Skip to main content

SERIKALI KUKUZA BUNIFU, COSTECH YAJIVUNIA

 


Na Mwandishi wetu, HabariPlus,Dar

Serikali imesema itaendelea kusapoti bunifu zote zinazofanywa na watu mbalimbali, huku ikiahidi kukuza sayansi kwa lengo la kuchagiza maendeleo chini Tanzania.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Sayansi na Teknolojia kutoka Wizara ya elimu sayansi na Teknolojia Profesa Ladslaus Mnyone wakati akimuwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Carolyne Nombo katika mdahalo maalum uliowakutanisha wahariri, waandishi wa habari na wadau wa ubunifu, ulioandaliwa na Tume ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (COSTECH) chini ya programu ya ufunguo.

Amesema kuwa, pia Serikali itahakikisha inakuza sayansi, teknolojia na ubunifu, lengo ikiwa kusaidia kufanyika kwa tafiti zinazojibu changamoto za watanzania, katika kuhakikisha sekta ya teknolojia na ubunifu inakua huku ikikamilisha mkakati wa teknolojia ya TEHAMA

Kwa upande wake,  Mkurugenzi wa COSTECH Dk.Amos Nungu, amesema wiki ya ubunifu, costech na wadau wa maendeleo wanajivunia mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na uwepo wa uelewa wa pamoja ulioleta matokeo chanya.

Amesema kuwa, wiki ya bunifu itazinduliwa leo katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Julias Nyerere (JNICC), huku kilele chake kikitarajiwa kufanyika mkoani Tanga.

Amesema kuwa, wiki hiyo ya ubunifu itaenda sanjari na maadhimisho ya miaka 10 ya toka kuanzishwa kwakwake,ambayo kwa mwaka huu imebebwa na kauli mbiu “Ubunifu kwa maendeleo jumuishi ya rasilimali watu”.

Aidha ameongeza kuwa, wiki ya bunifu imeweza kutoa fursa na kuongeza uelewa kwa vijana wengi na baadhi yao wamepata fursa ya kuonekana na kujulikana zaidi.

Hata hivyo, amesema maendeleo jumuishi ya rasilimali watu”.

“Katika kuelekea wiki ya ubunifu COSTECH na wadau wa maendeleo tunajivunia mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na uwepo wa uelewa wa pamoja ulioleta matokeo chanya,”amesema Dkt Nungu

Aidha ameongeza kuwa, wiki ya bunifu imeweza kutoa fursa na kuongeza uelewa kwa vijana wengi na baadhi yao wamepata fursa ya kuonekana na kujulikana zaidi.

Naye, Meneja Progaramu kutoka funguo, Joseph Manirakiza amesemakatika wiki ya uvumbuzi wanafurahia nguvu ya mageuzi ya juhudi shirikishi katika kuendeleza teknolojia na uvumbuzi.

Amesema kuwa, tukio hilo linatoa jukwaa kwa wiki ijayo ya kitaifa ya ujuzi wa elimu na uvumbuzi inayoangazia makutano muhimu ya nyanja hizi.

Janeth Martoo ni Meneja Progaramu wa Umoja wa Ulaya amesema ubunifu unahitajika zaidi kwasababu unasaidia katika kukuza ustawi wa uchumi wa taifa.

Amesema licha ya chagamoto zinazotokana na mabadiliko ya tabia chi bado anaamini sekta ya ubunifu ikipewa kipaumbele itaongeza nguvu katika kukuza uchumi.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...