Skip to main content

MAWAZIRI, WANASHERIA WAJIFUNGIA DAR KUJADILI MCHAKATO WA KATIBA MPYA

 

Na fatma Ally, HPMedia, Dar 

Waziri wa Katiba na Sheria Dkt Damas Ndumbaro amesema kuwa zaidi ya asilimia 50 ya watanzania hawaifahamu katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo wengine hawajaiona kabisa hivyo ni wajibu wao kuhakikisha watanzania wanaifahamu ili kupuuza maneno wanayoambiwa. 

Kauli hiyo ameitoa jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa akifungua kikao cha Mawaziri wa sheria na wanasheria wakuu wa Serikali wastafu na waliopo madarakani kuhusu majadiliano ya mchakato wa katiba mpya pamoja na mkakati wa Taifa wa elimu ya umma (MTEKU 2023/2026).

Amesema kuwa,ipo haja ya watanzania kueleweshwa kuhusu katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na kuijua ili kuuza maneno wanayoambiwa ambayo hayahusu katiba ikiwemo kupanda kwa bei bidhaa ikiwemo vyakula pamoja ugumu wa maisha.

"Wapo watanzania ambao hawaijui kabisa katiba na wengine hawajaiona kabisa hivyo ni muhimu kuifahamu ili yanapozungumzwa mambo yanayohusu katiba iwe ni rahisi kuweza kuyafahamu kwa upana wake, ili wasije wakaingiziwa mambo ambayo siyo ya kikatiba"amesema Dkt Ndumbaro.

Ameongeza kuwa, viongozi wa dini pamoja na viongozi wa siasa wamekua wakijadili sana kuhusu mchakato wa katiba mpya ambapo wengine wanatofautiana katika mitazamo yao juu ya mchakato wa katiba mpya.

"Wapo ambao wanataka mchakato uishie ulipoanzia, wapo ambao wanataka twende kwenye rasimu na wapo ambao wanataka sheria zibadilishwe, leo tutayapitia maoni yote ili tutoke na kauli ya pamoja kuhusu katiba mpya"amesema Waziri Dkt Ndubaro.

Aidha, amesema kikao hiko kitapokea maoni ya mchakato wa katiba mpya kutoka upande wa Tanzania bara na Zanzibar ili kufahamu ni maeneo gani ambayo yanatakiwa kufanyiwa marekebisho katika katiba ya mwaka 1977.

Kwa upande wake, Waziri Mstaafu wa Katiba na Sheria Mery Nagu amesema ujio wa katiba ni muhimu sana kwa Taifa hasa linalopiga hatua kiuchumi na kisiasa kwani kuna baadhi ya vifungu vya sheria vilivyopo kwenye katiba ya 1977 vinahitaji vifanyiwe marekebisho.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...