Skip to main content

WANANCHI WATAKIWA KUKUZA UCHUMI MKUTANONWA RASILIAMALI WATU

 

Na Mwandishi wetu HPMedia, Dar 

Imeelezwa kuwa kupitia mkutano wa kimataifa wa wakuu wa nchi za Afrika kuhusu rasilimali watu  utakaofanyika Julai 25 hadi 26 jijini Dar es Salaam utasaidia kukuza pato la taifa na kuimarisha uchumi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Albert Chalamila amesema kuwa, mkutano huo ni matunda ni Rais Dkt Samia katika kuifungua nchi na kutangaza utalii  wa ndani hivyo kupitia mkutano huo kutakua na fursa na nyingi za kukuza uchumi.

Amesema kuwa, mkutano huo utahudhuriwa na wageni 1200 kutoka katika nchi hizo ambao watakula na kulala katika holeti zaidi ya 40 ambapo wafanyabishara zaidi ya 100 wameshaandaliwa vizuri kuhusu bidhaa zao pamoja na uuzaji wao jambo ambalo litatoa fursa nyingi kwa hususani kwa watanzania ambao ndio wenyeji wa mkutano huo.

"Kupitia ugeni huu watanzania hawana budi kutumia fursa hiyo kuweza kutangaza utalii wa ndani pamoja na kutangaza biashara zao, mahoteli, kupika vyakula vya kitanzania kwani hii ni sehemu ya utalii hiyvyo lazima wachangamkie fursa "amesema Rc Chalamila.

Kwa upande wake,Mkurugenzi wa ukumbi wa kimataifa JNCC Ephraim Makuru amesema kumbi zote za JNCC zipo tayari kwa ajili ya mikutano na kuwa kila nchi inahitaji kupata taarifa kwa lugha zao vifaa vimekamilika ili kila mgeni atakapoondoka kurudi nchini kwao aondoke akiwa na furaha na neno Asante Tanzania.



Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...