Skip to main content

JUMIKITA YAALANI VIKALI WANAOTUMIA MITANDAO YA KIJAMII VIBAYA

 

Na mwandishi wetu, HabariPlus, Dar

Mwenyekiti wa Jukwaa la wanahabari wa Mtandao wa kijamii Tanzania (JUMIKITA ) Shabani Matwebe amelaani vikali vitendo vinavyofanywa na baadhi ya watu kutumia mitandao ya kijamii vibaya kwa kutoa lugha za matusi ambazo zimelenga kumdhalilisha mwanamke. 

Akizungumza na waandishi wa habari  Jijini Dar es salaam Matwebe amesema kumekuwepo na tabia kwa baadhibya watu kutumia mitandao hiyo vibaya kujadili matusi badala ya kujadili mambo ya maendeleo, huku tabia hiyo ikichukuliwa ni hali ya kawaida kwa baadhi ya watu.

Amesema kuwa, matusi yanayoendelea si kitendo cha kiungwana, matusi yanayojadiliwa mengi ambayo sasahivi yameshika hatamu ni kwamba mwanamke amekuwa mtu wa kutwezwa utu wake.

"Kwenye mitandao panapotokea matusi ya kuondoa utu wa mtu kwa namna ambavyo heshima na utu wake unavyotwezwa kutokana na kafsha au kebehi au dhalilishaji maana yake sisi kama taaisisi tuna wajibu wa kutoa mawazo yetu", amesema Matwebe.

Amesema kuwa, leo dunia nzima inapambana namna ya kumlinda mwanamke, na hakuna namna ya kulifanikisha jambo hili kama kwa kauli Moja tukikubaliana kwamba tujadili hoja, tuikosoe serikali, tuseme mahitaji ya wananchi, tuseme changamoto za wananchi ili Serikali ichukue hatua.

Hata hivyo, amesema wao kama Taasisi wameona wana mambo makuu mawili,wayatoletee ufafanuzi ikiwemo kukemea, kuendelea kunyamaza kimya ni kwamba tunaendelea kufanya jambo liendelea pasipo na msingi maalumu.

"Serikali mwaka huu inaingia kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa na mwakani uchaguzi mkuu, wapo watu mbalimbali watagombea wenye jinsia ya kike, kama leo hii watatwezwa na kudhalilishwa, nani mtoto wa kike atapata ujasiri wa kwenda kuchukua fomu,? anasimamaje jukwaani kusema chochote!"amesema Shaban.

Aidha, amevitaka vyombo na tasisi zote zinazotetea masuala ya wanawake kuacha kukaa kimya na badala yake wakemee na kulaani matusi ya mwanamke mwenzao kwa kuwa kukaa kimya kwao kuna maslahi wanayoyapata na matusi hayo.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...