Skip to main content

PURA NA ZPRA WAJADILI NAMNA YA KUENDESHA SEKTA YA MAFUTA NA GESI ASILIA

 

Na fatma Ally, Matukio DaimaApp, Dar 

Mamlaka ya udhibiti mkondo wa juu wa Mafuta na gesi asilia PURA  na Mamlaka ya udhibiti wa utafutaji na uchimbaji wa mafuta na Gesi asilia Zanzibar (ZPRA) leo wamekutana jijini Dar es Salaam kwa lengo la  kuzishauri Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanziba jinsi gani ya kuendesha sekta za gesi na mafuta hapa nchini.

Akizungumza jijini Dar es Salaam na waandishi wa habari Mwenyekiti wa Bodi ya PURA, Khalfan Khalfan amesema kuwa baada ya kumaliza kikao hicho ni mashirikiano makubwa kati ya ZPRA na PURA.

Aidha, amesema kikao hicho kinategemea kutengeneza  fursa ya kunadi maeneo wazi (Vitalu) ambayo ni moja ya sera ya Serikali ya kutangaza uwekezaji.

Amesema kuwa, baada ya kikao hicho watakua na msimamo wa pamoja ni kwa jisni gani sekta ya mafuta itapata wawekezaji katika pande zote bara na visiwani.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Udhibiti mkondo wa juu wa Petrol (PURA) Mhandisi Charles Sangweni amesema kuwa leo wamekutana wakurugenzi wa bodi mbili kati ya Pura Zpra ambapo wamekuwa na mahusiano hayo kwa muda mrefu ambapo wameamua kuingia kwenye makubaliano kati yao Feb 19 mwaka 2022 hivyo waliunda timu ya pamoja.

Aidha, amesema kuwa, wao kama watendaji wamekuwa na mahusiano ya muda mrefu ya pande zote mbili ambapo kikao hicho kinalenga kubadilishana uzoefu wa kiutendaji sambamba na kuelekezana kwa yale ambayo upande mmoja hayajui katika utafitaji wa mafuta na gesi asilia.

Hata hivyo, amesema kikao ahiko pia kinalenga kutoa taarifa ambazo zimekuwa zikichukuliwa katika ardhi ya Tanzania, hivyo wameona ni vyema kushirikisha watendaji wa bodi kwani bodi ndio inayokuwa ikiwapa maelekezo ya kiutendaji na kuyatekeleza kiutendaji.

"Moja ya mambo ambayo tunakwenda kutekeleza pande zote mbili ni vitalu, baadae izae mikataba ya utafutaji wa mafuta na gesi, hivyo tumegundua wenzetu wa ZPRA na sisi tunaenda pamoja ndio maana tukaona tushirikiane ili kuleta hamasa na gharama za kutekeleza jambo hili na hii nchi ni moja na faida itakayopatikana ni kwa pande zote mbili"amesema Mhandisi Sangweni.

Naye, Mkurugenzi Mwendeshaji ZPRA,  Adam Abdulla Makame amesema kuwa Taasisi hiyo imekua na majukumu sawa na PURA  ambapo kazi kubwa ni kusimamia sekta ya mafuta na gesi katika mkondo wa juu ili kuhakikisha Tanzania  inanufaika na sekta ya nishati na gesi asilia.

"leo tumekutana hapa ikiwa ni kikao chetu cha kwanza cha bodi zetu mbili ikiwa ni ZPRA na PURA ili kuweza kujadiliana kwa pamoja ni jansi gani tutaweza kufanya kazi kwa pamoja kufungua maeneo yetu na kufanya kazi kwa pamoja katika utafutaji wa mafuta na gesi asilia"amesema  Makame.

Aidha, amesema kuwa katika historia inaonesha kuwa suala la kunadi vitalu ama kuvutia wawekezaji lilifanywa kwa miaka 10 iliyopita ambapo tangu mwaka 2013 hawakuendelea tena na zoezi hilo, hivyo kupitia kikao hicho watapata makubaliano ya pamoja kwa Tanzania bara na Visiwani na kuwa na mkakati wa pamoja ambapo ni kwa namna gani wataweza kuvitangaza vitalu hivyo.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...