Skip to main content

ONESHO LA KWANZA LA EONII JUNE 23, MLIMANI CITY

 

Na Mwandishi wetu HPMedia, Dar 

Kampuni ya Azam Media Ltd (AML) kwa kushirikiana na Studio za PowerBrush (PBS) wanatarajia kuonesha  rasmi filamu ya Kisayansi ya EONII Juni 23, 2023 katika Ukumbi wa Century Sinemax Mlimani City Jijini Dar es salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam Afisa Mwendeshaji Mkuu wa Azam Media, Divisheni ya Maudhui na Utangazaji Yahya Mohamed amesema mipango yote muhimu imekamilika tayari kwa Onyesho hilo  la kwanza la uzinduzi wa kihistoria.

"Tutumie fursa hii kwa niaba ya Azam Media Ltd na PowerBrush Studios kutambua mchango makubwa wa Serikali yetu katika kusimamia michezo na sanaa nchini na kuweka mipango endelevu ambayo tunashuhudia matunda yake kupitia mageuzi haya kwenye tasnia ya Filamu nchini,"amesema Mohamed.

Aidha, amesema kuwa bodi ya Filamu wamekuwa mhimili mkubwa katika kutoa hamasa, kuratibu njia sahihi za kuisukuma sanaa ya Filamu na kipekee amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka chachu iliyopeleka saa sasa ya Filamu Kimataifa.

Ameongeza kuwa, hamasa hizo na sera na kanuni madhubuti timu yao ya uzalishaji pamoja na PowerBrush Studios wamewekeza katika ubunifu na umakini mkubwa kunadaa Filamu ya EONII ambayo inasukuma mipaka ya kuwaza na kusimulia hadithi.

Amesema juhudi hizo za kipekee ni uthibitisho wa kukua kwa vipaji na matamanio ndani ya Tasnia ya Filamu Tanzania

"Nimatarajio yetu viongozi na waalikwa wengine watakuwa mabalozi Wazuri baada ya onyesho la Awali la Premier siku ya Ijumaa Juni 23, 2023 pale Mlimani City, mabali na onyesho kuu la Dar es Salaam, EONII itaoneshwa katika mikoa ya Dodoma, Arusha, Tanga na Mwanza kwa upande wa Tanzania Bara, huku Zanzibar ikiwa kituo muhimu," ameeleza Mohamed.

Kwa upande wake, Katibu Mtendaji bodi ya filamu Dkt Kiagho Kilonzo amesema Filamu hiyo ni ya kwanza ilitumia muda wa miaka minne na kugharimu dola laki mbili ikiwa imebeba maudhui ya uhitaji wa nishati ambapo nchi ikiwa katikati ya Ombwe la kukosekana kwa nishati ndiyo filamu inakuja. 

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...