Skip to main content

RAIS DKT SAMIA KESHO KUTUA KOREA, MIKATABA SABA KUSAINIWA

 

Na Mwandishi wetu, HabariPlus

Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kesho anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi ya siku sita nchini korea yenye lengo la kukuza ushirikiano kati ya nchi hizo mbili. anaenda kufanya  Ziara ya kikazi. 

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Waziri wa Mambo ya Nje January Makamba amesema kuwa pamoja na mambo mengine pia atasaini mikataba saba na Rais wa nchi ya korea yenye lengo la ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

"Miongoni mwa mikataba  hiyo ni pamoja na mikataba  hati ya makubaliano kati ya Taasisi ya madini Tanzania na Taasisi ya miamba nchini korea, huu ni ushirikiano unahusu utafiti, uchoraji ramani, rasilimali na uchoraji  wa maabara"amesema Waziri Makamba.

Ameongeza"mkataba wa pili ambao unaenda kusainiwa ni ushirikiano wa uchumi wa bluu, huku mkataba wa tatu ukihusu kwenda kutambua vyeti vya mabaharia  na tutaweza kusaini tamko la pamoja kuhusu siasa  na makubaliano ya hati ya madini, viwanda na biashara  "amesema Waziri makamba

Hata hivyo, mkataba mwingine ni msaada wa fedha kutoka benki ya Exim nchini korea  na Serikali ya  Jamhuri ya muungano wa Tanzania ambao unaenda kupelekea Tanzania  kupata msaada na mikopo nafuu, pia wanakwenda kushirikiana na chuo kikuu kutoka nchini korea katika kuendeleza huduma za usafiri wa anga nchini.

Aidha, amesema ziara hiyo imedhamiria  kuendeleza  ushirikiano  baina ya Serikali ya Tanzania na Korea kwenye mambo muhimu ikiwemo elimu, afya, na miundombinu hivyo ziara hiyo inaenda kuleta mafanikio mbalimbali nchini Tanzania.

Aidha  Waziri  Makamba ameongeza kuwa kuhusu madini kwenye mkakati watasaini  mkataba katika kuwezesha  kuchambua, na kufanya mkakati na shirika la madini Tanzania  STAMICO na shirika la ukarabati  wa madini nchini Korea.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...