Skip to main content

IET NOV 30 KUANZA KONGAMANO

Na Mwandishi wetu, Dar 

Taasisi ya Wahandisi Tanzania (IET) inatarajia kufanya kongamano kubwa la 32 ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa .

 Aidha, IET inawakaribisha wahandisi na wadau wote wa sekta mbalimbali za uchumi nchini kwenda kushiriki kwenye kongamano hilo muhimu ambalo litahudhuriwa na washiriki zaid ya 1000.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Rais wa Taasisi hiyo, Eng Mgema Mudo amesema kuwa, kongamano hilo litafanyika tareh 30 mwezi wa 11 hadi tarehe 2 mwezi wa 12 mwaka 2023 katika ukumbi wa kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha .

Aidha amesema kuwa, miongoni mwa watu watakaoshiriki ni mafundi, wahandisi, wanafunzi na wadau wengine kutoka mikoa mbalimbali nchini na nje ya nchi watashiriki kongamano hilo muhimu ambapo wengine watashiriki kwa njia ya mitandao.

Aidha, amesema kuwa miongoni mwa mada zitajazojadiliwa ni pamoja na kutoa elimu ya ubunifu na zinalenga kuhimiza na kuchochea ari ya kuondoa  dhana ya ufanyaji kazi kwa mazoea na kusisitiza kuzingatia ubunifu, umakini, ufanisi na weledi pamoja na uwajibikaji.

"Tunapaswa kufahamu kuwa utekelezaji wa mikakati mbalimbali ya maendeleo unahitaji sio tu kukuza ujuzi na maarifa katika uhandisi bali pia kukuza kiwango na uwezo wa ubunifu  wa kisayansi na teknolojia na ujuzi nyengine karne ya 21, zikiwemo nidhamu, umakini, ufanisi, uwezo, juhudi na weledi"amesema Eng Mgema.

Hata hivyo, amesema katika kila nyanja Ili kuboresha au kuibua suluhu mpya katika utekelezaji wa kazi mbalimbali za kihandisi ambpo hiyo itafungua njia katika safari ya kufikia maendeleo endelevu na kuifanya Tanzania kuwa mshindi katika ngazi za kikanda na kimataifa.


Aidha, amesema kuwa, taasisi hiyo ina malengo ya kufungua matawi katika mikoa yote nchini ili kuongeza wigo na ushiriki wa wahandisi katika katika kutekeleza dira na dhamira ya taasisi hiyo.


Kwa upande wake, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji IET Eng Upendo Haule amewataka wahandisi wazama kujitokeza kwa wingi kushindania zabuni zinapotangazwa ili kuweza kufanya kazi kwa uadilifu na kuonesha uwezo wao.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...