Skip to main content

WAZIRI PROF MKENDA AITAKA BODI YA MAKTABA KUEKEZA UNUNUZI WA VITABU.

 

Na Mwandishi wetu,  HPMedia, Dar 

Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof Adolf Mkenda ameitaka bodi ya Maktaba kuwekeza zaidi kwenye ununuzi wa vitabu kuliko ujenzi wa majengo ya Maktaba kwani wanaweza kushirikiana na mashule kuanzisha maktaba za jumuiya.

Kauli hiyo ameitoa Jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa akitembelea ukarabati wa bodi ya huduma za maktaba ambapo amesema ni vyema kuwekeza katika ununuzi wa vitabu kuliko kujenga kwani kunachukua gharama sana.

Aidha, amesema kuwa kuna changamoto kubwa ya uandishi na usomaji wa vitabu kutokana na wanaochapisha vitabu kukosa soko ambapo baadhi ya waandishi kutumia pesa zao kugharamia na wengine huacha kabisa.


 "Zamani wakati ninasoma Maktaba zilikuwa nyingi kutokana na kuwekwa kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo kanisani, misikitini na majengo ya Serikali hivyo niishauri bodi kutafuta maeneo ambayo wataweka vitabu ili kizazi cha sasa kuweze kusoma kwani kusubiri ujenzi wa Maktaba itachukua mda na kizazi cha sasa kitakosa kusoma" amesema Prof Mkenda.

Hata hivyo amesema katika kupunguza changamoto ya ukosefu wa sehemu za kuuza vitabu vinavyochapishwa wameanzisha tuzo za uandishi ya Mwalimu Nyerere ambapo mshindi vitabu vyake Serikali itanunu na kusambaza kwenye maktaba na shuleni.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania Dkt. Mboni Ruzegea amesema lengo kuu la maktaba ni kutoa fursa kwa umma kujipatia maarifa endelevu kwa watu wote kupitia usomaji wa machapisho mbalimbali.

Hata hivyo, amesema kuwa maktaba ni chombo muhimu na moyo katika taifa hususani kukusanya na kuhifadhi nyaraka kuwapatia walengwa kwa manufaa ya sasa na vizazi vijavyo ambapo Mwal Nyerere alisema vitabu njia nzuri katika kujiendeleza na kujitegemea.

Aidha, ameiomba Serikali kuisaidia  taasisi hiyo kwa kuiongezea gari kwa ajili ya kusafirisha vitabu ambavyo vimekuwa vikigharimu gharama kubwa wakituma kupitia shirika la posta pamoja na gari kwa ajili ya huduma za chuo.

Aidha, amesema maktaba inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa fedha, Changamoto katika chuo na maktaba ambazo zipo mikoani zinazohitaji ukarabati, uhaba wa vitendea kazi na vitabu vya kiada.




Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...