Skip to main content

TANZANIA KUJENGA USHIRIKIANO NA INDIA MAONYESHO YA CHAKULA



Na fatma Ally, HPMedia 

Tanzania kwa kushirikiana na India kupitia mkutano wa kimataifa wa chakula ambao unafanyika kwa mara ya kwanza barani Afrika wataweza kukabiliana na changamoto zilizopo na kuimarisha zaidi mahusiano yao na kuongeza uwekezaji kutoka India ambao utaongeza pato la taifa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa TASO Event Suveer Rajpuexlint amesema kwani India ni soko kubwa kwa nchi za Afrika hivyo Afrika wanakaribishwa kuwekeza nchini humo.

Aidha, kupitia mkutano huo utajenga ushirikiano kati ya India na nchi za Afrika kwenye maswali ya kiuchumi kibiashara na kijamii.

"Mahusiano kati ya Afrika na India yanazidi kukua hususani sekta ya kilimo kwani changamoto za wakulima Afrika zinafanana na za India hivyo lengo lao ni kukuza wakulima wadogo na kuimarisha ushirikiano kati ya Afrika na India kwenye bidhaa za kilimo"amesema.

Aidha, amesema Tanzania kwa mara ya kwanza kuwa mwenyeji wa mkutano wa kimataifa wa Chakula ambao kwa mara ya kwanza unafanyika Barani Afrika ukihusisha kampuni 500 toka nchini India na Asia katika ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam.

Amesema teknolojia pia inasaidia kutatua changamoto mbalimbali ikiwemo zile za mabadiliko ya hali ya hewa, na uhaba wa maji hivyo wakishirikuana kwa pamoja na kutatua changamoto wataweza kuzalisha bidhaa na kuilisha Afrika na Asia.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji Tanzania Pulses Network (TPN) Lirack Andrew amesema dhima ya mkutano huo ni kufungua masoko kwa mazao ya Afrika na kutoa taarifa kwa duniani nzima kuhusu uzalishaji uliopo Afrika ili nchi zenye uhitaji zifahamu na kuagiza bidhaa kutoka Afrika.

Hata hivyo, ametoa wito kwa wananchi kushiriki kwa wingi katika maonyesho hayo ambayo yatawawezesha kujenga mahusiano na kampuni za nje zitakazoshiriki kwenye maonyesho hayo na kukuza teknolojia zao na kupata fursa za masoko ya bidhaa zao.

Aidha amesema kupitia maonyesho yatakayofanyika wanatarajia kupokea watu zaidi ya 3000 ambao watatembelea mabanda ya wafanyabiashara na makampuni hivyo kujifunza mambo mbalimbali na kubadilishana uzoefu.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...