Skip to main content

WAPANGAJI WA NYUMBA ZA TBA, KULIPA KODI NI WAJIBU: WAZIRI BASHUNGWA

 



Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa(Mb) amewataka Wapangaji wanaokaa kwenye nyumba na majengo ya Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kutimiza wajibu wao wa kulipa kodi ya pango ili fedha hiyo itumike kujenga majengo mapya na kuboresha huduma katika majengo mengine ya Wakala huo.

Bashungwa ametoa agizo hilo leo Julai 23, 2024 katika hafla ya ufunguzi wa jengo la makazi ya watumishi wa umma la Magomeni Kota Awamu ya Pili B la ghorofa saba katika Halmshauri ya Manispaa ya Kinondoni, Mkoani Dar es Salaam.

“Serikali itaendelea kufanya kila jitihada za kujenga makazi bora ya watumishi, lakini Watumishi mliopata fursa ya kukaa kwenye nyumba za TBA, kulipa kodi ni wajibu. Mkilipa kodi inatupa uwezo wa kuboresha huduma ya makazi bora”, amesisitiza Bashungwa.

Bashungwa ameielekeza TBA kusimamia ukusanyaji wa madeni kwa wadaiwa sugu kulingana mikataba waliyojiwekea ili kodi hizo ziweze kukamilisha ujenzi wa jengo la tatu na nne (Block C na D) yanayoendelea katika eneo la Magomeni ambapo utekelezaji wake umefikia asilimia 15.

Aidha, amesema Serikali imerekebisha Sheria za TBA na kutoa fursa kwa kuingia ubia na sekta binafsi ili kurahisisha ushirikishwaji wa Sekta Binafsi na Taasisi za fedha kwa ajili ya uendelezaji wa milki, kuwahudumia watumishi wa umma wenye uhitaji wa makazi.

Bashungwa ameeleza kuwa ujenzi wa jengo la makazi ya watumishi wa umma la Magomeni Kota Awamu ya Pili B lililogharimu kiasi cha Shilingi Bilioni 5.6 ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya 2020 - 2025 na ni sehemu ya mkakati wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuboresha Makazi bora.

Kadhalika, Bashungwa ameipongeza TBA kwa matumizi bora ya ardhi na mipango mizuri ya majengo ya kisasa katika eneo la Magomeni lenye ekari 32,000 lililokuwa na wakazi zaidi ya 645 kwa kuweza kutumia ekari 9 kutosheleza wakazi hao.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila ameeleza kuwa Mkoa huo unatakiwa kupangwa upya kwa kuwa na mikakati ya pamoja kwa kushirikiana na Mashirika ya Kiserikali na Sekta Binafsi ili kuuwezesha Mkoa huo kuwa miongoni mwa miji mikubwa Afrika kufikia mwaka 2030.

Akitoa taarifa ya mradi, Mtendaji Mkuu wa TBA, Arch. Daud Kondoro ameeleza kuwa kazi zote katika mradi huo za ubunifu, ujenzi na usimamizi zimetekelezwa na TBA kwa kutumia Wataalam wake wenyewe kwa kuzingatia mabadiliko chanya ya ukuaji katika Sekta ya Uchumi, Mipango Miji na Teknolojia ya Ujenzi, Mawasiliano na Miundombinu.

Kondoro ameeleza kuwa jengo hilo limefungwa mfumo wa kisasa wa ‘Payless’ ambapo itakapofika wakati wa kulipa kodi ya pango na mpangaji akawa hajalipa, moja kwa moja anakosa huduma ya umeme na maji katika nyumba yake na akilipa kodi ya pango, muda huo huo huduma ya umeme na maji inarejea.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...