Skip to main content

ACT YATOA HOJA 7 KWA SERIKALI

Na Magrethy Katengu,HPMedia,Dar 

Chama cha ACT Wazalendo kimetoa hoja 7 mara baada ya hotuba ya Ofisi ya Waziri Mkuu kuhusu mapitio ya kazi na mwelekeo wa serikali na makadirio ya matumizi kwa mwaka wa fedha 2023/2024 hoja ikiwemo hali ngumu ya maisha,suala la ukosefu wa ajira,kukosekana kwa utaratibu wa kukabiliana na maafa ,kuchelewa kwa Miradi ya kimkakati.

Hoja hizo saba zimetolewa  leo Jijini Dar es saalam Waziri Mkuu kivuli chama cha ACT Wazalendo Dorothy Semu wakati akichambua Hotuba ya Ofisi  ya Waziri Mkuu kuhusu mapitio ya kazi na mwelekeo wa serikali makadirio ya matumizi kwa mwaka wa fedha 2023/2024 iliyowasilishwa Aprili 05 2023 Bungeni na Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa ambapo amesema Serikali iliyo chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan inahitaji Mabadiliko makubwa ya kiuchumi hivyo wametoa hoja zao zifanyiwe kazi.

Dorothy akifafanua hoja ya hali ngumu ya maisha amesema kutokana na Mabadiliko ya hali ya hewa serikali iangalie na namna ya kununua chakula cha kutosha angalau miezi 3 kutokana chakula kitakachovunwa mwaka huu ili kujiandaa na upungufu wa chakula kutokana na ukweli kuwa maeneo mengi nchini uzalishaji unaweza ukawa siyo mzuri hivyo ni vyema kuchukua tahadhari mapema

"Hatua hii ya kunusuru nchi na janga la ukosefu wa chakula na kusababisha njaa serikali kujenga uwezo wa wakala wa Taifa wa hifadhi ya chakula (NFRA) Kwa kutenga bajeti ya kutosha ya kununua chakula (Tan million 1.5 za mahindi ,Tani laki 5za mpunga ,maharagwe Tani milioni 1) na kuwezesha Bodi ya mazao mchanganyiko kununua na kusambaza katika maeneo yatakayokuwa na uhaba wa chakula"amesema Semu

Hata hivyo ameishauri serikali iweke mazingira bora Kwa wakulima wadogo Ili kuongeza uzalishaji zaidi Kwa kuendelea kutoa ruzuku katika mbolea na kusimamia usambazaji wake kuhakikisha usalama wa ardhi kwa wakulima na kushughulikia migogoro ya ardhi.

Sanjari na hayo akifanua hoja nyingine ya ukosefu wa ajira na maslahi ya Wafanyakazi amesema athari ni janga kubwa sana katika Jamii yetu husababisha ikiwemo kuongezeka wimbi la umasikini na utegemezi, kuongezeka kwa mmomonyoko wa maadili na uhalifu ikiwemo vitendo vya wizi,ukahaba,unyang'anyi,uporaji,kuongezeka kupendeleana na rushwa katika utolewaji wa ishughulikiwe mara Moja

Aidha, amesema katika sekta mbalimbali kumekuwa na uhitaji wa wataalamu hivyo na Vijana waliohitimu wapo wengi mtaana hawajui pa kwenda serikali iangalile suala hilo kwa jicho angavu 

"Tumedhuhudia mahitaji makubwa ya wafanyakazi na watumishi tena kwenye sekta nyeti kama vile Elimu,afya na kilimo lakini serikali hajaweka Mkazi kabisa kwenye kuhakikisha sekta hizo zinapata wataalamu na watumishi licha ya kuwepo wataalamu waliosomeshwa Kwa gharama kubwa na kuwaacha mtaani hivyo tunashauri serikali kupatia ufumbuzi jambo hilo "amesema Dorothy 

Aidha Serikali imeshauriwa kujenga uwezo wa kibajeti kununua vifaa vya kisasa vya uokoaji kujenga uwezo Idara ya maafa na taasisi zilizo chini yake kununua vifaa vya kuongeza ufanisi wa usimamizi wa kutumia Teknolojia ya Kufuatilia maafa sehemu mbalimbali za nchi

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...