Skip to main content

WANANCHI RUFIJI WAISHUKURU TAWA KWA KUWAOKOA DHIDI YA ATHARI ZA KUCHEPUKA KWA MTO

Na. Beatus Maganja 

Wananchi wa Kijiji cha Ngarambe, Kata ya Ngarambe wilaya ya Rufiji Mkoani Pwani wameishukuru Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA kwa msaada wa kuchepusha mto  uliobadili uelekeo wake  kutokana na mvua nyingi zilizonyesha Mwaka huu zikiambatana na kimbunga HIDAYA na kusababisha  uelekeo wa Mto kuelekea katika makazi na mashamba ya wakazi wa Kijiji hicho na kusababisha uharibifu wa mashamba na makazi ya wananchi hao.

Wananchi hao wametoa shukrani hizo Julai 26, 2024 kwa TAWA kupitia uongozi wa Pori la Akiba Selous Kituo cha Kingupira kwa kutoa mashine inayosaidia kuchepusha mto huo kutoka makazi ya watu, jambo ambalo wamekiri kuwa litasaidia kuokoa maisha ya watu na mali zao.

Salum Kassim ambaye ni  mkazi wa Kijiji cha Ngarambe amesema mvua kubwa zilizonyesha Mwaka huu ambazo ziliambatana na kimbunga HIDAYA zilisababisha athari kubwa kwa wakazi wa Kijiji hicho kama vile kuharibu makazi yao kwa kubomoa nyumba, kuharibu majengo ya shule na vyoo vya shule  hasa baada ya Mto kubadili uelekeo wake kutokana na kujaa maji mengi.

Salum anasema kutokana na ushirikiano mzuri na ujirani mwema baina ya Kijiji hicho na Pori la Akiba Selous , waliomba msaada  TAWA kupitia  uongozi wa Kituo cha Kingupira kilichopo  katika Hifadhi hiyo na uongozi huo kukubali kutoa mashine ambayo inaendelea kufanya kazi ya kuchepusha mto ili kuokoa maisha na mali za wananchi hao.

Kaimu Kamanda wa Pori la Akiba Selous ambaye pia ni msimamizi wa Kitengo cha ujirani mwema, Jimmy Mshana amesema Kijiji cha Ngarambe ni majirani wa Hifadhi hiyo ambao wamekuwa na ushirikiano nao wa muda mrefu katika masuala mbalimbali ya kijamii na kiuhifadhi hivyo baada ya kuona wamepata changamoto hiyo walilazimika kutoa msaada wa haraka ili kuweza kuwaokoa kwa kuchepusha mtu huo ili wasije wakapatwa madhara makubwa zaidi.

Amesema kazi ya kuchepusha mto huo imefanyika kwa ushirikiano mkubwa kupitia viongozi mbalimbali wa Kata na Kijiji husika pamoja na wananchi wote kwa ujumla.

TAWA imekuwa na mchango mkubwa kwa wananchi waishio pembezoni mwa Hifadhi mbalimbali inazozisimamia nchini kupitia progamu za ujirani mwema jambo ambalo limewafanya wananchi hao wajivunie uwepo wa Taasisi hiyo katika maeneo yao.

 Ikumbukwe kuwa mapema Mwaka huu TAWA ilitoa misaada mbalimbali ikiwemo vyakula na magodoro kwa wananchi wa wilaya ya Rufiji waliopatwa na mafuriko pamoja kuwapa elimu ya namna ya kuepuka madhara yanayoweza kusababishwa na wanyamapori wakali na waharibifu hususani mamba na viboko.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...