Skip to main content

KAMPUNI TANO ZA WAZAWA ZASHINDA ZABUNI UCHIMBAJI WA MAKAA YA MAWE

Na Fatma Ally,HPMedi, Dar

Katika kuhakikisha Serikali inatoa kipaumbele kwa wawekezaji wazawa imetiliana saini na kampuni tano za kitanzania ambazo zimeshinda zabuni ya uchimbaji wa makaa ya mawe eneo la Mchuchuma Wilaya ya Ludewa Mkoani Njombe.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mchimbaji na Mwekezaji wa Madini kutoka kampuni ya Cleveland Minging and Cervice Compan, Ndaisaba George Luhoro amesema kwa sasa wanaenda kuandika historia na kuongeza ajira katika pato la taifa kwa makaa ya mawe waliyokuwa wanayasikia toka wazaliwe sasa wanaenda kuyachimba.

"Kampuni yangu pamoja na makampuni mengine tulikuwa kwenye ushindani mkubwa ila kwa bahati nzuri kampuni tano ikiwemo na ya kwangu tumefanikiwa kupata mkataba huu hivyo tunaenda kuandika historia yale makaa ya mawe toka tuzaliwe tulikuwa tunayasikia sasa tunaenda kuya chimba na kuongeza ajira Kwa watanzania na kuchangia uchumi Kwa nchi yetu"amesema Mwekezaji Luhoro.

Aidha, amesema kupitia uchimbaji huo wataongeza pato la nchi kwa kulipa kodi na tozo mbalimbali hivyo anamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwaonyesha watanzania mapenzi ya dhati.

Ameongeza kuwa, kutokana na uhitaji wa makaa hayo ndani na nje ya nchi watahakikisha wanazalisha kwa kiwango kikubwa zaidi ili kuhakikisha wanafikia malengo ndani ya muda ambao umepangwa.

"Rais Dkt Samia Suluhu Hassan  amesema makaa ya mawe haya yakachimbwe na watanzania na sisi ni mashuhuda wa mapenzi yake ya dhati sasa tunaenda kuyachimba haya makaa ya mawe na kunufaisha taifa letu"ameongeza Mwekezaji Luhoro.

Hata hivyo, amesema wamepewa mda wa miezi sita kuhakikisha kuwa wanakamilisha taratibu zote na kuanzia uchimbaji wa makaa ya mawe na kuanzia kuzalisha angalau kwa mwezi mmoja wazalishe tani laki moja na nusu kwani kwa sasa yanahitajika sana Dunia hasa kipindi hiki ambacho Dunia inapambana kupata nishati.

Aidha amesema matarajio yao ni kukuza kampuni zao na kutoa ajira na kuchangia kwenye pato la taifa na kampuni zao kuzidi kukuza na kuchangamkia fursa za uchimbaji wa madini mengine hata nje ya nchi kwani mkataba huo unaenda kuwa mtaji mkubwa kwenye kampuni zao na kukuza ujuzi kwenye uchimbaji.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...