Skip to main content

RC CHALAMILA AONGOZA KIKAO CHA BODI YA BARABARA NA KAMATI YA USHAURI YA MKOA

#Atoa maelekezo mahususi juu ya ufanisi na utekekelezaja wa miradi ya barabara katika Mkoa.

#Ataka kuwa na ubunifu wa matumizi ya ‘Road Reserve’ na maeneo ya wazi.

#Asema Dar es Salaam ni salama sana vitendo vichache vya kiharifu vimeendelea kudhibitiwa.






Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo Julai 24,2024 ameongoza kikao cha bodi ya barabara na Kamati ya ushauri ya Mkoa kilichofanyika katika ukumbi wa Arnatoglo Mnazi mmoja -Ilala.

RC Chalamila akiongoza kikao hicho alipata wasaa wa kusikia michango na ushauri kutoka kwa wajumbe wa kikao hicho ambao ni waheshimiwa wabunge na wataalam wengine ambao walihudhuria kikao na baadaye Mhe Mkuu wa Mkoa aliwahakikishia wajumbe kulipatia suluhu tatizo la ucheleweshaji wa utekelezaji wa miradi ya barabara hususani ile ambayo tayari ilishatangazwa kutekelezwa, kwa hatua ya awali amemtaka Katibu Tawala wa Mkoa Dkt Toba Nguvila kuratibu timu ya watu wachache kwa ajili ya kwenda kumuona waziri mwenye dhamana.

Aidha RC Chalamila ameagiza kuendelea kutoa elimu na kuhamasisha watu kuacha kujenga kwenye mabonde,na kuendelea kulinda kingo za mito kwa kupanda miti kandokando ya mito ambapo ameshauri ipandwe miti ya michikichi ambayo inapatikana Kigoma,hivyo katibu Tawala wa Mkoa alifanyie kazi jambo hilo

Vilevile RC Chalamila ameagiza kuwapanga vizuri wafanyabiashara wadogo na maeneo ya ‘Road Reserve’ pamoja na ya wazi kuwe na ubunifu wa matumizi yenye tija na maslahi mapana kwa umma,pia wale ambao majengo yao yanaangalia barabarani washirikishwe kuweka perving na kupanda miti ya kuvutia ambayo italeta taswira nzuri ya Mkoa, hata hivyo kwenye suala la ubora na uwekaji wa viraka barabarani ameagiza kutekelezwa kwa wakati hususani zile sehemu zilizoharibiwa na mvua za El-Nino.

 

Sanjari na hilo RC Chalamila amesema kwa upande wa ulinzi na usalama Mkoa uko shwari sana vitendo vichache vya kiharifu vimeendelea kudhibitiwa ambapo ametoa rai kwa kila mtu kuelimisha jamii kufuatia uzushi unaosambazwa katika mitandao ya kijami kuhusu kutekwa na ukatili dhidi ya watoto ni vizuri kutoa elimu ili kuondoa taharuki kwa jamii “suala la usalama ni jukumu letu sote tuendelee kushikamana” Alisema Chalamila.

Aidha kikao hicho kilihudhuriwa na Kamati ya Usalama ya Mkoa, Viongozi wa chama Mkoa, TARURA, TANROAD, makatibu Tawala wa Wilaya kwa niaba ya wakuu wa Wilaya, Mameya, Katibu Tawala wa Mkoa Dkt Toba Nguvila na wataalamu wengine kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...