Skip to main content

WAZEE WA NGOME ACT WAPEWA NASAHA HIZI, SHEIKH PONDA YUMO

 


Na Mwandishi wetu, HabariPlus, Dar

NGOME ya Wazee wa Chama cha ACT Wazalendo imetakiwa kuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha umoja na mshikamano ndani ya chama na jamii kwa ujumla ikiwemo kuwa na sauti ya pamoja katika kutetea maslahi mapana ya Taifa.

Rai hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salam na Mjumbe wa bodi ya wadhamini wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Prof Azaveri Lwaitama wakati akifungua mkutano mkuu wa pili wa Chama hicho ambao umeenda sambamba na kuchagua viongozi wa nafasi mbalimbali katika ngome hiyo.

Amesema kuwa, ni vyema wajumbe wa mkutano huo kuchagua viongozi ambao wanauwezo wa kuongoza na kuacha tabia ya kuchagua viongozi kwa mfumo kwani matokeo yake wanakosekana viongozi bora wanaoweza kuongoza katika misingi inayotakiwa kwa busara na hekima .

"Mukitaka kufika mbali lazima muwe na sauti ya pamoja hata kama munatofautiana kwa itikadi ya vyama vyenu lakini linapokuja suala la kutetea maslahi ya nchi lazima mushikamane, hamuwezi kuondoa chama kilicho madarakani kwa kujitenga "amesema Prof Lwaitama.

Akitoa salamu fupi katika mkutano huo, Kamishna Msaidizi Mstaafu wa Jeshi la Polisi SACP Jamal Rwambo amesema kuwa mfumo katika vyama vya siasa ni tatizo sana, hivyo kama upo katika chama cha Act Wazalendo wanachama wanatakiwa kuukataa kwa vitendo kwani unakwamisha sana kupata viongozi bora ndani ya chama.

"Mfumo wa rushwa unawaweka pembeni watu ambao wangeweza kulisaidia taifa kwa uongozi wao, wachagueni watu wenye sifa kiongozi mzuri anaeweza kuisaidia ngome ya wazee ni yule ambae ni mkweli na sio muongo"amesema  SACP Jamal.

Awali akitoa salamu za Chama cha ACT Wazalendo  Mshauri wa Chama hicho, Juma Sanani amesema kuwa Wazee ndio kila kitu kwenye uongozi hivyo vijana wanapopewa ushauri wanatakiwa kuuzingatia kwani chama hicho hakina maslahi kwa mtu binafsi bali kwa wanachama wote.

Aidha, amewaomba wasimamizi wa uchaguzi huo kuhakikisha unakua wa huru na haki na kuzingatia ubora na viwango vya kimataifa, huku akiwataka wazee hapo kutumia hekima na busara katika kuhakikisha wanachagua viongozi bora watakaoongoza chama kwa maslahi ya Taifa.

Miongoni mwa wageni waalikwa katika mkutano huo ni pamoja na Sheikh Issa Ponda amesema kuwa wazee wana mambo mengi hivyo vijana wanaposhauriwa ni busara kuwasikiliza kwani hata wakiandika vitabu watu wakavisoma wataweza kujifunza vitu vingi sana.

"Wazee ndio chimbuko la fikra nzuri kwa hiyo wanatakiwa washirikishwe kwenye kila jambo, uchaguzi makini uzingatie uhalisia tunaoufahamu kuweni mfano mzuri wa kuigwa"amesema Sheikh Ponda.

Naye, Askofu Mwamakula amesema kuwa asimilia kubwa ya wananchi wanapokuona kwenye siasa unahutubia kiongozi wa dini wanakujaji kama wewe ni mwanachama wa chama fulani kumbe uhalisia haupo hivyo inawezekana umealikwa tu, hakuna ukweli hata asilimia moja.








Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...