Skip to main content

TANZANIA YAPOKEA MELI KUBWA YA WATALII, MABORESHO YA BANDARI YAZAA MATUNDA


Na Mwandishi wetu, Dar

Tanzania kupitia Mamlaka ya Bandari TPA imeweka historia kwa kupokea meli kubwa ya watalii ikitokea nchini Norway inayomilikiwa na kampuni ya Norwegian Cruiseline Holdings ya Marekani, yenye urefu wa mita 294 ambapo meli hiyo ni ya kwanza kutia nanga katika bandari ya Dar es Salaam tangu nchi hiyo ilipopata uhuru mwaka 1964.

Hatua hiyo imekuja mara baada ya maboresho makubwa yanayoendelea kufanyika katika bandari ya Dar es Salaam kupitia mradi wa maboresho ya bandari ya Dar es Salaam (DMGP) ambayo yamechagia ujio wa meli hiyo, hali  itakayopelekea kuongezeka kwa watalii nchini humo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mara baada ya kupokea meli hiyo iliotia nanga majira ya saa 11 alfajiri mapema leo hii, Mkurugenzi Mkuu wa Bandari hiyo, Mrisho Mrisho amesema kuwa,malengo ya bandari hiyo ni kuhudumia meli zenye urefu wa mita 305 hadi 350. 

Amesema kuwa, meli hiyo ina uwezo wa kubeba abiria 4700 lakini kwa Tanzania wamekuja wageni zaidi ya  2000 ambapo wageni 1100 walishuka katika bandari ya Zanzibar na kuelekea katika vivutio mbalimbali vikiwemo Ngorongoro na Serengeti kupitia ndege za kukodi na hatimaye wataungana na abiria wenzao katika bandari ya Dar es Salaam na kuendelea na safari. 

"Ujio wa meli hii kubwa katika bandari yetu yenye uwezo wa kubeba abiria 4,700 kutafungua milango kwa wadau wengine wenye meli kubwa zaidi duniani kutia nanga kwenye bandari hii,tukumbuka haya ni matunda ya Royal Tour Rais Dkt Samia ametufungulia milango ya kuongeza watalii nchini kupitia filamu yake"amesema Mrisho

Hata hivyo, wageni zaidi ya 300 wameshuka katika bandari ya Dar es Salaam na kufanya matembezi katikati ya jiji la Dar es Salaam (City Tour) kupitia wakala wa utalii. 

Kwa upande wake, Nahodha Mkuu wa Mamlaka ya Bandari TPA, Abdula Yussuf Mwingamno amesema kuwa ujio wa meli hiyo ni jambo la kujivunia sana kwani maboresho yanayoendelea katika bandari hiyo ndio yanatoa fursa kupokea meli zenye urefu mkubwa zaidi kuwahi kutia nanga katika bandari hiyo.

"Meli kubwa mara nyingi sana tumekua tukizipokea mchana lakini kwa maboresho tulioyafanya katika bandari yetu, meli hii imeweza kutia nanga saa 11 alfajiri bila matatizo yoyote na captain wao wameisifia sana bandari yetu katika bandari zote walizopita"amesema Nahodha Mwangamno.

Amesema kuwa, Kwa kushirikiana na waongozaji wa meli nchini wameweza kuweka mazingira wezeshi ya kupokea bidhaa kutoka kwenye meli na rasiliamali za watu hivyo Bandari ya Dar es Salaam, Mtwara na Tanga kutakua na ushindani wa kibiashara.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...