Skip to main content

KILO 3,182, ZAKAMATWA DAR NA IRINGA,DCEA YAFUNGUKA

Na Mwandishi wetu, Dar

Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa Tanzania (DCEA) imekamata jumla ya kilogram 3,182 za dawa za kulevya aina ya Heroin na Methamphetamine katika oparesheni maalum iliyofanyika jijini Dar es Salaam na Mkoani Iringa kati ya tarehe 5 hadi 23 mwezi Dicemba mwaka 2023.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, mapema leo hii Kamishna Jeneral wa DCEA Aretas Lyimo amesema kuwa katika oparesheni hiyo jumala ya watu saba wamekamatwa kuhusika na dawa hizo ambapo wawili kati yao wana asili ya Asia.

Amesema kuwa, kiasi hicho cha dawa za kulevya hakijawai kukamatwa katika historia ya Tanzania tangu kuanza kwa shughuli za udhibiti wa dawa za kulevya, hivyo watuhumiwa waliokamatwa ni miongoni mwa mitandao mikubwa ya wauzaji wa dawa za kulevya inayofuatiliwa nchini na duniani.

"Kiasi hiki cha dawa za kulevya kinajumuisha kilogramu 2,180,29 za dawa aina ya methamphetamine na kilogramu 1001.71 aina ya heroin zilizokamatwa katika Wilaya 

za Kigamboni, Ubungo na Kinondoni jijini Dar es Salaam pamoja na Wilaya ya Iringa mkoani Iringa"amesema Kamishna Lyimo.

Aidha, dawa hizo zilizokamatwa zilikuwa zimefungashwa kwenye vifungashio vyenye chapa mbalimbali za kahawa na majani ya chai ambapo mbinu hiyo inatumika kwa lengo la usafirishaji wake kukwepa kubainika.

Hata hivyo, amesema kuwa dawa aina ya methamphetamine ni dawa mpya ya kulevya iliyopo katika kundi la vichangamshi sawa cocaine ambapo dawa hiyo huwa kwenye mfumo wa vidonge, unga au chembechembe mithili ya chunvi ang'avu yenye rangi mbalimbali ambayo huzalishwa kwenye maabara bubu kwa kuchanganya aina mbalimbali za kemikali bashirifu.

"Dawa hii ni hatari kwa afya ya mtumiaji madhara yake ni makubwa na hayatibiki kirahisi kwani mtumiaji hupata madhara ya kudumu kwenye ubongo na hivyo hupunguza uwezo wa kutunza kumbukumbu na kusababisha uraibu na kuathiri mfumo mzima wa fahamu.

Ameongeza kuwa, kiasi cha dawa za kulevya zilizokamatwa zingefanikiwa kuingia mtaani zingeweza kuathiri zaid ya watu 76, 368,000 kwa siku hivyo, ukamataji huo umeokoa nguvu kazi ambayo ingeangamia kutokana na madhara yatokanayo na madawa ya kulevya ndani na nje ya nchi.

Sambamba na hayo DCEA imetoa onyo kwa wote wanaoendelea kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya nchini Tanzania, huku ikiwataka wajikite kwenye biashara nyengine halali kwani mamlaka imejidhatiti kukomesha biashara hiyo kwa kufanya oparesheni katika maeneo mbalimbali nchin.

Aidha, DCEA imeishukuru Serikali ya Jamuhuri ya muunganobwa Tanzania inayoongozwa na Rais Samia Suluh Hassa kwa kuendelea kuiwezesha mamlaka hiyo katika kutekeleza kazi zake kwa ufanisi mkubwa.



Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...