Skip to main content

BABU OWINO ATOA RAI KWA VIJANA WA ACT WAZALENDO, NONDO NAE YUPO


Na Mwandishi wetu, Habari Plus Dar

MBUNGE wa Jimbo la Embakasi Mashariki Nairobi, Kenya Poul Owino amewataka vijana nchini Tanzania kupigania kupata haki zao katika kulitetea taifa lao pamoja na kuwa viongozi bora kwa maslah mapana ya Taifa.

Rai hiyo ameitoa jijini Dar es Salaam mapema leo wakati alipokua akifungua kongamano la Ngome ya Vijana lililokwenda sambamba na uchaguzi wa viongozi mbalimbali ikiwemo nafasi ya Mwenyekiti, Makamo Mwenyekiti, Katibu, pamoja nafasi nyengine mbalimbali.

Amesema kuwa, Chama cha ACT Wazalendo ni cha kuigwa kutokana na kuwa chama bora chenye mfumo imara wa kupigania haki na kuwalea vijana ambao wana uwezo wa kukipigania kwa  maslahi ya Taifa kwa ujumla.

"Vijana ni Taifa la leo sio la kesho, mapambano yanatakiwa kuanza leo,  hivyo usikuabali kukaa kimya kwani usipokubali kuwa kwenye meza ukala utakua menu uliwe, vunja hiyo meza usipokua sehemu yao, Hayyat Mwalim Julias Nyerere, Kawawa na Kwame Nkuruma wangekua waoga unadhani uhuru ungepatikana? "amehoji Dkt Babu Owino.

Akitoa nasaha za Chama cha ACT Wazalendo, Katibu Mkuu Ado Shaibu amewataka wajumbe wa mkutano huo kuchagua viongozi ambao wataweza kuwaongoza wananchi, kukitetea na kukijenga Chama hicho kwani hilo ndio lengo la chama namba moja katika kuanzisha taasisi ndani ya chama.

Aidha, amesema kuwa, Chama hicho kinawategemea sana vijana kwani wamekua wakiwalea kwenye misingi iliyoimara ya uongozi na kimewaamini ndio maana hawategemei wanachama ambao wanatoka kwenye vyama vyengine kwenda kujinga kwao bali wanachagua viongozi waliowalea wenyewe.

"Kwa miaka minne mfululizo Chama chetu kimeachana na tabia ya kusubiri wanachama waliohama vyama vyao ili kuja kuwapa uongozi bali tunachagua viongozi ndani ya chama kwani wamewalea vizuri, na tunawaamini katika kusimamia katiba hivyo lazima mchague watu ambao wataweza kuwasimia vizuri katika kutatua changamoto za wananchi" amesema  KM Ado.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana Taifa, Abdul Nondo amewataka vijana kuwa tayari katika kukipigania chama na kutokuwa waoga, kwani Hayyat Mwalim Nyerere angekua muoga taifa la Tanzania lisingepata uhuru ili kuwa viongozi bora ni lazima ujitoe kwa taifa lako na kuwatumikia wananchi waliokuamini na kukuchagua.

Aidha, amesema kuwa, asilimia 75 ya watanzania ni vijana hivyo wanatakiwa kusimama imara kushiriki nafadi mbalimbali za uongozi si tu kujenga Chama bali hata kupigania maslahi ya wananchi kwani changamoto nyingi zinapotokea zinawakumba vijana.

Miongoni mwa wageni walioalikwa katika mkutano huo ni pamoja Katibu wa Cha Juvicuf ambapo amesema vijana wanahitaji kuwa na sauti ya pamoja ili kuhakikisha wananchi wanatetewa kwenye changamoto zao.







Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...