Skip to main content

TAWA YAWEKA KAMBI RUFIJI, ELIMU YA KUEPUKA MADHARA YA MAMBA NA VIBOKO YATOLEWA

Na. Beatus Maganja

Timu ya Maofisa uelimishaji kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA imeweka kambi maalumu wilayani Rufiji yenye lengo la kutoa elimu ya namna ya kuepuka madhara yatokanayo na mamba na viboko kwa wananchi walioathiriwa na mafuriko wilayani humo.

Hayo yamesemwa leo na Afisa habari wa TAWA Beatus Maganja alipokuwa akiongea na waandishi wa habari wilayani humo.

"TAWA tumeweka Kambi katika wilaya ya Rufiji kufuatia mafuriko yaliyojitokeza katika wilaya hii yaliyoathiri watanzania wenzetu" amesema

"Jambo lililotuleta hapa, kwanza ni kutoa pole kwa watanzania wenzetu ambao wamekumbwa na mafuriko haya, lakini pia tumekuja mahsusi kwa ajili  ya kutoa elimu ya namna  wananchi hawa wanaweza kuchukua tahadhari kwa madhara yanayoweza kutokea kutokana na wanyamapori wakali na waharibifu kama vile mamba na viboko" ameongeza Maganja

Afisa uelimishaji kutoka TAWA Kanda ya Kusini Mashariki Jimmy Mshana amesema TAWA ilianza kutoa elimu hiyo katika maeneo mbalimbali wilayani humo ikiwemo Kata ya chemchem na vitongoji vyake vyote na leo Aprili 15, 2024 elimu hiyo imeendelea kutolewa katika Kata ya mgomba na vijiji vyake vyote na kukiri kupata mwitikio mzuri kutoka kwa wananchi.

Mwenyekiti wa Kijiji cha mgomba kusini Kassim Ally Mtumbei ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Waziri wa TAMISEMI ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Rufiji Mhe. Mohamed Mchengerwa kwa elimu ya kujikinga na madhara ya wanyamapori wakali na waharibifu waliyoipata kutoka kwa maofisa wa TAWA walioweka kambi wilayani humo.

 Imeelezwa kuwa mafuriko katika wilaya hiyo mbali na kuharibu makazi ya watu na mali zao,  yameambatana na athari mbalimbali ikiwemo ongezeko la matukio ya wanyamapori wakali na waharibifu hususani mamba na viboko ambao wametoka kwenye maeneo yao ya asili na kusogea karibu na makazi ya watu kwa kusafirishwa na mikondo ya maji.

Ili kuepuka madhara yanayoweza kusababishwa na wanyamapori hao, TAWA imepeleka vikosi vya doria kwa ajili ya kuwadhibiti na kutoa elimu kwa jamii ya kuchukua tahadhari kuepukana na madhara yanayoweza kusababishwa na wanyamapori hao, na hii ni katika kuonesha namna ambavyo TAWA inavyothamini na kujali maisha ya binadamu

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...