Skip to main content

ZUNGU ATOA MAJIKO YA GESI 200 KWA MAMA LISHE ILALA

 

Na fatma Ally, Matukio DaimaApp, Dar 

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mbunge wa Jimbo la Ilala Mussa Zungu amegawa majiko 200 ya gesi kwa mama lishe wa soko la Machinga Complex lililopo Ilala Ili watumie nishati mbadala waache kutumia kuni katika kupika chakula .

Akizungumza mbele ya mama lishe hao na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam amesema Rais wa Dkt Samia Suluhu Hassan anajali afya za wafanyabiashara  wa mama lishe ndio maana amewagawia majiko Ili kurahisisha mapishi waache kutumia mapishi ya kutumia moshi ni hatari katika afya .

"Tumegawa majiko ya gesi kwa mama lishe wa Ilala soko la Machinga Complex, Ilala Boma, Mchikichini na Gerezani, hii itawasaidia mama lishe kupika chakula na kupasha moto kila wakati kwa wateja wao itawavutia biashara zao "amesema Zungu .

Aidha, amewataka waondokane na kasumba kwamba chakula ukipika na gesi sio kizuri badala yake watumie gesi katika mapishi yao mapishi ya gesi hayana  moshi na chakula kinakuwa kisafi .

Amesema kuwa, mapishi ya mama lishe wakitumia gesi inaokoa pesa kwa kutumia nishati mbadala pia hawawezi kupata ugonjwa wa kifua kikuu .

Ameongeza kuwa, hewa ya ukaa inaenda angani kuharibu mazingira majiko ya gesi watu watakuwa salama bila kupata magonjwa na nazingira hayawezi kuharibika .

Kwa upande wake, Meneja wa Soko la Machinga Complex Stella Mgumia, ameipongeza Serikali kupitia Mbunge wa Jimbo la Ilala Mussa Zungu, kugawa majiko ya gesi kwa mama Lishe wa Machinga Complex .

Aidha Meneja huyo  amewataka wafanyabiashara wanaofanya biashara maeneo ambayo sio rasmi kuondoka maeneo hayo kwenda kufanya biashara zao Machinga Complex na wauza chips na mihogo waliopo pembeni mwa barabara ya Kawawa waondoke maeneo hayo .

Aliwataka wafanyabiashara kufanya biashara zao katika soko la Machinga complex kwani kuna fursa mbalimbali za kukuza uchumi .

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...