Skip to main content

ACT YAPINGA TAMISEMI KUSIMAMIA UCHAGUZI

 

Na Mwandishi wetu, Habari Plus

Chama cha ACT-Wazalendo kimesikitishwa na taarifa walipokea kutoka kwa msajili wa vyama vya siasa kuwataarifu kuwa Wizara Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) itaendelea kusimamia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwani kufanya hivyo ni kuvunja sheria. 

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Chama hicho Ado Shaibu amesema wapokea barua ambayo inaeleza TAMISEMI inaendelea na maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa, ambapo Juni 15, 2024 itafanya kikao cha wadau kukusanya maoni ya rasimu ya kanuni zitakazosimamia uchaguzi huo.

Amesema kuwa kitendo cha Tamisemi kusimamia uchaguzi wa Serikali za mitaa ni kuvunja sheria kwani kifungu cha 10(1)(c) cha Sheria ya Tume Huru ya Uchaguzi ya Mwaka 2024, kinaeleza tume hiyo ndio  imepewa jukumu la kusimamia uchaguzi wa mitaa, vijiji na vitongoji. 

"Msimamo wa muda mrefu wa Chama chetu ni kuwa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi badala ya TAMISEMI ndiyo maana ACT Wazalendo tulishiriki kikamilifu kuhakikisha kuwa Bunge linapitisha kifungu cha Sheria kuwezesha jambo hilo," amesema Ado

Ameongeza"Ni jambo la kusikitisha kuwa Serikali hadi leo inasuasua kupeleka muswada Bungeni kutekeleza matakwa haya ya Sheria na badala yake inataka kuvunja Sheria kwa kuipa madaraka TAMISEMI kusimamia uchaguzi wa Serikali za Mitaa,".

Amesema kuwa, hatua yoyote inayochukuliwa na TAMISEMI hivi sasa kuhusiana na usimamizi wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni batili na ni kinyume na sheria.

Akieleza kuhusu msimamo wa ACT Wazalendo, ameeleza watakwenda kwenye kikao cha wadau kilichoitishwa Juni 15, 2024 Dodoma kuieleza TAMISEMI isimamishe mara moja michakato inayoendelea nao wa maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa sababu ni batili na unavunja sheria za nchi.

Katika kuhakikisha hawakubalinia na uamuzi huo, chama hicho wamewasiliana na Asasi za Kiraia juu ya umuhimu wa kufungua kesi mahakamani kuzuia hatua za maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa zinazoendelea kuchukuliwa na TAMISEMI. 

"Tumefarijika kuwa Asasi hizo zipo kwenye hatua za mwisho kufungua kesi hiyo. ACT Wazalendo itatoa ushirikiano kwa taasisi hizo kwenye kesi hiyo" amesema Ado.

Sambamba  na hayo amebainisha kuwa kufuatia hali inayoendelea na kutokana na unyeti wa jambo lenyewe, wataandaa kikao maalum na kuvialika vyama vingine vya siasa kuweka msimamo wa pamoja juu ya kuizuia TAMISEMI kusimamia uchaguzi wa Serikali za Mitaa na pia kuteuliwa wajumbe wapya wa Tume Huru ya Uchaguzi ili wachukue nafasi ya waliopo sasa kwa mujibu wa sheria, ambao ndio waliovuruga uchaguzi wa 2020.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...