Skip to main content

KAMATI YA BUNGE YAKAGUA UJENZI WA JENGO LA WIZARA YA NISHATI MTUMBA

 Yapongeza Wizara kushirikisha Taasisi za Umma kwenye ujenzi

Yataka mkandarasi kuongeza kasi ya ujenzi

 Ujenzi wafikia asilimia 75

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeipongeza Wizara ya Nishati kwa kushirikisha Taasisi  za Umma katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa jengo la Wizara katika Mji wa Serikali-Mtumba na hivyo kuziimarisha Taasisi hizo katika utoaji wa huduma.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Kilumbe Ng’enda ametoa pongezi hizo wakati Wajumbe wa Kamati hiyo walipokagua ujenzi wa Jengo la Wizara ya Nishati katika Mji wa Serikali, Mtumba jijini Dodoma tarehe 12 Machi, 2024.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto  Biteko, Naibu wake, Mhe. Judith Kapinga, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba pamoja na Menejimenti ya Wizara ya Nishati walishiriki katika ukaguzi wa jengo hilo.

“Baada ya kufika hapa tumeona kuwa mkandarasi wa mradi huu ni Shirika la Nyumba la Taifa (NHC)  na Mshauri Elekezi  ni kampuni ya ABECC ambayo ipo chini ya Chuo Kikuu Ardhi, Kamati inawapongeza kwa hatua hii ya kuzishirikisha Taasisi hizi za umma kwani pesa inayotolewa hapa na Wizara inarudi kuiimarisha mihimili mingine ya Serikali.” Amesema Mhe. Ng’enda

Aidha, Mhe. Ng’enda amezitaka Taasisi hizo zifanye kazi kwa kasi, weledi na kwa wakati ili kuwawezesha watumishi kuanza kutumia jengo hilo kutoa huduma kwa wananchi.

“ Kwa kuwa mkandarasi umethibitisha kuwa fedha ya kutekeleza kazi hii unayo na unalipwa kwa wakati, hakikisha mnafanya kazi usiku na mchana na mhakikishe kuwa mafundi na vibarua wanalipwa pesa zao kwa wakati ili kuleta ufanisi kwenye kazi.” Amesema Mhe. Ng’enda

Vilevile, amemtaka mkandarasi kuhakikisha  vifaa vyote vinavyohitajika kwenye kazi ya umaliziaji wa jengo hilo vinapatikana kwa wakati ili kutochelewesha kazi nzuri ambayo imefanyika hadi sasa.

Awali, Msimamizi Kazi za Ujenzi wa Jengo la Wizara ya Nishati, Alphonce Kilovere alisema kuwa  mradi huo umefikia asilimia 75 ambapo gharama ya mradi ni shilingi bilioni 25.2.

Aidha ameeleza kuwa, kazi ujenzi wa jengo hilo inatarajiwa kukamilika mwezi Mei mwaka huu.



Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...