Skip to main content

WAMILIKI WA MALORI WATAKIWA WAWAJALI MADEREVA WAO

Na mwandishi wetu, Dar

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wamiliki wa malori nchini wawajali madereva na wahudumu wa magari hayo ikiwa ni pamoja na kuboresha maslahi yao.

Amesema uanzishwaji wa kanzidata ya taarifa za madereva utawawezesha wamiliki hao kutumia taarifa hizo kwa lengo la kusimamia usalama wa madereva pamoja na kufuatilia mienendo na ufanisi wao.

“Katika hili, niwasisitize kuhusu kuzingatia usalama na maslahi ya madereva wenu ambao kimsingi ni walinzi wa mitaji yenu kupitia vyombo ambavyo mmewapa dhamana ya kuviendesha. Haki iende na wajibu, yaani mnataka wawatumikie, kwa hiyo na ninyi mboreshe maslahi yao,” amesisitiza.

Ametoa wito huo wakati akizungumza na wadau wa sekta ya usafirishaji waliohudhuria uzinduzi wa kanzidata ya madereva wa malori nchini leo (Alhamisi, Desemba 14, 2023) jijini Dar es Salaam. Kanzidata hiyo imeandaliwa na Chama cha Wamiliki wa Malori Tanzania (TATOA).

Akizungumza na wadau wa sekta hiyo, Waziri Mkuu amesema azma ya Serikali ya awamu ya sita ni kuendeleza sekta hiyo ili iweze kuharakisha ukuaji wa uchumi. “Hatua iliyofikiwa leo ni kuhakikisha makao makuu ya mikoa yote inafikika kwa lami na shoroba zote za Kusini, Kati na Kaskazini kuelekea nchi za jirani za Kenya, Kongo, Malawi na Zambia zinapitika bila shida.”

Akielezea maboresho ya sekta hiyo, Waziri Mkuu amesema Serikali tayari imekamilisha ujenzi wa barabara za lami zenye urefu wa km. 2,183.82 na km. 14,348 za changarawe. Licha ya hayo imekuwa ikiendelea na matengenezo ya kawaida ili kuzifanya barabara zetu ziweze kupitika wakati wote.

Sambamba na maboresho hayo ya barabara, Waziri Mku amesema Serikali inaendelea na ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kimataifa (SGR) unaoambatana na uundaji wa vichwa 17 vya treni, uboreshaji wa bandari za Dar es Salaam, Mtwara, Tanga na kwenye maziwa makuu ya Victoria, Tanganyika na Nyasa ambapo muda wa kugomboa mizigo bandarini umepungua kutoka siku 14 hadi siku sita.

“Uimarishwaji wa sekta hizi haulengi kuua usafirishaji wa malori kwani ujenzi upanuzi wa bandari zetu, utaleta mizigo mingi zaidi na kazi ya usafirishaji itafanywa na ninyi,” amesema.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu alipokea hundi kutoka kwa wanachama wa TATOA wenye thamani ya sh. milioni 100 ikiwa ni mchango wao kwa waathirika wa maafa ya mafuriko huko Katesh, wilayani Hanang, mkoani Manyara.

Akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na washiriki wa hafla hiyo, Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile, aliwapongeza viongozi wa TATOA kwa ubunifu wao mkubwa wa kuamua kuandaa kanzidata hiyo.

Alisema Serikali inao mfumo wa kusajili madereva ulioko chini ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) ambao umeshasajili madereva 19,709 wakiwemo wa mabasi na malori. “Kanzidata hii itatumiwa pia na Serikali kufuatiulia mwenendo wa madereva wa malori,” alisema.

Naye Mwenyekiti wa TATOA, Elias Lukumay alisema kuundwa kwa kanzidata hiyo kutasaidia mambo mengi kwani kitakuwa ni chombo chenye nguvu kwa vile kitakuwa na taarifa zaidi ya majina na leseni zao.


“Chombo hiki kitatoa taarifa baina ya madereva na wamiliki wa malori, pia kitaondoa changamoto wa watu wasio waaminifu na kitakuwa alama ya usalama kati ya dereva, mmiliki wa lori na mteja,” alisema.


Awali, Mwakilishi wa Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Bw. Louis Manzombi Kisombo alisema suala la mawasiliano ni pana sana na akaomba suala la kuunda Kamati ya Pamoja ya kufuatilia malalamiko ya madereva lifanyiwe kazi mapema ifikapo Januari, 2024.


Alisema Kamati hiyo itakayokuwa na jukumu la kupokea malalamiko ya pande zote, itapaswa kuwa inakutana walau kila baada ya miezi mitatu na kwamba ubalozi wao uko tayari kutoa ushirikiano kwa Kamati hiyo.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...