Skip to main content

WATANZANIA WATAKIWA KUFANYA MAOMBI


Na Mwandishi wetu, HPMedia, Dar

Nabii wa Taifa Dkt. Kennedy Mwasumbi kupitia huduma ya Tanzania Itubu Ministry amesema kutokana na mambo yanayoendelea kwa sasa, Tanzania hali sio nzuri, hivyo kuna haja kama taifa kufanya maombi ya kutubu.

Rai hiyo ameitoa jijini Dar es Salaam wakati alipokua akizungumza na waandishi wa habari ambapo amesema amekua akipata maono kuhusu nchi ya Tanzania, hivyo anaomba kuonana Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwenda kumueleza kwa mustakabali wa nchi.

"Nimejitokeza mbele yenu waandishinwa habari kuongea na watanzania kupitia vyombo vyenu, watanzania wanatakiwa wafanye maombi ya kutubu ili nchi iwe salama ipate utulivu, nchi yetu sio maskini lakini inahitajika kufunguliwa macho ili kuufikia utajiri uliopo,lazima tumtegemee Mungu"amesema Nabii Mwasumbi.

Hata hivyo, amesema kumekuwa na mijadala mingi kupitia makundi tofauti kutumia sheria kutafsiri mambo kupitia hiyo mijadala kuna wenye hila wanaojificha nyuma ya matukio hayo hivyo ili nchi iendelee kuwa na amani na Rais Dkt Samia atawale vizuri na makanisa yaendeshwe vizuri lazima kuchukuliwe hatua ya maombi na kutubu.

"Jambo ambalo nataka kwenda kuzungumza na linamsaada kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bunge letu, vyama vya siasa na vyombo mbalimbali hususani vya dini ikiwemo TEC na CCT na nimepata ujasiri wa kuja kuzungumza kwa sababu mwaka 1997 na mwaka 2015 Mungu amekuwa akinisemesha vituo vinavyohusiana na nchi hivyo nikipata nafasi ya kuonana na Rais nitamueleza kwa manufaa ya nchi yetu"amesema Nabii Mwasumbi.

Aidha amesema katika unabii aliotoa ni pamoja na  kusema kuwa nchi ya Tanzania sio maskini ila tatizo liko kwenye ufahamu na kufunguliwa macho kuwa wakimtegemea Mungu Tanzania ni tajiri.

"Hapa tulipofika hali ya nchi sio nzuri, tunatakiwa kumuomba Mungu ili neema itokee, unapozungumza nchi ni habari ya watanzania wote kwa ujumla ambao wanahitaji kupata mema na utulivu wa kutosha sasa kama utulivu ukikosekana hakuna kitu kizuri kinaweza kutokea na watu wakafurahi lakini mabaya yakitokea ni hatari na mbaya sana"ameongeza Nabii Mwasumbi.

Kwa upande wake Askofu wa Kanisa la Pentekoste PCCT Tegeta Dkt. Fredrick Simon amewaomba watanzania kuwa na wakati mzuri wa kumuomba Mungu na wanatarajia kuwa Dodoma kuanzia tarehe 27 hadi 30 mwezi mwezi wa 9/2023 kwa ajili ya kuliombea Taifa.

Amesema kuwa, taifa linahitaji maombi na bila msaada wa Mungu haliwezi kusogea na kufika mbali hivyo watanzania wajitokeza kwa wingi Dodoma katika ukumbi wa African Dreams Conference Center ambapo maombi ya kuliombea Taifa yatafanyika.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...