Skip to main content

NHIF YAFANYA MABORESHO YA KITITA CHA HUDUMA ZA MATIBABU, YAENDELEA KUPOKEA MAONI


Na Mwandishi wetu, Habari Plus, Dar

Mfuko wa Bima wa Taifa wa NHIF imefanya maboresho ya kitita cha mafao kwa wanachama wake ambayo utekelezaji wake utaanza rasmi Machi Mosi mwaka 2024 ikwa lengo ni upatikanaji wa huduma bora wa wanachama pamoja na kuongeza huduma ambazo hazikuepo hapo awali.

Akizungumza na waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Dkt Bernad Konga amesema maboresho ya mwisho ya kiticha cha mafao ya mfuko huo kichotumika sasa yalifanyika June 2016 sawa na takribani miaka 8 iliyopita na hivyo upo umuhimu wa kufanya marejeo yake kutokana na sababu mbalimbali.

Aidha, amesema kuwa,  maboresho hayo ya orodha ya huduma za matibabu ambazo zinatolewa kwa wanufaika wa NHIF na bei zake ambazo hutumika wakati wa malipo kwa madai ya watoa huduma za matibabu yamezingatia maendeleo ya teknolojia na hali halisi ya bei katika soko pia kuwianisha kitita cha mafao na miongozo ya tiba iliyoboreshwa Ili kuongeza ubora wa huduma zinazotolewa Kwa wanufaika wa mfuko.

Sambamba na hayo, amefafanua kuwa maeneo yaliofanyiwa mapitio na maboresho ya kitita cha mafao ni pamoja na ada ya usajili na kupata ushauri wa daktari, huduma za dawa, vipimo, upasuaji na gharama za kliniki za kawaida na kibingwa.

"Kuhusu Huduma za dawa jumla ya dawa ya 736 zimefanyiwa mapitio kwa kuzingatia bei ya soko na gharama za uendeshaji na wastani wa faida ,hii itaondoa changamoto ya wananchi kukosa baadhi ya huduma za dawa kutokana na changamoto ya bei, pia tumeongeza dawa mpya 247 ambazo zinatokana na dawa mpya zilizopo kwenye muongozo wa orodha wa dawa muhimu za Taifa (NEMLIT)" amesema Dkt Konga

Ameongeza "Gharama za vipimo 311 na upasuaji zimefanyiwa mapitio kwa kuzingatia bei za soko katika ununuzi wa vifaa na vitendanishi, gharama za uendeshaji na wastani wa faida hii itaondoa changamoto ya kukosekana Huduma za vipimo na upasuaji kutokana na changamoto ya bei"

Hata hivyo, amewaomba wananchi kuendelea kujiunga kutumia na mfuko huo kwani lengo la Serikali ni kutoa huduma za Afya kuanzia ngazi ya Zahanati, hadi Hospital ngazi ya Taifa.

Aidha, amesema mfuko huo utaendelea kupokea maoni kutoka kwa wadau na itaendelea kuwajulisha pindi maboresho yoyote yatakapotokea Ili kuwa na ufanisi katika utoaji wa huduma huku akiwataka wanachama na watoa huduma watakao pata changamoto wakati wa kutoa huduma kuwasiliana na mfuko huo kupitia kituo cha huduma Kwa wateja 199 bure.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...