Skip to main content

MEYA WA JIJI LA DAR ATUMA SALAMU KWA MWARI KIGEGO


Na mwandishi wetu, HabariPlus, Dar

Diwani wa Kata ya Vingunguti ambae pia ni Meya wa jiji la Dar es Salaam Omar Kumbilamoto ametuma salamu kwa watu wanaomchafua kuwa hakuna maendeleo yoyote anayoyafanya katika kata hiyo na badala yake ana mpango wa kuuza shule na Zahanati kwa mwekezaji.

Salamu hizo amezitoa jijini Dar es Salaam wakati alipokua akizungumza na wachama wa  umoja wa wanawake (UWT) Kata ya Vingunguti na wananchi katika mkutano maalum wa uzinduzi wa kampeni za uchaguzi wa Serikali za mitaa wa mwaka huu.

Amesema kuwa, kuna baadhi ya watu ambao hawana nia njema na Kata wamekua wakisambaza taarifa za uongo hivyo amesema maendeleo yaliofanywa na Rais Dkt Samia katika hiyo ni makubwa kwani amegusa sekta zote kwenye maendeleo.

"Nimekua nikisimamia miradi mbalimbali ya maendeleo katika kata hii ikiwemo sekta ya elimu kama vile ujenzi wa shule, madawati, pamoja na miundombinu ikiwemo barabara na maji na hivi sasa kuna barabara 3 ambazo zimeingia katika mpango wa ujenzi wa lami"amesema Kumbilamoto.

Ameongeza"Nataka nimtumie salamu huyu mwari kigego ambae anapita akisambaza taarifa za uongo Zahanat na Shule ni mali ya Serikali nauza mimi kama nani, Ccm ndio chama pekee ambacho kimeleta maendeleo kabla ya uongozi huu uliopita ulitoka ukanda wa gaza walifanya nini cha maana katika Kata hii"amesema 

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Kata ya Vingunguti, Sharifa Mwendo amewataka wanawake wa kata hiyo kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa Serikali ya mtaa huku akiwapigia kampeni viongozi waliopo madarakani .

"Viongozi waliopo sasa hivi wanatosha kuanzia Diwani, Mbunge na Rais kwani wametumia madaraka yao vizuri kwa kuletea  maendeleo makubwa katika sekta zote, nitawashangaa nikimuona mtu anachukua fomu ya nafasi ya udiwani, ubunge na Urais"amesema Mwendo.




Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...