Skip to main content

UWT KUNDUCHI YATOA ELIMU YA UKALITI NA MAADILI MEMA KWA WANAFUNZI 5000




Na Mwandishi wetu HPMedia, Dar 

Umoja wa Wanawake Kata Kunduchi (UWT) imewajengea uwezo wanafunzi zaidi ya 5000kutoka Shule ya Sekondari Kondo, Shule za Msingi Pius Msekwa na Shule ya Msingi Kunduchi lengo ikiwa ni kuwataka watambue cha kufanya hasa wanapotendewa ukatili wa kijinsia ama wanapokutana nao.

Akizungumza na wanafunzi katika ziara hiyo, Mwenyekiti wa UWT Kata ya Kunduchi Twilumba Jane Balama amesema watahakikisha wanawafikia wanafunzi wote katika shule zilizopo kwenye Kata ya Kunduchi ili kuisaidia Serikali kupambana na ukatili na hasa kutengeneza kizazi kilicho bora zaidi kwa maslahi mapana ya nchi ya Tanzania.

Amesema kuwa, lengo kufanya ziara hiyo ni kutokana na vitendo vya ukatili wa kijinsia  kuongezeka siku hadi, hivyo wameona ni jambo jema kuanzia mashuleni ambako ndio kuna wahanga wakubwa.

"Tumeona tuanzie mashuleni kwani watoto wengi ndio waathirika wa vitendo vya ukatili  kwa hiyo tumewafikia watoto wasiopungua 5000 na kuzungumza nao kuhusu maadili mema na namna ya kutambua ukatili wa kijinsia na nini cha kufanya endapo watakutana na ukatili"amesema Twilumba. 

Hata hivyo, amewashukuru wadau wote kwa kuweza kufika kuungana nao katika kutoa elimu hiyo ya malezi na maadili bora kwa watoto waliopo mashuleni ambapo itaweza kuwafikia watoto wengi zaidi.

Aidha, katika ziara hiyo waliambatana na Katibu UWT Wilaya ya Kinondoni Aziat Juma, Mjumbe Halmashauri Kuu CCm Mkoa wa Dar es Salaam Francis Nanai, Diwani wa Kata ya Kunduchi  Michael Urio, Dawati la Jinsia Mkoa wa Kawe, mwakilishi kutoka SMAUJATA Irene Mashine, Afisa Ustawi wa jamii na Afisa Maendeleo Kata ya Kunduchi ambao wote walikuwa wazungumzaji katika ziara hiyo.

Mbali na kuwajengea uwezo, UWT Kunduchi waliwapa Motisha watoto hao kwa kuwapa zawadi (counter books, mathematical sets, kalamu na penseli) wanafunzi walioibuka Tano bora katika Kila darasa.

Aidha Michael Urio ambae ni Diwani wa Kata hiyo,ametoa wito kwa wakuu wa shule kuandaa mkutano na wazazi ambapo Uwt Kunduchi pamoja na wadau wote waliofika kuwajengea uwezo watoto hao waweze kuzungumza na wazazi kuhusu malezi bora kwa watoto wetu.



Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...