Skip to main content

SERIKALI YASITISHA UMEZESHAJI WA KINGA TIBA

 


Na Mwandishi wetu, Habari Plus, Dar

Serikali kupitia Wizara ya Afya imesitisha kampeni za umezeshaji wa kingatiba ya ugonjwa wa Matende na Mabusha katika maeneo ya Mkoa wa Dar es Salaam kutokana na kufanikiwa kuthibiti magonjwa hayo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Waziri wa Afya Ummy Mwalimu ambapo amesema maeneo waliositisha ni pamoja na Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni, Ubungo, Temeke na Halmashauri ya Jiji la Dar Es Salaam pamoja na kata 10 za Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni baada ya kujiridhisha kutokuwa na maambukizi mapya ya ugonjwa wa Mabusha na Matende katika maeneo hayo.

Aidha amesema kuwa Serikali kwa kushirikiana na wadau hadi sasa imeweza kudhibiti Ugonjwa wa Matende na Mabusha (ngirimaji) katika Halmashauri 112 kati ya 119 na kubakiwa na Halmashauri saba nchi nzima.

"Ugonjwa wa Matende na Mabusha (ngirimaji) ni miongoni mwa changamoto kubwa za kiafya zinazoathiri wananchi katika maeneo hatarishi dhidi ya ugonjwa huu nchini, hapo awali maambukizi makubwa ya ugonjwa huu yalikuwa na katika Halmashauri 119 nchini ambapo watu milioni 31.2 walikuwa katika hatari ya kupata maambukizi ya vimelea vya ugonjwa huu" amesema Waziri Ummy.

Hata hivyo, ametaja Halmashauri zenye maambukizi mapya ya ugonjwa huo kwa hivi sasa kuwa ni Pangani, Mafia, Kinondoni, Kilwa, Lindi Manispaa, Mtama na Mtwara-Mikindani ambako kuna jumla ya wakazi 1,203,359.

Kwa upande wa Mkoa wa Dar es Salaam, Waziri Ummya amebainisha kuwa mnamo Machi na Agosti mwaka jana na Februari mwaka huu, Wizara ya Afya kwa kushirikiana na uongozi wa Mkoa huo na Halmashauri za Manispaa ya Kigamboni, Manispaa ya Ubungo, Manispaa ya Temeke, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na Manispaa ya Kinondoni walifanya zoezi la tathmini ya kiwango cha maambukizi ya ugonjwa huo katika halmashauri hizo.

"Kwamba matokeo ya tathmini hiyo yanaonyesha kuwa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni na Manispaa ya Ubungo hazina maambukizi mapya ya ugonjwa huo kwa kipindi cha miaka sita (6) baada ya kusitisha umezeshaji wa Kingatiba katika Halmashauri hizo"amesema Waziri Ummy.

Ameongeza kuwa, kwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Manispaa ya Temeke na Kata 10 za Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni ambazo ni Bunju, Kawe, Kunduchi, Mabwepande, Makongo, Mbezi Juu, Msasani, Mbweni, Wazo na Mikocheni kwa sasa hazina maambukizi mapya ya ugonjwa wa Matende na Mabusha.

Sambamba na hayo, amesema matokeo ya tathmini hiyo yanaonyesha Kata 10 za Manispaa ya Kinondoni ambazo ni Tandale, Kijitonyama, Mwananyamala, Kigogo, Mzimuni, Magomeni, Ndugumbi, Hananasifu, Kinondoni na Makumbusho bado zina maambukizi mapya ya ugonjwa wa Matende na Mabusha kwa kiwango cha asilimia 2.3.

Hata hivyo, amesema kutokana na matokeo hayo Wizara ya Afya imesitisha kampeni ya umezeshaji wa Kingatiba ya ugonjwa wa Matende na Mabusha katika maeneo husika ya Mkoa wa Dar es Salaam ambayo hayana maambukizi mapya.

“Maeneo haya ni Jiji la Dar es Salaam, Manispaa ya Temeke na Kata 10 za Manispaa ya Kinondoni. Maeneo haya yanaungana na Manispaaa ya Kigamboni na Ubungo ambazo tulisitisha kampeni za umezeshaji Kingatiba ya Matende na Mabusha mika sita (6) iliyopita,” amebainisha Waziri Ummy.

Amesema kuwa, zoezi la kampeni za umezeshaji wa Kingatiba ya ugonjwa wa Matende na Mabusha katika Kata 10 za Manispaa ya Kinondoni ambazo ni Tandale, Kijitonyama, Mwananyamala, Kigogo, Mzimuni, Magomeni, Ndugumbi, Hananasifu, Kinondoni na Makumbusho ambapo zoezi hilo litaendelea angalau kwa kipindi cha miaka miwili mfululizo kabla ya kurudia tena kufanya tathmini.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...