Skip to main content

PODIUM INC KUWANOA WAANDISHINWA HABARI




Na Mwandishi wetu HPMedia, Dar 

Katika kukuza sekta ya habari hapa nchini Kampuni ya Podium inayojihusisha na masuala ya Habari, Mawasiliano na Utafiti imeandaa mijadala ya kila mwezi ambayo inatarajiwa kuanza mwisho wa mwezi wa nane na itahusisha wanahabari hususani vijana wanaochipukia ili kuhakikisha kuwa jamii inapata taarifa kwa usahihi.

Haya yameelezwa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Podium Ezekiel Kamwaga ambapo amesema kupitia mijadala hiyo wanahabari watapewa fursa ya kujifunza jinsi ya kuripoti taarifa mbalimbali za kimataifa na kujiongezea maarifa kwa mambo ambayo hawakufundishwa vyuoni.

“Kupitia mijadala hiyo wanahabari watatuambia wao wanataka mafunzo gani pengine vyuoni hayakuwepo ila wameingia kazini wakakutana nayo, hivyo nitakuwa namleta mtu kufundisha kile ambacho wanataka kufundishwa, pia nitatoa elimu kuhusu matukio makubwa yanayotokea Duniani kama Tanzania tunakipi cha kujifunza mfano kwa sasa Mapinduzi yaliyotokea katika nchi ya Niger  kutokana na mafunzo niliyopata Uingereza kuhusu Siasa za Afrika nami niwashirikishe wengine” Amesema Bw. Kamwaga.

Aidha amesema lengo la Podium ni kusaidia watu kutoka sehemu  walipo na kuwapeleka hatua nyingine ikiwemo mashirika mbalimbali, wanahabari na watu binafsi.

Sambamba na hayo amesema mbali na mijadala hiyo pia wana gazeti la Dunia la mtandaoni ambalo linachambua habari za kisiasa kwa viwango vya kimataifa kwa lugha ya Kiswahili.

“Mimi nafahamu lugha ya kingereza na kifaransa, uchambuzi unaofanywa kwenye gazeti la Dunia ni wa viwango vya juu kuliko hata kwenye vyombo vingine vya kimataifa, mfano chambuzi anazozifanya mwandishi mkongwe Ahmed Rajab kwenye gazeti la Dunia zina ubora zaidi kuliko zile zinazoandikwa na mashirika mengine ya kimataifa na anaandika kwa viwango vya kimataifa na kwa lugha ya Kiswahili ambayo kwa sasa inawazungumzajj zaidi ya milioni 200"Ameongeza Bw. Kamwaga.

Hata hivyo ametoa wito kwa waandishi wakongwe kutambua kuwa wanawajibu wa kuwasaidia waandishi wanaochipukia na hawana bahati ya mafunzo kama walivyopata wao kutoka kwa waandishi wenye uzoefu waliokutana nao.

Katika hatua nyingine amesema ukiaji wa teknolojia ni fursa kwa waandishi wa habari kwani takribani asilimia 70 ya Watanzania ni vijana ambao taarifa nyingi wanazifuatilia mitandaoni hivyo waitumie vizuri kuhakikisha kuwa watu wote wanapata taarifa sawa wa mjini na vijijini.

Ameongeza kuwa wanahabari wanaochipukia mitandao ndio sehemu yao ya kujidai hivyo wanachopaswa kupewa ni uelewa, maarifa ili ajue jinsi ya kutoa taarifa kwa jamii ili kupunguza kiwango cha uwepo wa habari ambazo hazijaandikwa vizuri na hatarishi kwa umma.

Ametoa wito kwa wanahabari kutokata tamaa licha ya changamoto iliyojitokeza kipindi cha miaka 15 iliyopita ya kupungua kwa vyombo vya habari kwani hali sasa inarudi, kujiongeza kwa kufanya vipindi vya kibunifu na kuongeza maarifa.

Kampuni y Podium mbali na kujihusisha na masuala ya Habari pia inafanya kazi ya mahusiano na jamii, kampuni, vyama vya siasa na Asasi za kiraia toka nje ya nchi pia kufanya tafiti kwa kampuni zinazotaka kuwekeza sehemu mbalimbali hapa nchini na hazina uelewa wakutosha kuhusu njia gani au taarifa zipi ambazo watanzania wanapendelea na ambazo zitawaletea tija kwenye uwekezaji wao.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...