Skip to main content

TAASISI YA MAMA ONGEA NA MWANAO YATOA VITI MWENDO 250 KWA WATOTO WENYE UHITAJI


Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wametoa msaada wa viti mwendo 250 kwa ajili ya watoto wenye uhitaji maalum ambavyo vitawasaidia kutimiza ndoto zao za kupata elimu.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Steve Nyerere amesema kuwa kampeni hiyo ya kugawa viti mwendo kwa watu wenye mahitaji maalum ni juhudi za kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluh Hassan katika kuhakikisha watoto wote wanapata elimu.

Amesema kuwa, kuna baadhi ya wazazi wamekuwa wakipitia wakati mgumu mara baada ya kujifungua watoto wa aina hiyo kwani hutelekezwa na waume zao.

"Kuna wanaume ni wazembe katika kulea watoto wenye ulemavu ambapo hufikia kusema watoto hao sio wa kwao na kuwatelekeza, kuwaacha katika mazingira magumu"amesema Steve.

Ameongeza kuwa, mtoto kuzaliwa na hali ya ulemavu haimzui kupata haki yake ya msingi ya kupata elimu bora kwani kupata mtoto mwenye hali hiyo ni mipango ya Mwenyezi Mungu, hivyo wana haki sawa kama watoto ambao wamezaliwa bila ulemavu.

"Naomba jamii iondoe dhana potofu juu ya mtoto mwenye ulemavu hasa wanaume maana hawa ndio wamekua wakiwatelekeza sana, sisi kama taasisi tupo tayari kupeleka msaada popote hivyo tunaomba na wadau wengine watuinge mkono"amesema Steve.

Kwa upande wake Katibu wa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao,  Evon Sherry (Monalisa)  amesema taasisi hiyo imetembelea mikoa mitano na kubakisha mikoa miwili kwa jili ya viti mwendo kwa wahitaji.

Amesema kuwa, kampeni ya "Baskeli ya shule ya Mama" inalenga kumsaidia mtoto mwenye uhitaji kupata elimu, hivyo watahakikisha wanawafikia watoto wengi ili waweze kutimiza ndoto zao.

"Rais Dk.Samia Suluhu Hassan anawasaidia wakina mama katika sekta mbalimbali ikiwemo afya,  maji na nishati lakini sisi tumeamua kumtua mama mtoto mgongoni"amesema Evon

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...