Skip to main content

BATA LA MSITUNI FESTIVAL KUFANYIKA PUGU KAZIMZUMBWI, DC MAGOTI AELEZEA

Na Mwandishi wetu, Habari Plus, Dar

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Mkoani Pwani Petro Magoti amewataka watanzania kushiriki kikamilifu katika tamasha kubwa la Msituni maarufu kama "Bata Msituni Festival" lengo ni kuunga mkono jitihada za Rais Dkt Samia katika kutangaza utalii wa Tanzania.

Aidha, tamasha hilo linatarajia kuwakutanisha watu 3000 kutoka ndani na nje ya nchi ambapo mpaka sasa nchi tatu zimeshathibitisha kushiriki katika tamasha hilo na nyengine zinajiorodhesha ambapo pamoja na mambo mengine watu wataweza kupata burudani za kutosha kutoka kwa wasanii mbalimbali.

Akizungumza na waandishi wa habari wilaya ya kisarawe  katika hifadhi ya msitu wa mazingira asilia Pugu  Kazimzumbwi ambao unasimamiwa na wakala wa huduma za misitu Tanzania (TFS) ambapo amesema  tamasha hilo kwa mwaka huu litakuwa ni la kipekee kwani watanzania watapata fursa ya kukaa katika msitu huo kwa takribani siku sita wakifurahia maisha na mandhari ya msitu huo.

 "Msitu huu hauna wanyama wakali bali una mandhari mazuri sana na wanyama mbalimbali wa kuvutia ikiwemo, panzi mwenye rangi ya bendera ya Taifa, ushoroba na Bwawa la Minaki ambapo watapata fursa ya kuvua samaki, kutembea na mitumbwi ndani ya bwawa, kuweka kempu maalum, kula na kunywa na kupata burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali na ngoma za asili ikiwemo ngoma ya vanga ya kizaramo" amesema Dc Magoti.

"Tamasha hili pia litahusisha mama ntilie ambao watapika vyakula mbalimbali, hivyo tunaomba waje wajiandikishe kutakua na mbio za pikipiki, kukimbia Msituni pia kutakuwa na samaki choma, nyama choma, Mihogo pamoja na ngoma za asili yaani hata wewe na mkeo mkija mkataka mchomewe mbuzi mzima mtachomewa halafu kutakuwa na siku ya kupanda Mlima ambapo wahudhuriaji watapata fursa ya kuliona Jiji lote la Dar Es Salaam kwa takribani asilimia 95 kutokea juu ya mlima hapa hapa Kisarawe" amesema DC Magoti.

Aidha, ameongeza uwa tamasha hilo kubwa la Msituni Afrika ya Mashariki linatarajiwa kuhudhuriwa na watu takribani elfu tatu wengi wakiwa ni watalii kutoka nje ya Mipaka ya Tanzania kwa kukaa katika eneo moja na Watanzania kusheherekea utamaduni na uzuri wa asili wa Afrika  na ambapo watakaohudhuria tamasha hilo watapata Kila aina ya burudani wanayoitaka maishani kupitia utalii wa ndani sawa na dhana ya utalii hapa nchini 'Tanzania Unforgetable' yaani Tanzania isiyosahaulika.

Amesema Tamasha hilo litahusisha watu kutoka mataifa mbalimbali ikiwemo Afrika ya Kusini, Kenya,Uganda huku Tanzania ikiwa mwenyeji wa shughuli hiyo ambayo itafanyika ndani ya hifadhi ya msitu wa asili,Pugu Kazimzumbwi ambapo kiingilio cha juu kitakuwa shilingi laki moja na nusu 15,0000 kwa watanzania kwa siku zote nne watakazokuwa ndani ya msitu huo, kwa wageni laki 250000.

Kwa upande wake, Afisa Mhifadhi wa wilaya ya Kisarawe kutoka wakala wa huduma za misitu Tanzania(TFS) ambaye pia ni Meneja  wa hifadhi hiyo ya msitu  asili,Pugu-Kazimzumbwi Baraka Mtemwa amewakaribisha watanzania kutembelea hifadhi hiyo kwani watajionea vitu mbalimbali ikiwemo miti, ndege panzi mwenye rangi za bendera ya Taifa la Tanzani,Ushoroba na Bwawa la Minaki,huku akisisitiza pia huduma ya malazi kwenye mazingira ya msitu huo pia inapatika na wamejipanga vyema kuwahudumia watakaoshiriki Bata msituni Festival.

Tamasha la 'Bata Msituni Festival' ni sherehe ya kipekee ya Kiafrika inayolenga kuenzi na kukuza utalii wa mazingira na utamaduni, uzuri wa asili wa Afrika na Tanzania kwa ujumla, na watu wake kupitia utamaduni, sanaa na shughuli mbalimbali za burudani.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...