziri amewaasa viongozi wa vyama hivyo  kutotumia wanasiasa katika vyama vyao kuwasemea changamoto zao kwani Wana uwezo wa kukaa pamoja na kusuluhisha palipo na shida siyo kama ni hapo awali miaka ya kadhaa ya nya baadhi yao wametumia vyama hivyo kwa ajili ya maslahi yao ya kisiasa hivyo kupitia Warsha hii ya leo iwasaidie kuzungumza pamoja changamoto zenu na kuzitatua pasipo kupitia viongozi wanasiasa

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda biashara,taasisi za fedha ,huduma na Ushauri (TUICO)Paul Sangeze amesema Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi waandamizi waliohudhuria itakuwa chachu yale yatatakayojadiliwa italeta tija kwa kwa kuboresha mazingira mahala pa kazi.

Kwa Upande wake Afisa Mkuu Mtendaji wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE)  Suzanne Naomba amesema Waajiri haki ya kujiunga na Chama Cha Wafanyakazi ipo kikatiba mtu binafsi hashurutishwi anajiunga kwa hiari yake mwenyewe na anatakiwa afuate utaratibu..

Aidha Waajiri ni Wadau wakubwa hivyo ushirikiano huo utasaidia kutatua changamoto mahala pa kazi hivyo ni vyema mikaba yote yote ya kazi ifanyike kwa uwazi na majadiliano yafanyike Kwa Nia njema pande zote waridhike

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...