Skip to main content

TAKUKURU KINONDONI YAPOKEA MALALAMIKO 84, YABAINI MAPUNGUFU MIRADI 6



Na Mwandishi wetu, Habari Plus, Dar

Mamlaka ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imebaini mapungufu kwenye miradi 6 ya maendeleo yenye thamani ya bill 61.910.746.284.42 ambapo wameahidi kuifuatilia kwa ukaribu zaidi miradi hiyo ili ikamilike kwa viwango vinavyoendana na thamani ya fedha iliyotolewa.

Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam na Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Kinondoni Elizabeth Mokiwa wakati alipokuwa akitoa taarifa ya kipindi cha miezi mitatu kuanzia January hadi March 2024 ambapo imekua  na utaratibu wa kutoa taarifa ya utendaji kazi kila baada ya miezi 3.

Amesema kuwa, miongoni mwa miradi walioifuatilia ni pamoja na ujenzi wa uwanja wa michezo Mwenge wenye thamani ya shill 4.065.100.285.23 ambapo umekamilika kwa asilimia 92  huku ikibaki ubandikaji wa kapeti ya nyasi.

"Mradi huu unakaribia kukamilika April 21 2024 kwa mujibu wa makubaliano mkataba, ufuatiliaji wa karibu unaendelea kuhakikisha mradi unakamilika kwa ubora na kuzingatia thamani ya fedha"amesema Mokiwa.

Ameongeza kuwa, pia wamefuatilia mradi wa mikopo wa asilimia 10 kwa makundi maalum ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kwa kipindi cha mwaka 2021/2022 katika Manispaa ya Ubungo wenye thamani ta Shill 2.504.217.430.00.

"Fedha, zilizotolewa kwa vikundi 382 ambapo vikundi 281 havijaresha kwa wakati mkopo wa kiasi cha shill 1.448.991.898.00, ufuatiliaji unaendelea ili kuhakikisha fedha za Serikali zinarejeshwa ili kusaidia makundi mengine mengi zaidi kujikwamua kiuchumi"amesema Mokiwa.

Aidha, Takukuru imepokea jumla ya malalamiko 84 ambapo malalamiko 40 yalihusu rushwa na 44 yasiohusu rushwa huku walalamikaji wakishauriwa na majadala kufungwa na wengine wameelekezwa sehemu sahihi ya kupeleka malalamiko yao.

"Malalamiko tuliyoyapokelewa Asasi binafsi 35,Tamisemi/Manispaa 19, Mahakama 6, Polisi 7, Benki 5, Elimu 3, Wizara ya ardhi 2, Tlb 1, Dini 1, Jkt 1, Nida 1, Tra 2 pamoja na Dawasa 1 ambapo inafanya jumla ya malalamiko 84 huku malalamiko mengine yalihusu madai, dhulma, kughushi, kutapeli, mikopo umiza na kutoridhishwa na kesi mahakamani"amesema Mokiwa.

Hata hivyo, amesema katika kuhakikisha Takukuru inatoa huduma inayowafikia wananchi wote wamejiwekea mikakati kwa kipindi cha April/Juni 2024 ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa Progrumu ya Takukuru-Rafiki kwa lengo la kuendeleza ushirikiano na wananchi pamoja na wadau.

Aidha, amesema wanaendelea kutoa elimu ya rushwa na dawa za kulevya kwa vijana walioko mashuleni ili watambue madhara ya rushwa na dawa za kulevya na kuchukua hatua kwa maslahi ya taifa pamoja na kufanya vikao vya wadau na watoa huduma katika kata zao.

Aidha, wametoa wito kwa wananchi wote katika mkoa wa kinondoni wanapopata taarifa zozote za rushwa  kutoa taarifa kupitia mitandao yote ya simu kwa kupiga au kutuma ujumbe mfupi kwa namba ya dharura 113 bure au uwasiliane kupitia namba ya mkuu wa Takukuru kinondoni 0738150236 pamoja na mkuu wa Takukuru wilaya ya Ubungo 0738150238.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...