Skip to main content

SUKA KURAHISISHA USAFIRI

Na Mwandishi wetu, Habari Plus, Dar

Kampuni ya Teksol Limited iliyoko Jijini Dar es salaam imezindua Suka App maalum kwa ajili ya kurahisisha usafiri wa abiria ambayo itatoa huduma ya kipekee kutokana na mfumo huo namna ulivyotengenezwa na ulivyo rafiki kwa abiria.

 Akizungumza jijini Dar es Salaam Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Mkoa huo SACP Jumanne Murilo, wakati akimuwakilisha IGP Kamilius Wambura amesema kuwa kumekua na madereva wengi kuvunja sheria za barabarani hivyo haitasita kuwachukulia hatua za kisheria 

Aidha, amewata madereva wa Kampuni hiyo  kuwa waadilifu pindi wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao.

Kamanda Murilo amesema kwa kupitia Kampuni zilizopita zinazofanana na Suka App ikiwemo Uba na Bolt miongoni mwa vitu ambavyo vilikuwa vikilalamikiwa na wateja katika uendeshaji wa Kampuni hizo ni tabia za utendaji wa kazi ikiwemo lugha,mavazi, na heshima ambavyo ni miongoni mwa vitu vilivyojenga au kushusha heshima ya kampuni hizo.

"Katika kutekeleza ajira yenu ipo haja ya kufanya mafunzo na kuelekeza jinsi watu watakavyoendesha kampuni katika kutoa huduma sanjari na kutumia lugha zenye staha wakati wa kuwahudumia watu" amesema Kamishina Murilo

Amesema kampuni zinazotoa huduma ni wadau muhimu sana kwa Jeshi la Polisi na Serikali kwenye masuala ya kiusalama licha ya watu hao kupata kazi wao kama Jeshi wanatarajia kuwa nao karibu sana kama sehemu yao ya tatu ya jicho ya masuala ya kiusalama.

Aidha,ameitaka Kampuni ya Teksol kutoa ajira kwa watu ambao wanamsaada siyo tu kwa faida yao bali kwa faida ya Mkoa wa Dar es salaam na Taifa kwa ujumla.

Kwaupande wake Msimamizi wa mifumo ya Tehama Kampuni ya Teksol Limited Raphael Ndagala, amesema faida za kutumia Suka App ni usalama wa uhakika na bei.

"Kumekuwa na mfumuko wa bei katika kutumia usafiri huu mara bei inaongezeka bila utaratibu maalumu hivyo unapotumia huduma yetu unaweza kufuatilia gharama zako na kujua umetumia kiasi gani, amesema Ndagala.

Amesema suala la usalama tunalizingatia sana kutokana na kuwepo tabia za madereva kutofuata sheria za barabarani hivyo wao kama Suka App wamekuja na utaratibu wa kuhakikisha dereva anaekiuka sheria anawajibishwa ipasavyo kwa mujibu wa sheria hususani madereva pikipiki na bajaji.

Naye Afisa Leseni kutoka Mamlaka ya udhibiti usafiri ardhini (LATRA) Jonathani Kitururu, amesema kupitia kanuni za LATRA za usafiri wa kukodi za mwaka 2020 kanuni ya 18 ndio iayozungumzia Tax mtandao na unatoa mashariti ili Kampuni iweze kutoa huduma ni lazima wasajiliwe.

"Pia kanuni za LATRA zinatoa masharti kadhaa ikiwemo upatikanaji wa mfumo muda wote,kutoa taarifa sahihi kwa wakati pamoja na mtoa huduma aliesajiliwa kutoruhusiwa kutoa huduma kale ambapo leseni yake imemaliza muda wake", amesema Kitururu

Akizungumza kwenye uzinduzi huo Naibu Kamishina kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Alex Katundu, amesema uwepo wa huduma hiyo ni kigezo cha ukuaji wa uchumi ndani ya nchi.

"Kuongezeka kwa wadau wa uwekezaji kama Suka App ni Imani yangu kuwa tutaendelea kuwavutia wawekezaji kutoka nje ya nchi na ndani ya nchi hatua itakayosaidia kukuza uchumi wetu", amesema Katundu.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...