Skip to main content

JESHI LA POLISI LAJIPANGA KUKABILIANA NA VITENDO VYA KIHALIFU

Jeshi la Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam Aprili mwaka huu,limesema limeongeza nguvu ya kukabilli viashiria vya vitendo vya kialifu na waarifu na kufanikiwa kukamata watu 13 wanaotuhumiwa kutumia, kuuza na  kuusambaza dawa za kulevya jijini humo.

Pia kuanzia kipindi hicho limefanikiwa kukamata watuhumiwa hao wakiwa na kete 2,639, misokoto 158 na Puli 531 za bangi iliyokuwa imefungashwa tayari kwa matumizi,  viroba vinne vya dawa hizo pamoja na pikipiki mbili ambazo zinaaminika kutumika kisafirishia.

Hayo yamebanishwa leo, Juni 7, 2024 jijini Dar es Salaam na  Kamanda wa Kanda Maalumu  wa jiji hilo SACP, Jumanne Muliro wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari.

"Hatutaki kurudi nyuma tulikotoka ambako kulikuwa na vitendo vingi vya kiarifu, tutaendelea kudhibiti viashiria vyote vya kiarifu na waharifu ili  kulifanya Jiji hili kuendelea kuwa tulivu na usalama wakati wote.

"Katika operesheni ambayo tumefanya baada kubaini uwepo wa viashiria vya vitendo vya kiharifu kutaka kufanyika kutokana na baadhi ya watu waliohukumiwa kumaliza adhabu zao na  kurejea  mitaani na kuonekana kutaka kufanya tena uharifu, tumekamata watuhumiwa 13 wakiwa wanapanga njama hovu  wakiwa siraha toi (bandia).

"Katika watuhumiwa hao yupo anayefahamika kwa jina la Hamisi Seif (18) mkazi wa Mbondole na Bosco Bosco mkazi wa Kipunguni Ilala (18), hivyo tunatoa onyo kwa yeyote anayetaka kufanya uharifu afahamu kuwa tutamdhibiti na kumshugulikia kabla hajafanikisha adhima yake na tuomba wananchi waendelee kutupa ushirikiano,"  amesema.

SACP Muliro ametaja pikipiki mbili ambazo zimekamatwa ni MC 673 CKM na MC 591 CUW ambazo zinaaminika zilikuwa zinatumika kusambaza bangi hizo. 

“Jeshi la Polisi linaendelea kusimamia mkakati wakemaalum wa kuzuia vitendo vyote vya kihalifu katika jiji la Dar es Salaam. Kazi hii maalum ya kuzuia vitendo vya kihalifu ni muendelezo wa kazi hiyo iliyoanza Aprili 2024 na inayoendelea kulenga, kufuatilia, kuchunguza na kukamata wahalifu mbalimbali pamoja na wanaopanga njama za kuiba, kuvunja nyumba, wanaouza, kusafirisha na kutumia dawa za kulevya”amesema SACP Muliro

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...