Skip to main content

MAMA ONGEA NA MWANAO KUFANYA TAMASHA KUBWA, MIAKA 3 YA RAIS SAMIA NEEMA TUPU

Na Mwandishi wetu, HabarPlus, Dar

TASISI ya Mama Ongea na Mwanao inatarajia kufanya Tamasha kubwa la walemavu ambalo limelenga kuwasilikiza changamoto zao na kuwapatia mahitaji yao muhimu ikiwa ni mwendelezo wa kampeni hiyo kuunga mkono jitihada za Rais Dkt Samia Suluh Hassan.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Taadisi hiyo, Steven Nyerere amesema kuwa tamasha hilo litafanyika nchi nzima ambapo wataungana na watu wa makundi mbalimbali ikiwemo vijana, mabodaboda, wajasiri amali ambapo kauli mbiu yake "Mtonye Mwenzako Mama Tena".

Amesema kuwa, moja ya mikakati ya taasisi hiyo ni kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ambapo wamekua wakisaidia watu wenye mahitaji maalum ikiwemo kugawa viatu kwa wanafunzi mashuleni.

"Katika miaka mitatu ya Rais Dkt Samia amefanya kazi kwa vitendo katika kuwahudumia wananchi ikiwemo umeme, sisi kama Taasisi tunawaahidi tutaendelea kuwashika mkondo nyinyi ni wapiga kura nchi hii, nyinyi ni watu kama watu wengine na mnahaki sawa na wengine".

Aidha, amesema Rais  Samia amekuwa akijikita katika kusaidia watanzania wa hali ya chini katika kipindi cha miaka mitatu yake ya uongozi anastahili kupongezwa, ameona tatizo la umeme na kulitafutia ufumbuzi na kujenga bwawa la mwalimu nyerere ambalo likianza kutoa huduma tutauza umeme mpaka nje ya Tanzania".

Hata hivyo, amesema pia kwenye sekta ya michezo Tanzania inafanya vizuri imeacha kuwa mtazamaji na mshiriki bali sasa imekuwa mshindani mkubwa na hata kushinda kwenye majukwaa makubwa ambapo wanamichezo wa sarakasi Ramadhani brothers na wengi wengi.

"Na sisi kutokana na jitihada za mama anazozifanya katika kuketa maendeleo katika taifa hili tukajitwika jukumu la kuwavika viatu watoto wa shule ambao hawana uwezo sasa hivi tumebakisha mikoa 13 kukamilisha mikoa yote Tanzania.

Aidha Steve Nyerere amekemea wanaharajati wanaotumia Mitandao ya kijamii kutukana viongozi wa juu Serikalini na kubeza jitihada zao na kuwasisitiza kuwa watumie hoja kupinga na si kutumia matusi katika kukosoa kwao.

Kwa upande wake, Susan Lewis maarufu kama Mama Natasha amesema Taasisi ya Mama ongea na Mwanao inasimamia wasanii mbalimbali ambao wanalenga kutumia Taasisi hiyo kusaidia jamii katika nyanja mbalimbali ikiwemo kusaidia vifaa vya shule vua watoto na kadhalika.

Nae, Katibu wa Jumuiya ya watu wenye ulemavu ameipongeza Taasisi hiyo kwa kuwashurikisha mara kwa mara watu wenye ulemavu katika shughuli zake mbalimbali ikiwemo makongamano, mikutano na warsha ikiwa ni pamoja na kuwapa misaada watu wenye ulemavu.

"Wanayotafanya mama ongea na mwanao ni kumuunga mkono Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu katika adhima yake ya kuwainua watu wasiojiweza, wenye ulemavu,wajasiliamali".

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...