Skip to main content

NAIBU WAZIRI MKUU DKT BITEKO KUFUNGUA KONGAMANO LA KIMATAIFA LA UCHUMI WA BLUU


Na Mwandishi wetu, HabariPlus

Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI)  kwa kushirikiana na Chuo Cha Bahari cha Ghana wameandaa kongamano la 3 la kimataifa la uchumi wa bluu ambalo pamoja na mambo mengine wanakwenda kujadili maendeleo ya teknolojia ili kuhakikisha uchumi wa bluu unakua endelevu.

Aidha, Naibu Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Dotto Mashaka Biteko anatarajiwa kufungua kongamano hilo la siku mbili  ambalo litahudhuriwa na wadau mbalimbali wa mnyororo wa thamani wa uchumi wa bluu.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Mkuu wa Chuo cha DMI, Dkt Tumain Gurumo amesema kuwa lengo la kongamano hilo ni kuiangalia kesho ya uchumi wa bluu inayojumuisha ulinzi, usalama na mabadiliko ya tabia ya nchi pamoja na maendeleo ya teknolojia kwa ukuaji wa uchumi wa bluu .

Amesema kuwa, katika kongamano hilo litahudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo taasisi za umma, binafsi, Serikali, wanasiasa , wataalamu wa bahari, utalii, bandari, mafuta na gesi pamoja na uvuvi.

"Lengo la kuwaalika wadau wote hawa ni kutaka ushiriki wa kila mdau katika mnyororo wa thamani wa uchumi wa bluu, mfano samaki anapovuliwa baharini kunakuwa na wadau wengi wanahusika hadi anapokufikia wewe mlaji, hivyo hawa wote wanatakiwa wapate mafunzo na elimu"amesema Dkt Gurumo.

Aidha, amesema kuna fursa nyingi kwenye uchumi wa bluu hivyo ni vyema kuzingalia kwa pamoja kwa kuwashirikisha vijana kwani wasipozifahamu hawawezi kuzindea wala kutoa msaada wowote wa ukuaji kwenye uchumi wa bluu .

Hata hivyo, amesema tafiti mbalimbali zimefanywa na wadau hivyo, kupitia kongamano hilo zitajadiliwa na wadau hao kutoka na   mapendekezo ambayo yatasaidia nchi ya Tanzania katika kukuza uchumi wa bluu.

Ameongeza kuwa, pia kongamano hilo linatarajia kujumuisha nchi 11 ikiwemo Kenya, Comoro, Liberia, Ghana Nigeria, Sieraleone, Denmark, Italy, Sweeden, Korea Kusini na China ambapo lengo ni kutoa elimu na mafunzo pamoja na kuangalia vyanzo vya maji na faida zake katika kukuza kipato.

Aidha, Kongamano la kwanza lilifanyika mwaka 2022, la pili lilifanyika mwaka 2023 na la tatu linatarajiwa kufanyika Julai 4  hadi 5 mwaka huu katika ukumbi wa kimataifa wa Julius Nyerere ( JINCC) ambapo mambo mbalimbali yatajadiliwa na wadau hao ikiwemo kujifunza namna ya kukuza uchumi wa bluu kwenye nchi zao.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...