Skip to main content

TREN YA MWENDOKASI YAANZA MAJARIBIO DAR - MOR0


Na Mwandishi wetu, HabariPlus,Dar

Shirika la Reli Tanzania (TRC) leo limeanza safari ya kwanza ya majaribio kwa Treni ya umeme ya Abiria (SGR)  kutoka ofisi zake zilizopo jengo la Tinzanite maeneo ya stetion Jijini Dar es salaam kuelekea Mkoani Morogoro.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini humo mapema leo hii Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo Masanja kadogosa amesema Usafiri huo wa Treni utatumia umeme wa kawaida kutoka TANESCO na wanatarajia kuanza safari za abiria hivi karibuni.

Aidha amewatoa wasiwasi watanzania wanaodhania kuwa umeme ukikatika utaweza kuleta athari kwa Treni hizo kuwa sio kweli umeme wake umeunganishwa kutoka grid ya taifa hivyo si rahisi umeme kukatika kwenye njia ya Treni.

Ameongeza kuwa,katika majaribio hayo walimeambatana pamoja na msemaji wa Serikali, wasanii, waandishi wa habari, wahariri na baadhi ya wafanyakazi wa TRC, ambapo treni hiyo inauwezo wa kutembea Km/h100-160.

Kwa upande wake, Msamaji Mkuu wa Serikali Mohbare Matinyi amesema kuwa, ujio wa treni hiyo ya mwendokasi utakua fursa kwa wananchi ambapo watu wa morogoro na kupeleka Dar es Salaam ambapo zoezi hilo litafanyika kwa mikoa yote ambayo itapitiwa na mradi huo.

"Leo tumeweza kuanza hatua ya majaribio kwa treni yetu ya abiria kutoka Dar es Salaam mpaka Morogoro, miezi michache ijayo treni hii itaanza safari zake hadi kufika Dodoma ni jambo la kupongeza kwa Serikali yetu, hii inatoa fursa za kiuchumi wananchi wetu wanatakiwa wafanye biashara na mrandi huu utakapokamilika tutaweza kufanya biashara na nchi jirani"

Ameongeza kuwa "Tren ni usafiri wa usalama na uhakika na wa bei nafuu, hapa biashara zitafanyika wananchi watafaika kwa kazi nzuri iliyofanywa na Serikali kwa mfano Mkoa wa Dar es Salaam sio wakulima kwa iyo watachukua mazao kutoka Morogoro, Morogoro wataletewa bidhaa za kiwandani kutoka Dar es Salaam ambapo zoezi hilo litafanyika pia na kwa mikoa mengine mradi ukikamilika"amesema Martin.

Imeondoka saa 10:30 asubuhi katika ofisi zake za Tanzanite jijini Dar es Salaam na kufika Morogoro na 12:47 ambapo imefanya tena safari ya kurudi Dar kutoka Morogoro 1:47 .

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...