Skip to main content

WANAOPANDISHA BEI YA SUKARI KIHOLELA KUKIONA


Na Mwandishi wetu, Dar

KATIKA kukabiliana na uhaba wa sukari nchini Tanzania Serikali imetoa kibali cha kuagiza sukari nje ya nchi tani 50,000 ambapo inatarajiwa kuingia Januari 22, mwaka huu pamoja na kuvifungulia viwanda vyote vinavyozalisha sukari  ili kukidhi mahitaji ya wananchi.

Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi mkuu wa Bodi ya Sukari Tanzania Prof Kenneth Bengesi wakati alipokua akizungumza na waandishi wa habari ambapo amesema sukari iliyopo nchini kwa sasa haikidhi mahitaji ya wananchi, hivyo Serikali imejipanga kuchukua hatua ili kukabiliana na changamoto hiyo.

Amesema kuwa, miongoni mwa sababu zilizopelekea kuwepo kwa changamoto hiyo ni pamoja na mvua za El-nino ambazo zimenyesha mwezi Novemba na Disemba mwaka 2023 ambapo zimesababisha mashamba ya miwa kujaa maji na miundombinu hivyo kupelekea uzalishaji mdogo wa miwa.

Katika hatua nyengine Bodi ya Sukari Tanzania imewataka wafanyabiashara wanaouza sukari kuacha tabia ya kujipangia bei hali  inayopelekea kuwaumiza wananchi kwani bei ya sukari kwa sasa wanauza hadi shill 6000 kutoka 3000 bei ya kawaida.

"Tumeshangazwa na taarifa tunazozisikia kuwa huko mtaani bei ya sukari imepanda sana, hakuna bei mpya ambayo imetoka wananunua kwa bei ile ile, sijui kwa nini wanapandisha, Serikali inafanya kila jitihada kuhakikisha inatatua tatizo hili, hawa wanaojipangia bei tutawashughulikia kwa mujibu wa sheria"amesema Prof Kenneth.

Ameongeza kuwa, "Bodi inatambua kuwa kila mkoa unatofautiana bei ya sukari hivyo wafanyabiashara wanaopandisha bei kwa maslahi yao binafsi tofafauti na bei halali ya mkoa huo tukiwabaini hatutawaacha tutahakikisha tunawachukulia hatua kali za kisheria kwani hatupendi kuona wananchi wakilalamika juu ya bidhaa hii muhimu kupandishiwa bei holela” amesisitiza mkurugenzi.

"Mwaka 2023 tumezalisha tani 345,000 pekee ambazo hazitoshelezi lakini kawaida mahitaji huwa ni tani 520,000 na katika uzalishaji tunapenda malengo yetu ni kuzalisha tani laki tano na hamsini na tano ili tuwe na akiba ya sukari ya kutosha lakini kutokana Msimu huu wa mvua za El nino tumeshindwa kufikia lengo ndiyo maaana tuna uhaba wa sukari"amesema Bengesi.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...